Ikitokea Rais Samia akakemea kufungwa kanisa la Gwajima na kutengua uteuzi wa Bashungwa CCM hawatamsifia?

Ikitokea Rais Samia akakemea kufungwa kanisa la Gwajima na kutengua uteuzi wa Bashungwa CCM hawatamsifia?

Mudawote

JF-Expert Member
Joined
Jul 10, 2013
Posts
11,569
Reaction score
16,027
GTs,
Hebu fikiria tu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amekemea vikali hatua ya kufungiwa kwa Kanisa la Ufufuo na Uzima inayoongozwa na Askofu Josephat Gwajima, akieleza kuwa ni ukiukwaji wa haki ya kuabudu inayolindwa na Katiba. Hebu fikiria tu akizungumza haya yote akiwa katika ziara ya kikazi jijini Dar es Salaam, Rais Dkt Samia alieleza kushangazwa na uamuzi huo wa mamlaka bila kujumuisha majadiliano ya wazi na viongozi wa dini. Rais alisisitiza kuwa serikali yake inaheshimu uhuru wa kidini na haitavumilia matumizi mabaya ya madaraka kwa kuzuia watu kushiriki ibada zao kwa misingi isiyoeleweka.

Katika hatua nyingine, Rais Dkt Samia ametengua uteuzi wa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi kufuatia kushindwa kwake kushughulikia matukio ya utekwaji wa watu yanayoendelea kushika kasi nchini. Dkt. Samia alisema serikali haiwezi kufumbia macho vitendo vya kihalifu vinavyohatarisha usalama wa raia na kuvuruga amani ya nchi. Aliahidi kuchukua hatua kali kwa watendaji wote wa umma wanaoshindwa kutimiza majukumu yao ipasavyo, akisisitiza kuwa suala la utekaji halitavumiliwa na linahitaji hatua za haraka na za kimkakati kutoka kwa vyombo vya usalama.

Wadau nimewaza hivyo, je ikitokea Rais Dkt Samia kafanya hivyo CCM viherehere hawataitisha press kumsifia Rais Dkt Samia? Je wana JF tutamsifia?
 
GTs,
Hebu fikiria tu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amekemea vikali hatua ya kufungiwa kwa Kanisa la Ufufuo na Uzima inayoongozwa na Askofu Josephat Gwajima, akieleza kuwa ni ukiukwaji wa haki ya kuabudu inayolindwa na Katiba. Hebu fikiria tu akizungumza haya yote akiwa katika ziara ya kikazi jijini Dar es Salaam, Rais Dkt Samia alieleza kushangazwa na uamuzi huo wa mamlaka bila kujumuisha majadiliano ya wazi na viongozi wa dini. Rais alisisitiza kuwa serikali yake inaheshimu uhuru wa kidini na haitavumilia matumizi mabaya ya madaraka kwa kuzuia watu kushiriki ibada zao kwa misingi isiyoeleweka.

Katika hatua nyingine, Rais Dkt Samia ametengua uteuzi wa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi kufuatia kushindwa kwake kushughulikia matukio ya utekwaji wa watu yanayoendelea kushika kasi nchini. Dkt. Samia alisema serikali haiwezi kufumbia macho vitendo vya kihalifu vinavyohatarisha usalama wa raia na kuvuruga amani ya nchi. Aliahidi kuchukua hatua kali kwa watendaji wote wa umma wanaoshindwa kutimiza majukumu yao ipasavyo, akisisitiza kuwa suala la utekaji halitavumiliwa na linahitaji hatua za haraka na za kimkakati kutoka kwa vyombo vya usalama.

Wadau nimewaza hivyo, je ikitokea Rais Dkt Samia kafanya hivyo CCM viherehere hawataitisha press kumsifia Rais Dkt Samia? Je wana JF tutamsifia?


Utekaji ni msimamo wa Chama cha Mauaji .

Mwana CCM yeyote ni lazima aunge mkono suala la utekaji .
Ukipinga utekaji unaachwa nje au unatekwa au kufunguliwa kesi kwa sababu unapingana na msimamo wa Chama na Serikali.

Tumeibiwa vya kutosha
Tumepandishiwa bei vya kutosha
Tumewekewa vikokotoo vya kutosha
Watu wetu wametekwa vya kutosha Watu wetu wameuawa vya kutosha
Wapiga kura wamedharauliwa vya kutosha
Dini zimedharauliwa vya kutosha
Watu wamebambikiwa kesi vya kutosha
Bunge limekua la hovyo vya kutosha
Madiwani wamekuwa wapiga dili vya kutosha
Mawaziri wamejilimbikizia mali vya kutosha
Viongozi wa dini wauawa vya kutosha.
Rais amekua dikteta vya kutosha
Vyombo vya dola vimeipendelea CCM vya kutosha .

Uwezo wa kuiondoa CCM makarakani tunao .
Sababu ya kuindoa CCM madarakani tunayo .
Nia ya kuiondoa CCM madarakani tunayo


Sasa watanzania tuna kazi moja tu kuzuia bunge lisivunjwe na uchaguzi usifanyike bila marekebisho ya tume ya uchaguzi .
 
HEHEHEHEeeeeenHEEEEEnHeeeeee1

Wacha tu nicheke miye!

Hii sinema au komedi?

Mbona amechelewa sana!

Kama anataka hata sisi wengine tuanze kumtazama tena; afanye lililo la muhimu zaidi kwa sasa hivi kwa nchi yetu hii.

Kesho asubuhi aitishe kikao na waandishi wa habari, aseme waziwazi kuwa "Marekebisho ya taratibu za uchaguzi ni lazima zifanyike kabla ya uchaguzi wowote kufanyika ndani ya nchi hii.

Akitamka hayo, nasamehe mengine yote, isipokuwa waTanzania wakiopotezwa, walioteswa, waliouawa, ni lazima uchunguzi wa kina ufanyike, na ijulikane ni nani wahusika wa uovu huo.

Huyo aliyetumbuliwa alicheleweshwa sana. Huyo mtu ni taahira wa aina yake.
 
GTs,
Hebu fikiria tu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amekemea vikali hatua ya kufungiwa kwa Kanisa la Ufufuo na Uzima inayoongozwa na Askofu Josephat Gwajima, akieleza kuwa ni ukiukwaji wa haki ya kuabudu inayolindwa na Katiba. Hebu fikiria tu akizungumza haya yote akiwa katika ziara ya kikazi jijini Dar es Salaam, Rais Dkt Samia alieleza kushangazwa na uamuzi huo wa mamlaka bila kujumuisha majadiliano ya wazi na viongozi wa dini. Rais alisisitiza kuwa serikali yake inaheshimu uhuru wa kidini na haitavumilia matumizi mabaya ya madaraka kwa kuzuia watu kushiriki ibada zao kwa misingi isiyoeleweka.

Katika hatua nyingine, Rais Dkt Samia ametengua uteuzi wa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi kufuatia kushindwa kwake kushughulikia matukio ya utekwaji wa watu yanayoendelea kushika kasi nchini. Dkt. Samia alisema serikali haiwezi kufumbia macho vitendo vya kihalifu vinavyohatarisha usalama wa raia na kuvuruga amani ya nchi. Aliahidi kuchukua hatua kali kwa watendaji wote wa umma wanaoshindwa kutimiza majukumu yao ipasavyo, akisisitiza kuwa suala la utekaji halitavumiliwa na linahitaji hatua za haraka na za kimkakati kutoka kwa vyombo vya usalama.

Wadau nimewaza hivyo, je ikitokea Rais Dkt Samia kafanya hivyo CCM viherehere hawataitisha press kumsifia Rais Dkt Samia? Je wana JF tutamsifia?
Samia wa nchi ya kusadikika?
 
Back
Top Bottom