Ikimpendeza Mh. Rais aongoze maridhiano ya kitaifa. Ni muhimu kwa ustawi wa Taifa leo na kesho

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
1572522400334.png
Ki msingi siasa za ushindani hazipaswi kuwa ugomvi ijapokuwa kuna wakati zinageuka kuwa kama ugomvi mkubwa na hii hutokea kwenye nchi mbalimbali duniani.Hata hivyo hali inapokuwa hivyo kwenye nchi yoyote sio jambo zuri sana.

Siasa za ushindani zinapogeuka kuwa kama ugomvi; mara nyingi mwisho wake unakuwa haupendezi sana. Katika mazingira mengine inaweza kusababisha changamoto kubwa kuliko ambavyo watu wanaweza kudhania kabla.

Inavyoonekana ni kama siasa za ushindani Tanzania zina hako ka muelekeo ka kukaa ki ‘Ugomvi’ na tunaweza kukubaliana kamba “kama muelekeo huo upo” sio mzuri na wakushabikia.Sifikiri kama ikiwa uhusiano uliopo sio mzuri kweli, kuna anayeweza kuamini kwa dhati kabisa kama yeye ananufaika na hilo.

Tunaweza kushauri kuwa, itakuwa ni jambo zuri na muhimu kama Mh. Rais ataona inafaa na kuamua kuitisha maridhiano ya kitaifa.

Kwenye maridhiano hayo kusiwe na vyombo vya habari, viongozi wa vyama vyote waalikwe, wajifungie mahali, kila mwenye lake aseme, anayeona kadhulumiwa mahali afunguke, anayeona amekosewa aseme, anayeona mwenzake kakosea mahali fulani aambiwe; yaani iwe ni kuambiana ukweli.

Baada ya hapo kila mmoja atakuwa katua mizigo aliyo nayo na baada ya hapo yanafanyika maridhiano na kufanya makubaliano kwenye mambo ya msingi juu ya ni nini tunataka, ni nini hatutaki na wapi tunakotaka kwenda kama taifa.

Moja ya mambo ambayo ni vizuri kuwa na muafaka wa kitaifa ni pamoja na ikiwa tunataka demokrasia ama hatutaki, na kama tunataka demokrasia ya namna gani na ni kivipi itekelezwe.

Baada ya maridhiano hayo, itakuwa sasa ni muhimu kila mmoja kutekeleza maridhiano kwa utashi wake mwenyewe. Ikumbukwe ijapokuwa kuwa tuna Katiba na sheria, ila “Utashi wa kisiasa “ ni muhimu sana kwenye kufanikisha karibu kila jambo. Naamini jambo hilo litakuwa la faida kwa wote na hakuna atakayepoteza bali kama nchi tutakuwa tumeshinda wote kwa pamoja.

Ni kweli kwamba wapinzani wa Tanzania wana mapungufu mengi, lakini tukumbuke kuwa nao ni binadamu na ni sehemu ya watanzania hawa hawa ambao tunajijua vizuri sana tulivyo.

Hata hivyo pamoja na mapungufu yao, lakini bado ni watanzania na kuna mahali wanaweza kusaidia. Unaweza hata kukutana na mtu mwenye uwezo mdogo labda kwenye kila kitu, ila angalau akakuambia huko unakoenda nimetoka huko, kuna nyoka kwa hiyo pita pembeni. Kwa hiyo licha ya uwezo wake mdogo, lakini anakuwa amekusaidia pengine kuokoa maisha yako.

Kwa hiyo pamoja na matatizo waliyo nayo, bado wanaweza kusaidia kitu flani , wakati fulani na mahali fulani na mwisho wa siku bado ni wanajamii na Watanzania.

Uzuri pia ni kwamba Mh. Magufuli ni ‘Optimist’, anaangalia ni lipi lenye faida zaidi na ndilo analofanya, na hili tumeliona kwenye kuwasamehe wenye kesi za ufisadi kwa masharti ya kulipa wanachodaiwa kwa kuamini kuwa;kufanya hivyo ni faida kwa wahusika lakini pia faida kwa taifa. Kimsingi kama hilo kaliweza kwa maslahi ya taifa, akiamua hili ni jambo dogo sana kwake kulifanikisha, na kwa kuwa lina faida kuliko hasara; bila shaka ataona umuhimu wake.

Kadhalika, kwa uelwa wake mzuri juu ya dhana hii ya ushirikishwaji, kutoa nafasi ya kila mtu kusema ya moyoni na baadae kufanya maridhiano; mara kadhaa tumeshuhudia akiyafanya haya na makundi mbalimbali ikiwepo wafanya biashara. Kwa hiyo hili nalo linaweza kuwa zuri vilevile.

Kama Mandela aliweza kufanya kikao cha kuelezana ukweli na maridhiano na wana Afrika kusini wakasamehena na kuridhiana licha ya makorokoro yote waliyofanyiana, Tanzania tunayo nafasi nzuri sana katika hili kwa sababu hatuna tatizo kubwa la kutisha kimahusiano.

Wasiwasi ni kwamba, chuki huwa ina tabia ya kuingia kwa haraka kwenye nafsi ya binadamu lakini ni ngumu sana kutoka. Kwa hiyo inapowezekana kuizuia kuingia; ni bora kufanya hivyo hasa kama gharama yake sio kubwa sana, maana ikitokea watu wakianza kuchukiana wenyewe kwa wenyewe watakuwa pia wanatafuta namna ya kuhujumiana wenyewe kwa wenyewe, na watu wakiwa wanahujumiana wenyewe kwa wenyewe, ni rahisi na maadui wa pembeni kutumia mwanya huo huo kuchomekea mokorokoro.

Samahani kwa yoyote atakayekuwa amekwazika kwa kusoma mambo mengi maana wengi hili linawakwaza.
 
Rais anatekeleza Ilani ya CCM 2015 - 2020. Kama ina hiyo hoja [ya MARIDHIANO] sawa ila kama haina utakuwa unampotosha. Hawezi kufanya kitu ambacho hakutumwa kufanya na alichotumwa kufanya ni kutekeleza Ilani.
 
Rais anatekeleza Ilani ya CCM 2015 - 2020. Kama ina hiyo hoja [ya MARIDHIANO] sawa ila kama haina utakuwa unampotosha. Hawezi kufanya kitu ambacho hakutumwa kufanya na alichotumwa kufanya ni kutekeleza Ilani.
Mkuu, Tuna Katiba, Tuna sheria , Tuna ilani lakini kuna changamoto ambazo zinajigtokeza zinahitaji kitu Zaidi ya hivyo, Busara!. Ndio maana tuna viongozi. Hilo ni muhimu sana. Hayo unayosema utekelezeji wake sio lazima kiongozi, heta meneja ukimpa orodha ya vitu vya kutekeleza vilivyoandikwa mahali, na rasilimali atatekeleza. Kiongozi anafanya zaidi ya yaliyoandikwa. MH. Rais ni kiongozi, sio meneja.
 
Dawa ni kutengeneza serikali ya mseto vyama vyote vyenye wabunge bungeni viwe na watu wa kuunda serikali ndio dawa wa aya yote.

Chama kimepata kura mil 6 halafu eti hakishirikishwi kwa chochote unategemea nini kula mil 6 ata nusu ya watu wakiamua kuingi barabarani wote mnajua nini kitatoke.
 
Tanzania tumefikia hatua hiyo kweli? Sidhani.
Hatua gani?Nadhani kama unachotaka kusema unaamini ni sahihi na muhimu na ingependeza ungeeleza vizuri ueleweke unazungumzia nini.
Otherwise unaweza kuboresha mawazo where appropriate.
 
Rais anatekeleza Ilani ya CCM 2015 - 2020. Kama ina hiyo hoja [ya MARIDHIANO] sawa ila kama haina utakuwa unampotosha. Hawezi kufanya kitu ambacho hakutumwa kufanya na alichotumwa kufanya ni kutekeleza Ilani.
Simpingi wala kumuunga mkono mleta uzi lakini nakwazwa na hii hoja yako. Flexibility ni njia nzuri ya kwenda nayo naama maisha hayana formular na ni wazi kuwa sio yote yaliyopangwa 2015 yartatokea kama yalivyotarajiwa, mfano uharibifu uliosababishwa na mafuriko huko Tanga na kwingineko huwezi kusema hatushughuliki navyo kwa sababu havikuandikwa kwenye irani!.
Mbali na hapo tutasema itani ya uchaguzi ya ccm 2015-2020 ni a perfect document kuzidi hata Misahafu!
 
Dawa ni kutengeneza serikali ya mseto vyama vyote vyenye wabunge bungeni viwe na watu wa kuunda serikali ndio dawa wa aya yote.

Chama kimepata kura mil 6 halafu eti hakishirikishwi kwa chochote unategemea nini kula mil 6 ata nusu ya watu wakiamua kuingi barabarani wote mnajua nini kitatoke.
Moja ya mambo ambayo tunatakiwa tujaribu kuyafikiria ni kupunguza siasa za madaraka. Hata sasa moja ya kitu kinacholeta shida kubwa ni hicho. Hivi mtu akishajua kwamba unachotaka ni madaraka tu na ikiwezekana hata kumtoa yeye uingie wewe, hivi unafikiri hata ukijenga hoja nzuri kiasi gani mtaaminiana, na unadhani akiwa na uwezo wa kukudhibiti ataacha?

Kuhusu hilo la kuingia mtaani hilo halipo wala halitegemiwi kuwezekana na wala hatushauri maridhiano yaongozwe kwa misingi ya woga wa kuogopa mtu flani.

Ukisema hivyo unaharibu kila kitu. Maridhiano yanaongozwa na msingi wa kwamba watanzania ni wamoja na wanataka kwenda mbele kwa mshikamano na kupata matokeo bora Zaidi, na ili kulifanikisha hilo, ni lazima pawe na mambo kadhaa ya msingi ambayo watu wanakubaliana. Ila ukileta dhana ya kwamba iwe nani anamuogopa nani inaharibu kila kitu.
 
Simpingi wala kumuunga mkono mleta uzi lakini nakwazwa na hii hoja yako. Flexibility ni njia nzuri ya kwenda nayo naama maisha hayana formular na ni wazi kuwa sio yote yaliyopangwa 2015 yartatokea kama yalivyotarajiwa, mfano uharibifu uliosababishwa na mafuriko huko Tanga na kwingineko huwezi kusema hatushughuliki navyo kwa sababu havikuandikwa kwenye irani!.
Mbali na hapo tutasema itani ya uchaguzi ya ccm 2015-2020 ni a perfect document kuzidi hata Misahafu!
Ni kweli. Miongozo ipo ili ifuatwe ila haina maana kwamba kwa mwenye uwezo asifanye zaidi kama kuna jambo zuri za ziada anaweza kulifanya.

Pia flexibility kama ulivyosema ni jambo zuri maana mazingira na matukio wakati mwingine hutokea kinyume na matarajio.
 
Rais anatekeleza Ilani ya CCM 2015 - 2020. Kama ina hiyo hoja [ya MARIDHIANO] sawa ila kama haina utakuwa unampotosha. Hawezi kufanya kitu ambacho hakutumwa kufanya na alichotumwa kufanya ni kutekeleza Ilani.
Yapo mambo mengi ambayo rais anayafanya kwasasa na hayapo kwenye ILANI ya ccm, mfano, tafuta KOTE, hakuna sehemu kwenye ilani ya ccm kuna kitu kama NDEGE au ATC, hakuna, tafuta kwenye Ilani ya ccm kama kuna kitu UMEME au stigilazi JOJI, pia hakuna but rais ka inject pesa nyingi sana kwenye hiyo miradi. Kihistoria, since mfumo wa vyama vingi unaanza, rais anaeingia madarakani kwa muhula wake wa kwanza is like huaga hashirikishwi kwenye uandaaji wa ILANI ya chama chake, refer malalamiko ya Mkapa mwaka 1997 kwamba ILANI ya ccm haitekelezeki, yeye aliamua kujikita kwenye barabara na miundo mbinu mingine ili hali Ilani ya chama chake was silence about it, mwaka 2006 Kikwete nae alilalamikia ILANI ya ccm hasa kwenye kile kipengere cha Kadhi wa Waislamu kwamba yeye wala hakushirikishwa, tena alilalamikia kanisani nadhani ilikua Lutherani, again kwenye uchaguzi wa 2010 hakukua na kitu kinaitwa "KATIBA" mpya but Kikwete alijaribu, alipata shida sana kwenye chama chake but aliendelea tu hadi baadae kelele za chama chake zilivyo kua kubwa nae akachemka, so Ilani sio msahafu, tunazo historia
 
Ki msingi siasa za ushindani hazipaswi kuwa ugomvi ijapokuwa kuna wakati zinageuka kuwa kama ugomvi mkubwa na hii hutokea kwenye nchi mbalimbali duniani.Hata hivyo hali inapokuwa hivyo kwenye nchi yoyote sio jambo zuri sana.

Siasa za ushindani zinapogeuka kuwa kama ugomvi; mara nyingi mwisho wake unakuwa haupendezi sana. Katika mazingira mengine inaweza kusababisha changamoto kubwa kuliko ambavyo watu wanaweza kudhania kabla.

Inavyoonekana ni kama siasa za ushindani Tanzania zina hako ka muelekeo ka kukaa ki ‘Ugomvi’ na tunaweza kukubaliana kamba “kama muelekeo huo upo” sio mzuri na wakushabikia.Sifikiri kama ikiwa uhusiano uliopo sio mzuri kweli, kuna anayeweza kuamini kwa dhati kabisa kama yeye ananufaika na hilo.

Tunaweza kushauri kuwa, itakuwa ni jambo zuri na muhimu kama Mh. Rais ataona inafaa na kuamua kuitisha maridhiano ya kitaifa.

Kwenye maridhiano hayo kusiwe na vyombo vya habari, viongozi wa vyama vyote waalikwe, wajifungie mahali, kila mwenye lake aseme, anayeona kadhulumiwa mahali afunguke, anayeona amekosewa aseme, anayeona mwenzake kakosea mahali fulani aambiwe; yaani iwe ni kuambiana ukweli.

Baada ya hapo kila mmoja atakuwa katua mizigo aliyo nayo na baada ya hapo yanafanyika maridhiano na kufanya makubaliano kwenye mambo ya msingi juu ya ni nini tunataka, ni nini hatutaki na wapi tunakotaka kwenda kama taifa.

Moja ya mambo ambayo ni vizuri kuwa na muafaka wa kitaifa ni pamoja na ikiwa tunataka demokrasia ama hatutaki, na kama tunataka demokrasia ya namna gani na ni kivipi itekelezwe.

Baada ya maridhiano hayo, itakuwa sasa ni muhimu kila mmoja kutekeleza maridhiano kwa utashi wake mwenyewe. Ikumbukwe ijapokuwa kuwa tuna Katiba na sheria, ila “Utashi wa kisiasa “ ni muhimu sana kwenye kufanikisha karibu kila jambo. Naamini jambo hilo litakuwa la faida kwa wote na hakuna atakayepoteza bali kama nchi tutakuwa tumeshinda wote kwa pamoja.

Ni kweli kwamba wapinzani wa Tanzania wana mapungufu mengi, lakini tukumbuke kuwa nao ni binadamu na ni sehemu ya watanzania hawa hawa ambao tunajijua vizuri sana tulivyo.

Hata hivyo pamoja na mapungufu yao, lakini bado ni watanzania na kuna mahali wanaweza kusaidia. Unaweza hata kukutana na mtu mwenye uwezo mdogo labda kwenye kila kitu, ila angalau akakuambia huko unakoenda nimetoka huko, kuna nyoka kwa hiyo pita pembeni. Kwa hiyo licha ya uwezo wake mdogo, lakini anakuwa amekusaidia pengine kuokoa maisha yako.

Kwa hiyo pamoja na matatizo waliyo nayo, bado wanaweza kusaidia kitu flani , wakati fulani na mahali fulani na mwisho wa siku bado ni wanajamii na Watanzania.

Uzuri pia ni kwamba Mh. Magufuli ni ‘Optimist’, anaangalia ni lipi lenye faida zaidi na ndilo analofanya, na hili tumeliona kwenye kuwasamehe wenye kesi za ufisadi kwa masharti ya kulipa wanachodaiwa kwa kuamini kuwa;kufanya hivyo ni faida kwa wahusika lakini pia faida kwa taifa. Kimsingi kama hilo kaliweza kwa maslahi ya taifa, akiamua hili ni jambo dogo sana kwake kulifanikisha, na kwa kuwa lina faida kuliko hasara; bila shaka ataona umuhimu wake.

Kadhalika, kwa uelwa wake mzuri juu ya dhana hii ya ushirikishwaji, kutoa nafasi ya kila mtu kusema ya moyoni na baadae kufanya maridhiano; mara kadhaa tumeshuhudia akiyafanya haya na makundi mbalimbali ikiwepo wafanya biashara. Kwa hiyo hili nalo linaweza kuwa zuri vilevile.

Kama Mandela aliweza kufanya kikao cha kuelezana ukweli na maridhiano na wana Afrika kusini wakasamehena na kuridhiana licha ya makorokoro yote waliyofanyiana, Tanzania tunayo nafasi nzuri sana katika hili kwa sababu hatuna tatizo kubwa la kutisha kimahusiano.

Wasiwasi ni kwamba, chuki huwa ina tabia ya kuingia kwa haraka kwenye nafsi ya binadamu lakini ni ngumu sana kutoka. Kwa hiyo inapowezekana kuizuia kuingia; ni bora kufanya hivyo hasa kama gharama yake sio kubwa sana, maana ikitokea watu wakianza kuchukiana wenyewe kwa wenyewe watakuwa pia wanatafuta namna ya kuhujumiana wenyewe kwa wenyewe, na watu wakiwa wanahujumiana wenyewe kwa wenyewe, ni rahisi na maadui wa pembeni kutumia mwanya huo huo kuchomekea mokorokoro.

Samahani kwa yoyote atakayekuwa amekwazika kwa kusoma mambo mengi maana wengi hili linawakwaza.
Hoja ni ya msingi sana ila wale mashabik wa ccm wanaotanguliza maslai ya chama mbele kuliko Tanzania watakutukana but people say " when people are silence is when it becomes worst dangerous "
 
Tanzania tumefikia hatua hiyo kweli? Sidhani.
Hatua gani?Nadhani kama unachotaka kusema unaamini ni sahihi na muhimu na ingependeza ungeeleza vizuri ueleweke unazungumzia nini.
Otherwise unaweza kuboresha mawazo where appropriate.
 
Simpingi wala kumuunga mkono mleta uzi lakini nakwazwa na hii hoja yako. Flexibility ni njia nzuri ya kwenda nayo naama maisha hayana formular na ni wazi kuwa sio yote yaliyopangwa 2015 yartatokea kama yalivyotarajiwa, mfano uharibifu uliosababishwa na mafuriko huko Tanga na kwingineko huwezi kusema hatushughuliki navyo kwa sababu havikuandikwa kwenye irani!.
Mbali na hapo tutasema itani ya uchaguzi ya ccm 2015-2020 ni a perfect document kuzidi hata Misahafu!
Mkuu kama unaijua CCM vizuri probably utajua nilichomaanisha.
 
Mkuu kama unaijua CCM vizuri probably utajua nilichomaanisha.
Ninachoamini ni kwamba changamoto ni nyingi lakini haimaanishi kuwa vitu haviwezekani. Ukilinganisha na sehemu nyingine, Tanzania bado tuna mazingira Rafiki sana ya kufanya vitu vizuri na vikubwa kama tukiamua.

Kwenye Maisha changamoto hazikosekani na hazitakosekana, la msingi ni kuangalia positive possibilities katikati ya changamoto zilizopo.

Mwisho wa siku sisi ni watanzania, uimara wetu na udhaifu wetu tunaujua vizuri, lakini hiyo si sababu ya msingi ya kukwepa kufikiria na kufanya mambo ambayo tunaamini ni mazuri kwa hofu ambayo inaweza isiwe halisia.
 
Yapo mambo mengi ambayo rais anayafanya kwasasa na hayapo kwenye ILANI ya ccm, mfano, tafuta KOTE, hakuna sehemu kwenye ilani ya ccm kuna kitu kama NDEGE au ATC, hakuna, tafuta kwenye Ilani ya ccm kama kuna kitu UMEME au stigilazi JOJI, pia hakuna but rais ka inject pesa nyingi sana kwenye hiyo miradi. Kihistoria, since mfumo wa vyama vingi unaanza, rais anaeingia madarakani kwa muhula wake wa kwanza is like huaga hashirikishwi kwenye uandaaji wa ILANI ya chama chake, refer malalamiko ya Mkapa mwaka 1997 kwamba ILANI ya ccm haitekelezeki, yeye aliamua kujikita kwenye barabara na miundo mbinu mingine ili hali Ilani ya chama chake was silence about it, mwaka 2006 Kikwete nae alilalamikia ILANI ya ccm hasa kwenye kile kipengere cha Kadhi wa Waislamu kwamba yeye wala hakushirikishwa, tena alilalamikia kanisani nadhani ilikua Lutherani, again kwenye uchaguzi wa 2010 hakukua na kitu kinaitwa "KATIBA" mpya but Kikwete alijaribu, alipata shida sana kwenye chama chake but aliendelea tu hadi baadae kelele za chama chake zilivyo kua kubwa nae akachemka, so Ilani sio msahafu, tunazo historia
Asante kwa hoja nzuri! Post yangu niliiweka nikiwa nimevaa mawani ya kijani Mkuu; kwamba ni namna gani wazo la mleta mada litatazamwa from kijani perspective.
 
Asante kwa hoja nzuri! Post yangu niliiweka nikiwa nimevaa mawani ya kijani Mkuu; kwamba ni namna gani wazo la mleta mada litatazamwa from kijani perspective.
Usidhanie mtu vibaya kabla hajatenda ubaya. Unatakiwa umdhanie vizuri au uwe nutral, akitenda ubaya na ukahakikisha kashatenda na ukajiridhisha katenda kwa makusudi hapo sawa.

Nasema hivi kwa sababu mara nyingi vitu tunavyodhania huwa ni tofauti na ukweli (Hasa vitu vibaya). Unaweza kukutana na mtu ukadhani anakuwazia mabaya kumbe wala hata hana shida na wewe, hata kama kakunja uso ni stress zake tu wala hata hakufikirii wewe. Mfano mzuri zaidi kuuelewa, ni mara ngapi ushawahi kudhani kuna mtu kajificha uvunguni mwa kitanda chako ila toka uanze kuhisi hivyo unachungulia kila siku na hujawahi kumuona?
 
CCM haijawahi kuridhia uwepo wa vyama thabiti vya upinzani vya kisiasa dhidi yake. Kuanzishwa mfumo wa vyama vingi ilikuwa ni busara za Baba wa Taifa. Viongozi wote waliowahi kutawala chini ya mfumo hawakuuridhia kwa dhati toka mioyoni mwao, isipokuwa kutokana na matakwa ya mataifa yenye ufadhiri wa misaada ya maendeleo na mashirika ya kimataifa.

Mtoa mada pamoja na kujali kwako matumizi sahihi ya rasilimali watu zilizopo ndani taifa letu pasipo kujali milengo yenye kufungamana na itikadi za vyama, lkn nikwambie ukweli hakuna chama kilichojaa makada wenye maono mafupi kama wa chama tawala ktk nyakati hizi. Wewe jaribu kufikiria kila tukio la kitaifa, wao huona fahari kuvaa mavazi yao na kuwabeza wapinzani.

Hawajali kabisa athari za maneno na matendo yao yenye kujaa ubaguzi na huku wakionyesha chuki za wazi, hawajali kabisa kwa kupuuzia weledi, maarifa na ujuzi wa kufanya kazi, vikiwa ndivyo vigezo muhimu ktk utendaji wa kazi nyeti za taifa letu, kugawana wao vyeo kwa sifa za ukada hata kama kada husika ana sifa mbovu za kimaadili.

Kibaya zaidi ni pale wanapo kusanyana ktk vikao haramu na kupeana maelekezo ya kupindisha haki na sheria ili kukandamiza uhuru na demokrasia, hasa ktk kyzuia watu kufanya maamuzi wanayoyapenda. Endapo utaona wanafungamana na mpinzani, hapo ujue wame "set fake stage" ili kujenga ghiriba ktk sura za kimataifa. Hawana nia wala hamu ya kufanya hivyo, kwa kuwa wanatambua wakithubutu umahiri wa vichwa vya upinzani utaonekana kwa dhahiri kabisa.
 
Back
Top Bottom