Elections 2010 Ikiwa hatutambui matokeo kuna haja gani wabunge waapishwe?

Sokomoko

JF-Expert Member
Mar 29, 2008
1,915
127
Tangu matokeo yatangazwe kwa ujumla nimekuwa ninajiuliza maswali mengi sana moja wapo kama wapinzani na wanamapinduzi hawaikubali tume na kwa mfano chadema na dr slaa wamegomea matokeo kuna ulazima kweli wa kuwapeleka wabunge bungeni? kama upo kwanini? na kwanini iwe sitaki nataka? Naomba tusiwe wanafiki hapa kama umeamua kuoga basi huna budi kuvua nguo na ukishayavulia maji nguo huna budi kuyaoga. Chadema na Slaa waamue moja kukataa matokeo na kushinikiza wabunge wao wasiingie bungeni nadhani dunia itasikia na sio kwa chadema tu hata vyama vingine vya upinzani! sio kukaa kipembeni unalalamika huku unakula posho wakati sisi watanzania wa kawaida tukiumia na ugumu wa maisha.

Mtafakari tusikubali kutumiwa jamaniiiiiiiii
 
:smile-big::smile-big::smile-big: weee komea hapo? Ubunge walioupigania vile waukatae??? kwani ulisikia mahala wamepigana kwa sababu ya u-Rais???
 
kweli kabisa, kama kweli CHADEMA wanadai Matokeo yamechakachuliwa wasiwaruhusu wabunge wao kwenda kuapishwa, yaani wakithubutu kufanya hivi mimi na familia yangu wote waliotimiza miaka 18 wote tunakuja kuchukua kadi za CHADEMA.
 
kama ilivyo jadi yenu. mtawatisha hadi watoto wenu!!! hatutishiki ng'oooooooooooooooooooooooooooooo!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom