Ijuwe siri na faida kwa mabank kukusanya taarifa za wateja yani [ kyc]

TumainiEl

JF-Expert Member
Jan 13, 2010
6,188
11,219
Hivi karibuni watu wengi wamekuwa na maaswali yasio kuwa naa majibu baada yakuona wanaambiwa kuleta taarifa zao upya. Nilazima mimi na wewe tujuwe kwanini huu mpango umekuja kwa nguvu na nini faida zake kwetu na hata taifa kwa ujuml a. Mimi nikiwa kama mtaalamu wa maswala ya ki bank na uchumi napenda kusema mpango huu umechelewa sana kiasi mka serikali kuridhia mpango huu basi maji yamewafika shingoni.

Ndugu mtanzania ni lazima ujuwe mapango huu sio upo Tanzania tu, ila karibia dunia nzima wana fuwata mpango huu yani kitaalamu tunasema KNOW YOUR CUSTOMER [KYC]. Mpaango huu ulianza kwa mataifa ya magharibi na ulaya ilikuweza kuwalinda watumiaji wa bank, ugaidi, uzaji wa madawa ya kulevya, viongozi mafisadi wenye uchu wakuibaa rasilimali za nchizao, pia kuepuka malipo hewa ambayo kwa taifa hili ni janga lakitaifa, hivyo basi ukusanyaji huu wa taarifa za wateja ni muhimu sana na ndio maana BOT wakishirikiana na taasisi za fedha wanalisisitiza hilo.

Faida kwa mteja ni nyingi sana hatasiwezi kuzimaliza kuziandikaa ila nitajitaidi kuzielezea hizi zifuwatazo
-Kupunguza wizi ndani ya vyombo vya fedha hii mara nyingi ni kwawateja unakuta watu wakisaidiana na maofisa wa bank wasio waaminifu wanatumia udhaifu wa taarifa za mteja kufanya wizi ktk akaunti yamteja mimi nisingependa kutaja bank ila wewe utazijuw tu ni bank gani zinaongoza kwa u7salama mdogo wa fedha za wateja na sababu yakwanza ndio hii.

_Kurahisisha kufanya malipo iwe ni bank kwa mteja au serikali au mtu binfsi inakuwa rahisi sana, ngoja nikwaambie asilimia kubwa ya malipo hewa ni udhaifu ktk KYC, kama nilipokwisha gusia pale mwanzo wizi wowote unafanywa kwa kuangalia udhaifu ktk taasisi ya fedha.

-Kukiuwezesha wewe kama mteja kuishitaki bank pindi watalipa ama kufanya jambo lolote ambalo halipo ktk taarifa zako ulizo wapelekea. Kwa mfano wewe unaitwa Jomo Kapuku, inamaana lazima wamlipe mtu mwenye jina hilo hapo ikiwa itatoke ukagunduwa kuna pesa zimepotea ama kuna malipo uliandikiwa chq huyaoni ktk vitu vitaangaliwa ni majina sasa ikigundulika jina sio lenyewe mfano wamendika JOMOO Kapuko Basi hapa kuna kesi yakujibu ikiwa itathibitika wewe ulikuwa umetoa taarifa sahihi.
Zipo faida nyingi sana ila hizi zatosha kwa leo.

Faida kwa serikali ni nyingi sana ila hii nikubwa sana.

-Iposiri kubwa sana imefichika ktk malipo hewa kwa mmakampun na watu binafsi waatu wanaiba pesa SERIKALINI WANCHEZA DEAL NA MAAFISA WA BANK basi inafunguliwa akaunti au jamaa wanajuwa akaunti ni ya marehemu then wanafanya mambo tukumbuke marehem awezi kuja sikiliza kesi ya wizi hivyo serikali imekuwa ikipoteza a billion if not Trilion of money ktk wizzi wanamna hii, kwa kufanya hhili zoezi hakuna marehemu atakwenda ku update taarifa zake hivyo nilazima tujuwe wapo maafisa wa bank na serikalini sahizi matumbo yakuharisha yana wabana maana akaunti zinafungwa hivyo hata barch ya mshahara ikiwa na watumishi hewa haiwezzi kupita ikiwa watu watakuwa makini, itakuwa ni kwamara ya kwanza serikali itajuwa idadi ya wtu inawalipa mishahara jambo ambalo ni zuri kwa uchumi wetu.

Nimalizie kwa kusema haya ni baadhi tu ya yale nimekuandikia, pia wewe kama mtanzania okoa uchumi wako kwakwenda kutoa taarifa zako bank kwa usahihi usikubali kutumiwa na mafisadi kutoa taarifa za uwongo maana utafungwa na usionekane tena. Huu ni wakati pia wakuwa na akaunti yako binafsi, achan na mambo ya M-pesa tumia m-pesa kwa mambo madogo weka fedha bank ilikukuza uchumi wa taifa lako, kumbuka kunafaida nyingi kuweka pesa bank hivyo usikose nafasi hii

Kwaushahuri ni e-mail henrypoul@yahoo.com.
 
unasema tuachane na mpesa mbona imesajiliwa kisheria..na kama inamapungufu japo hujaainisha mapungufu yake kwa nini isifungiwe.....labda kama mtalam ungetupa faida na hasara za kutumia m-pesa tigo pesa nk.
 
Sababu zako hazina Mashika! hujaeleza kwa uwazi! yaleyale kila kitu kimejificha/kimefichwa!
 
Mhh asante kuwa kutujuza katika fani yako ila mimi naelewa kuwa huo ni mpango wa nchi za magharibi chini ya FMasons...katika mpango wa kutekeleza magoli yao ya millenia..lazima kujua financial info za watu ikiwezekana wote...hizo faida ulizotupa naona ni face-view tu ya kuuza sera zao ila kuna siri nyuma.
 
Back
Top Bottom