king kan
JF-Expert Member
- May 6, 2011
- 1,629
- 2,043
Je mtu mwenye miliki ya ardhi ya kijiji ilio chini ya hatimiliki ya kimila anaweza kupokonywa kwa kosa la kutoiendeleza .... Kma jibu ni ndio ni ndan ya muda gani mtu yampasa aendeleze na kw baada ya muda gani atapokonywa asipoendeleza.....NAOMBA MSAADA WAKUU
Kupokonywa ardhi kunatokea pale ambapo utakuwa umekwenda kinyume cha masharti yaliyowekwa kwenye hati husika.Masharti haya huwa yamewekwa wazi sio swala la kusema to hujaendeleza.
Kuendeleza sio lazima kujenga hata kulima. Dhana ya kuendeleza inategemeana na matumizi yaliyokubaliwa.
Hata hivyo kwa ardhi za vijijini hati za kimila nyingi nilizoona hazina hayo masharti hayo. Hivyo si rahisi kupokonywa.