Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,669
- 155,068
Kwa wakongwe kama Mshana Jr, mitaa ya Dizonga anainyaka vyema, kwani kakaa huko hadi pale alipohahamishwa na jini lililo mnasa vibao akitaka kulinanilihiiii kwenye nyumba ya wageni, akaona isiwe taabu, akahamia Masaki.
Sogodo ni eneo linalopatikana Mwananyamala Bwawani, nyuma ya mahakama ya Kinondoni, kanisa la KKKT Kinondoni, linasambaa hadi jirani na kwa Pawa, baba yake Jaki, alikuwa baunsa wa Billicanas Club Zama zile za kale.
Sogodo Empire, ilikuwa na watu wa hatari, watu wa Shari, wagomvi, watemi, waliojikataa, ambao wako tayari kwa lolote.
Watu wa jamhuri hiii walikuwa ni tishio kiasi kwamba walikuwa na mahakama yao, polisi wao na mamlaka yao wenyewe.
Ukiiba unapelekwa kwa Pawa, Pawa anakusikiliza mhalifu na washitaka wako, baada ya hapo anatoa hukumu.
Hukumu ikitekelezwa hamna kupelekana Polisi wala Nini. Kesi imeisha hiyo.
Sogodo Empire waliishi hivyo kwa miaka mingi.
Sogodo ni eneo linalopatikana Mwananyamala Bwawani, nyuma ya mahakama ya Kinondoni, kanisa la KKKT Kinondoni, linasambaa hadi jirani na kwa Pawa, baba yake Jaki, alikuwa baunsa wa Billicanas Club Zama zile za kale.
Sogodo Empire, ilikuwa na watu wa hatari, watu wa Shari, wagomvi, watemi, waliojikataa, ambao wako tayari kwa lolote.
Watu wa jamhuri hiii walikuwa ni tishio kiasi kwamba walikuwa na mahakama yao, polisi wao na mamlaka yao wenyewe.
Ukiiba unapelekwa kwa Pawa, Pawa anakusikiliza mhalifu na washitaka wako, baada ya hapo anatoa hukumu.
Hukumu ikitekelezwa hamna kupelekana Polisi wala Nini. Kesi imeisha hiyo.
Sogodo Empire waliishi hivyo kwa miaka mingi.