Ikiwa leo hii Rais Samia anatia sahihi makubaliano ya ulinzi na usalama na Msumbiji basi kuna kitu kiliharibika hapo nyuma

Kwamba panya road tumewashindwa hadi kuingia mkataba na msumbiji ili watusaidie?kwa nini kipindi cha magu tulikisambaratisha hiki kikundi cha panya road?
 
Kama huelewi haya mambo kaa kimya. Kwani nani amekuambia hatutaki mama afanye kazi? Tatizo wengi humu JF tunaangalia mambo juu juu sana
Usilete za kuleta mkuu.
Acheni mama afanye kazi ya watanzania.

Hao askari wetu wakienda huko Msumbiji utawalisha ,kuwapa malazi na utawalipa wewe?
Na wakifa fidia kwa familia zao je?
Muwage na upeo wa kufikiri.
 
Mambo ni mengi huenda wameongeza scope ya ushirikiano..kama mafunzo, kubadilishana wafungwa, kusaidia a ulinzi n.k..lolote lawezekana
 
Eti Rwanda ndio walikuwa wanaisaidia Msumbiji kiusalama, Rwanda ka nchi kiduchu kama utitiri
 
Una tatizo kubwa la uelewa.

Nimekueleza sababu ya kutiliana sana kwenye ulinzi na usalama ni kutokana na kinachoendelea mpakani kupambana na Wanamgambo wa kiislamu(IS). Na Tanzania ilianza kuchukua hatua ikiwemo kuweka kambi kubwa huko mpakani na hata hili suala lilifika bungeni na kujadiliwa.

Huenda hata hukusoma walichoongea hawa maraisi
Pitia hapa
Kwa hiyo tuliweka kambi na sasa ndio tuna saini mkataba? Tuliweka kambi chini ya mkataba gani sasa, na huu ni kwa ajili ya nini, kuweka kambi ya pili?
 
Sio Askari ni Islamic State (IS). Bado pia wanaendelea kuingia mara moja moja japo Tz inapambana nao sana.

Kuna kambi kubwa huko imewekwa kwa ajili ya hao IS, Ila msumbiji wana jeshi dhaifu sana
Mmmh, udhaifu wa Msumbiji sidhani, japo inawezekana pia, lakini naomba nizungumzie upande wa TZ.

1. Unakumbuka suala la Uamsho? Kile kilikuwa ni kikundi cha Ugaidi dhahiri. Mbali na siasa, kimekuja kuachiwa, maana yake hatupo serious kupambana na kesi za ugaidi, na tunaona kama mataifa mengine ni vichaa tu havijui madhara ya ugaidi.

2. Unakumbuka kesi za kibiti? Hakukuwahi kushambuliwa kituo cha polisi, wakaua polisi kisha wakatokomea na silaha? Mambo ya huko yakafanywa ni siri saana na vyombo vya usalama, wakumbuka mapango ya kule Tanga? Hakukuwahi kukamatwa kesi za Ugaidi? Video mpaka Youtube hazikurushwa? As usual tunaona tuna vikosi imara, na tukaamua tukae kimya, kila kitu ni siri.

3. 2020, uchaguzi mkuu Tz. Hakuwahi kutumwa picha na video za magaidi kuua askari wa JWTZ na kuteka vifaru na silaha zingine? Tukapiga kimya, kila kitu ni siri, tuna jeshi imara. Kabla ya wale askar wa JWTZ kuuwawa, inasemakana hao magaidi walikuwepo pale Mtwara siku nyingi saaana wakifanya mauaji, yamkini ndo maana kikapelekwa kikosi cha Jeshi eneo hilo.

MAONI YANGU NI HAYA

Embu tuwe serious kwa kila kinachotamkwa kuashiria kuharibu usalama wetu, evidence imepatikana watu fulani wanahusika na ugaidi, basi sheria ifuate mkondo wake, siasa tupa pembeni.

Kama Msumbiji walikuwa wakilalamika ugaidi, tulipaswa kuimarisha mapema mno vikosi vyetu hasa mipakani, huu ugaidi huko mtwara inasemekana ni mpakani baina ya Tz na Msumbiji. Hivi ni kweli ujue jirani yako anapambana na ugaidi, ushindwe kuimarisha vikosi mipakani mpaka usubiri waingie nchini mwako? Tena wanaingia na kutoka kikundi cha watu zaidi ya 200, bora ata wangekuwa wanaingia kiraia. Sakata lilianza kama utani ila kwa sasa ni kubwa haswa. Askari yoyote wa JW ambaye amefika huko Mtwara atakuhakikishia hili, suala ni zito la ugaidi maeneo ya huko.
 
Jiwe hakufaa kuwa Rais kabisa, sipati picha mpk leo angekuwepo, tungevunja mahusiano na nchi nyingi sababu ya kiburi chake Cha kishamba
Kaka lile kabila sio la kuongoza nchi, ndo maana hayati baba wa taifa aliyapinga baadhi ya makabila, yeye aliona mbali mno. Hatujawahi kuongozwa na mtu mshamba wa madalaka sampuli ya jiwe. Sifa, kutukuzwa, kuabudiwa n.k
 
Huenda una tatizo la uelewa. Hakujawahi kuwa na tatizo Kati ya Tz na msumbiji. Kutiliana saini kwenye masuala ya ulinzi hufanyika Mara kwa Mara kulingana na hali ya kiusalama mpakani ilivyo.
Tanzania hapa tulisaini mkataba wa ulinzi na usalama na Burundi, unataka kusema pia tumewahi kuwa na tatizo na Burundi?
View attachment 2364605
Aiseeee, kuna mambo huyatambui. Kuna kipindi TZ tulishutumiwa kuuza silaha mipakani, hasa burundi. Sijui una muda gani JF, kipindi JK anaruhusu JWTZ kwenda Congo kupambana na M23, Kagame alikuja juu na kusema Tz inafadhili vikundi vya Interahamwe/FDLR ambavyo ni maadui wa Rwanda.

Sasa achana na aloongea kagame, miezi michache mbele UN ikatoa tamko la kuishutuku TZ kuvifadhili vikundi vya kiasi vilivyopo Congo, ripoti haikusema ni vikundi vipi na vina nia ipi, ila kwa maelezo yale ya kagame, tunaunganisha dots kwa kusema yamkini ni vikundi vyenye nia ya kurudi Rwanda huko mbeleni kwa mtutu.

Nachotaka nikueleze hapa ni hiki, Tz ina chembechembe za Ujamaa, ni nchi inayoendeshwa na usiri ambao kwa namna flani ni kama hauna maana kwa dunia ya sasa. Kuna mambo mengi tunafichwa kutokana na mifumo tuliyokuwa nayo, mfano hapo unakuta tunasign lakini undani wa hiyo mikataba nchi yetu inafanya kuwa ni siri zaidi.
 
Kwa hiyo tuliweka kambi na sasa ndio tuna saini mkataba? Tuliweka kambi chini ya mkataba gani sasa, na huu ni kwa ajili ya nini, kuweka kambi ya pili?
Achana nao hawana akili hao, watakusumbua bure, mambo ya kiusalama wanachukulia simple.
 
Kaka lile kabila sio la kuongoza nchi, ndo maana hayati baba wa taifa aliyapinga baadhi ya makabila, yeye aliona mbali mno. Hatujawahi kuongozwa na mtu mshamba wa madalaka sampuli ya jiwe. Sifa, kutukuzwa, kuabudiwa n.k
hatari Sana mkuu
 
Serikali yetu ya Tanzania haitilii maanani ushirikiano kati yetu na Msumbiji kiulinzi na hata kibiashara nchi inahitaji viongozi wenye mitazamo mipana ili kuimarisha usalama wa nchi na hata maendeleo ya nchi tunahitaji ushirikiano thabiti na huku tukiweka malengo ya muda mfupi na mrefu na tuyafikie kivitendo
 
Leo hii nimesoma habari kwamba Tanzania na Msumbiji tumetia sahhi makubaliano ya ulinzi na usalama. Kwanza sikuamini kama ni Msumbiji kweli, au nchi nyingine. Yaani Msumbji, ile ninayoijua mimi, ambayo maelfu ya wanajeshi wa Tanzania walikufa huko katika kuisaidia kupambana na majeshi ya uasi ya wakati huo Renamo?

Nimejiuliza, ikiwa leo hii tunatia sahihi huu mkataba, basi huko nyuma Watanzania tulifia Msumbiji chini ya kivuli gani?

Kwa wale msiojua historia, Tanzania tulipoingia vita na Uganda ya chini ya Idd Amin, Raisi Samora wa Msumbiji alileta vikosi vyake Tanzania ili viende kupigana na Idd Amin bila hata kushauriana na Nyerere! Nyerere alimkatalia Samora kupeleka askari wake Uganda, akidai ingesababisha vita kupanuka zaidi ya Uganda na Tanzania - japo baadae majeshi ya Libya yalikuja kumsaidia Idd Amin. Ikabidi askari wa Msumbiji wabaki hap Dar kulinda doria usiku. Nadhani mtakumbuka walifundishwa neno moja tu la kiswahili, "kitambulisho?"

Sasa toka ule uhusiano uliokuwapo, nini kimetokea kati yetu na Msumbiji hadi tufikie mahali pa kutiliana sahihi kusaidana ulinzi? Na pia nikakumbuka kwamba hapa juzi Msumbiji walipopata tatizo la ugaidi tena walikimbilia Rwanda kuomba msaaada sio ndugu zao wa Tanzania. Nikajiuliza kwa nini?

Je inawezekana uhusiano uliharika wakati wa serikali ya awamu iliyopita chini ya John Pombe Magufuli? Hilo ni jambo nazidi kujiuliza. Kwangu mimi kutiliana sahihi makubaliano ya ulinzi na usalama na Msumbiji ni sawa na mtu na kaka yake kutiliana sahihi makubaliano ya kusaidiana wakati wa shida! Kweli Raisi Samia hilo ni jambo mojawapo muhimu ya yaliyokupeleka Msumbiji?

Na kama kulikuwa na tatizo, basi nitasema wazi haikuwa busara kwenu Raisi Samia na Raisi Nyusi wa Msumbiji kulitangaza hili hadharani. Lingejadiliwa kimya kimya kati ya dada na kaka.

Reference: Tanzania, Msumbiji zatiliana saini ulinzi na usalama
Yule mtu mlikuwa mnamuita Rais alikuwa na matatizo makubwa kichwani na aliharibu kila mahala na kugombana na kila jirani.
 
IKiwa ndivyo basi Raisi Samia na Raisi Nyusi watakuwa wamefanya jambo bila busara. Walipaswa kujadili hili jambo kimya kimya bila kutanganza hadharani kutiliana sahihi mkatana wa ulinzi na usalama. Wao ni dada na kaka kwa jinsi tulivyo Msumbiji na Tanzania
Hakuna kosa,mambo yote ya amani huwa yanasemwa wazi hivi hivi..

Ukweli ni kwamba kulikuwa na kutoelewana kwa Tanzania na Msumbiji.
 
Back
Top Bottom