MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,011
- 16,748
Leo Krav Maga niliamua kujipa tu Kazi binafsi ya kupitia Maamuzi ya Uchunguzi ya waliowahi kuwa Viongozi Serikalini katika Tawala mbalimbali ili Kujiridhisha na hili la aliyekuwa DC wa Moshi Ole Sabaya.
Nilichokigundua tu ni kwamba kati ya Watu kama nane ambao Marais waliwasimamisha Kazi kupisha Uchunguzi wote nane hao baadae walikuja Kuonekana hawana Hatia tena kuna wengine sasa wapo Kazini baada ya Kurejeshwa.
Hivyo basi kufuatia utaratibu huu naanza kuona kuwa hata huyo Ole Sabaya nae ambao Sisi Wababe wa Mitandao ( Keyboard Warriors ) tumekesha Kumshambulia, Kumcheka na Kumdhihaki kwa kila namna huenda nae akaja Kusafishika na Kutakata vyema na Sabuni nzuri ya Haki na tukakosa sehemu ya Kuficha Misura ( Minyago ) yetu iliyokomaa kama Kuta za Jengo la Tanganyika Packers Kawe.
Kwa mbali sana naanza Kuhisi hiki kilichomtokea DC Ole Sabaya ni Mchezo tu uliopangika vyema ili Kucheza na Akili za Watanzania wengi wanaopenda Mihemko, Matukio na ambao baadhi yao ( yetu ) wana ( tuna ) Mioyo iliyojaa Wivu ( Visununu ) tupu.
Nitaanza rasmi Kutowaamini Wanasiasa.
Nilichokigundua tu ni kwamba kati ya Watu kama nane ambao Marais waliwasimamisha Kazi kupisha Uchunguzi wote nane hao baadae walikuja Kuonekana hawana Hatia tena kuna wengine sasa wapo Kazini baada ya Kurejeshwa.
Hivyo basi kufuatia utaratibu huu naanza kuona kuwa hata huyo Ole Sabaya nae ambao Sisi Wababe wa Mitandao ( Keyboard Warriors ) tumekesha Kumshambulia, Kumcheka na Kumdhihaki kwa kila namna huenda nae akaja Kusafishika na Kutakata vyema na Sabuni nzuri ya Haki na tukakosa sehemu ya Kuficha Misura ( Minyago ) yetu iliyokomaa kama Kuta za Jengo la Tanganyika Packers Kawe.
Kwa mbali sana naanza Kuhisi hiki kilichomtokea DC Ole Sabaya ni Mchezo tu uliopangika vyema ili Kucheza na Akili za Watanzania wengi wanaopenda Mihemko, Matukio na ambao baadhi yao ( yetu ) wana ( tuna ) Mioyo iliyojaa Wivu ( Visununu ) tupu.
Nitaanza rasmi Kutowaamini Wanasiasa.