Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,480
- 30,152
Tumekuwa tukishuhudia kila kiongozi kabla ya kukabidhiwa madaraka, ni lazima kwanza aape na katika kiapo hicho, sharti kuu ni kuilinda na kuiheshimu Katiba ya nchi ambayo ndiyo sheria mama ya nchi yetu
Sasa ni kwanini baadhi ya viongozi Mara tu wanapoanza kutumikia nyadhifa hizo wanaipuuza Katiba ya nchi na kuiona kama takataka?
Ifahamike kuwa Katiba ya nchi ni lazima uitekeleze na kuipuuza Katiba hiyo ni sawasawa na uhaini na huyo kiongozi anastahili kushitakiwa.
Sasa ninachojiliuliza ni kwa nini baadhi ya viongozi wakubwa ambao nao wameapa kuitii na kuiheshimu Katiba hiyo wakiipuuza na kuiona kama takataka na kuisigina Katiba hiyo?
Mfano dhahiri ni kwa Spika wa Bunge letu la Jamhuri, Spika Ndugai, ambaye anajua kuwa huwezi kuwa mbunge kama umevuliwa uanachama wako na chama kilichokudhamini ubunge wako.
Spika Ndugai amesema hadharani kuwa atawalinda kwa nguvu zote wabunge wa viti maalum wa Chadema, ambao chama chao cha Chadema kimeutangazia Umma kuwa kimewavua uanachama wao.
Sasa kama Spika anaonyesha mfano mbaya kiasi hicho, wa kuamua kuisigina Katiba ya nchi kadri atakavyo, hivi huyu Spika ana nia ya kulitumbukiza Taifa hili shimoni na tusiweze tena kujikwamua?
Sasa ni kwanini baadhi ya viongozi Mara tu wanapoanza kutumikia nyadhifa hizo wanaipuuza Katiba ya nchi na kuiona kama takataka?
Ifahamike kuwa Katiba ya nchi ni lazima uitekeleze na kuipuuza Katiba hiyo ni sawasawa na uhaini na huyo kiongozi anastahili kushitakiwa.
Sasa ninachojiliuliza ni kwa nini baadhi ya viongozi wakubwa ambao nao wameapa kuitii na kuiheshimu Katiba hiyo wakiipuuza na kuiona kama takataka na kuisigina Katiba hiyo?
Mfano dhahiri ni kwa Spika wa Bunge letu la Jamhuri, Spika Ndugai, ambaye anajua kuwa huwezi kuwa mbunge kama umevuliwa uanachama wako na chama kilichokudhamini ubunge wako.
Spika Ndugai amesema hadharani kuwa atawalinda kwa nguvu zote wabunge wa viti maalum wa Chadema, ambao chama chao cha Chadema kimeutangazia Umma kuwa kimewavua uanachama wao.
Sasa kama Spika anaonyesha mfano mbaya kiasi hicho, wa kuamua kuisigina Katiba ya nchi kadri atakavyo, hivi huyu Spika ana nia ya kulitumbukiza Taifa hili shimoni na tusiweze tena kujikwamua?