Ijue historia ya mgogoro kati ya Iran na Marekani

Safi
SEHEMU YA KUMI NA TATU

Habari wandugu , tuendelee na tulipoishia baada ya Rouhan kukataa kukutana na Obama, tarehe 26 mwezi wa tisa serikali ya Iran na marekani zilifanya kikao kikubwa cha maofisa wa ngazi za juu ambacho hakikuwahi kufanyika tangu mwaka 1979.

Kikao hicho kiliongozwa na mkuu wa sera za mambo ya nje wa umoja wa ulaya Bi Catherine Ashton.
Maongezi hayo yalionekana kuleta matumaini ya kukuza uhusiano wa nchi hizo mbili, siku iliyofuatia rais Rouhani na Obama walizungumza kwa njia ya simu, hilo tukio lilikuwa la kipekee ambalo halikuwahi kutokea tangu mwaka 1979.

“Marg ba Amrika” ni maneno yaliyosikika katika jiji la Tehran wakati Rais Rouhani akiwasili jijini hapo, maneno hayo yalitoka kwenye vinywa vya waandamanaji wasiopenda mahusiano ya nchi yao na Marekani, hii ni baada ya kupata taarifa kwamba rais wao ameongea na Obama. Kwa lugha ya Persians “Marg bar Amrika” ina maanisha “Death to America” yaani “Kifo kwa marekani” au “Mauti kwa Marekani”.

Msemo huu kwa wamiliki wa lugha ya kiingereza wanaupooza makali na kuutafsiri kama “Down with America”.

Kwa upande wa Iran kuna kundi kubwa la raia wanaotamani serikali yao ijenge mahusiano mema na marekani, na hii ilionekana katika kumbukumbu ya miaka 34 ya utekaji katika ubalozi wa marekani jijini Tehran (2013-1979=34) ambapo waandamanaji hao walikusanyika katika eneo lilikuwa ubalozi wa marekani mwaka 1979 kulaana kitendo cha kuchelewesha mahisiano kati ya nchi hizo mbili ambapo wao wanaona serikali yao ndio inakwamisha.

Barack Obama mtu asiye na kinyongo au kama vitabu vya kidini vinavyotamka “mtu asiye na hila” alikuwa akiwapa watu mikono na ikatokea amepeana mkono na waiziri wa mambo ya nje wa Iran Javad Zarif katika mkutano wa Umoja wa Mataifa, hii ndio mara ya kwanza kwa rais wa marekani kushikana na mwanadiplomasia mkubwa wa Iran tangu mwaka 1979 (mwaka wa mapinduzi ya Iran), hii ilikuwa ni mwaka 2015 tarehe 28 mwezi wa 9.

Baada ya handshake katibu wa serikali wa marekani akamtambulisha Obama kwa maafisa wengine wakubwa wa Iran walioshiriki JCPOA (Iran deal utaiona aya inayofuata). Kitendo hicho cha kupeana mikono kiliwachukiza baadhi ya wabunge wa Iran na kumtaka waziri aombe radhi hadharani.

Kabla sijazungumzia Iran Nuclear Deal naomba nielezee “Kura turufu” , yaani nazungumzia nchi zenye kura turufu, ni mataifa matano duniani ambayo yana nguvu Zaidi katika maamuzi ya umoja wa mataifa , ni nchi ambao ni wajumbe wa kudumu wa baraza la Amani la umoja wa mataifa, hivyo wao ndio wanakuwa na maamuzi ya mwisho katika mada za baraza hili na wengi wakipitisha jambo linaamuliwa na kama mjumbe hakushiriki haitabatilisha uamuzi.

Hivyo Joint Comprehensive Plan of Action (JCPOA, or the Iran Deal) ni makubaliano ya pamoja juu ya matumizi ya nyuklia nchini Iran , waliokaa kuweka makubaliaona hayo ni Iran na zile nchi tano zenye kura turufu ukiongeza na Ujerumani, unaweza kujionea kuwa nguvu za nyuklia zinahusisha moja kwa moja baraza la Amani duniani ndio maana kikao hicho kiliitiswah , hiyo ilikuwa ni mwaka 2015 mwezi was aba tarehe 14.

Mataifa yenye kura turufu ni Marekani, Uingereza, Urusi, Ufaransa na China, katika kikao hicho aliongezeka na ujerumani bila kusahau uwakilishi wa umoja wa ulaya. Katika kikao hiki Ujerumani alikaribishwa kwa sababu kuu moja tu , alikuwa ndiye msingi wa biashara ya nyuklia huko Iran, yeye ndiye aliyekuwa kimuuzia vifaa na huduma nyinginezo. Vinu vya nyuklia Iran vinatumia softwares za kampuni ya ujerumani Siemens (Simatic WinCC step7).

Viwanda mbali mbali vya ujerumani vina matawi yake Iran na zaidi ya makampuni 12000 ya ujerumani ya wawakilishi wa biashara Iran.

Katika mkutano huo utawala wa Obama ulikubali kuwaondolea Iran vikwazo vya kiuchumi vilivyodororesha uchumi wao kwa miaka na Iran iliahidi kuachana na mpango wake wa Nyuklia na kuruhusu wakaguzi wa umoja wa mtaifa kwenda kukagua muda wowote wanaotaka.

Hivyo Iran ilikubali “Katika mazingira yoyote haitojaribu kutafuta, kutengeneza au kumiliki silaha yoyote ya nyuklia”. Ndani ya marekani mkataba huu ulikubaliwa na asilimia 50 pekee ya raia katika tafiti iliyofanywa.

Tukirudi tena tutaangalia Utawala wa Donald Trump, kuanzia 2017, kwa 2016 mgogoro huu ulikuwa wa kisheria Zaidi kwa mataifa hayo kutishia kudaiana fidia kwa matukio yaliyofanyiana katika historia lakini hamna lililotekelezwa.


Bado inaendelea…………………………………………………………..

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SEHEMU YA KUMI NA NNE
Mbaguzi wa rangi, Mnyanyasaji wa kijinsia, Kibaraka wa Urusi , Mwizi wa Demokrasia, Aliyeoa kahaba, Mbaguzi wa kidini na mbabe, Hayo ni baadhi ya majina yaliyotumika na wapinzani wake kumtaja rais wa 45 wa marekani Donald Trump.

Akiwa na wiki moja tu tangu aapishwe kuwa Rais wa marekani alikuja na Executive order 13769 nyaraka yenye kichwa kinachosema “Protecting the Nation from Foreign Terrorist Entry into the United States” naweza kutafsiri kwa kusema “kulilinda taifa kwa kuzuia magaidi kutoka nchi za nje kuingia marekani” , hii wanasiasa walikuwa wakiitafsiri kama “katazo hilo ni kwa ajili ya waislamu” wengine wakisema katazo hilo ni kupunguza wasafiri wanaoingia marekani .

Waliokumbwa na “travel ban” hiyo ni Iran pamoja na nchi zingine zilizohusishwa na ugaidi, hapa kama ni mfuatiliaje wa taarifa hizi nadhani utakumbuka kipindi kile marekani anaorodhosha nchi zitakazoathiriwa na ban hii , nchi hizo ni Iran, Iraq, Libya , Somalia , Sudan, Syria na Yemen, wasafiri Zaidi ya 700 walizuiwa kuingia marekani na VISA Zaidi ya 60000 zilikataliwa.

Hiyo ilikuwa 27 January 2017. Serikali ya marekani hairuhusu mtu yeyote ambaye ni raia au anayeshukiwa kuwa ni raia wa Iran kuingia marekani labda awe anapita kama njia, yaani zile ndege zinaenda nchi fulani basi lazima zipitie nchi fulani kujaza mafuta au kuongeza abiria. Abiria wote na wafanyakazi wa ndege zinazoingia marekani kutoka nchi yoyote ile lazima wahakikishe hawana VISA za Iran katika Passport zao yaani muhuri wa kuingia Iran usiwepo kwenye passport zao. Vilevile hakuna ndege ya moja kwa moja kutoka Iran kwenda marekani hivyo safari zote lazima zipitie katika nchi nyingine, Zaidi ya hayo hakuna ndege yoyote ya Iran inayoruhusiwa kupita katika anga la marekanin.

Katika harakati za kuidhoofisha Iran utawala wa rais Trump umeonekana kuingia katika njia ya kuimarisha umoja usio rasmi kati ya Saudi Arabia, Israel, U.A.E na mataifa mengine ya katika ghuba ya kisunni.

Kipindi cha kampeni za uchaguzi Trump aliwahi kunukuliwa akilaani JCPOA (Iran deal) kwa kusema ni dili la hovyo kabisa kuwahi kujadiliwa na linaweza kupelekea madhara makubwa Zaidi ya nguvu za nyuklia duniani, lakini katika hali ya kustaajabisha mwezi wan ne 2017 iliweka hadharani kwamba Iran bado inatimiza makubaliano ya JCPOA , Nadhani bado mnakumbuka ahadi ya Iran katika dili hilo kwamba haitomiliki , kujaribu kumiliki ama kutengeneza silaha za nyuklia.

Mgogoro huu unatumika sana kisiasa nchini Iran na marekani kama moja wapo ya sera za kumuingiza mtu ikulu, kama ulivyo umaskini nchi za afrika. Wenzetu wameendelea kidogo kwani wengi wao wanatumia sana mitandao ya kijamii kama Twitter , kutoka January hadi July pekee mwaka 2017 Twitter walitambua na kuzifungia account bandia Zaidi ya 7000.

Mchezo huo wa accounts bandia unatumika sana kwa wenzetu na ni katika level za kimataifa, accounts nyingi zilionekana kuwepo urusi na Iran na zililenga kutoa taarifa za uongo juu ya mgogoro huu au habari nyingine za siasa nchini marekani kwa ajili ya kuathiri uchaguzi ujao wa nchi hiyo,

yaani ni kama watanzania tuwachezee wakenya mchezo huu tukitaka aingie madarakani rais tunaemtaka sisi. Mfano kuwe na account Zaidi ya 100 kama za kigogo_14 halafu kumbe sio za Tanzania , wamekaa nchini kwao mfano (Rwanda) wanacheka tu namna waziri akijibizana nae kama ni mtanzania kumbe yupo Kigali na analipwa na serikali ya huko (NIMETOA MFANO, MSINI-QUOTE vibaya).

Mwezi huo huo July wabunge wengi wa Congress kutoka republican na democratic walipigia kura za ndio muswada wa CAATSA (Countering America’s Adversaries Through Sanctions Act) yaani kukabiliana na maadui wa marekani kupitia vikwazo. Maadui hao wakubwa ni Iran, Urusi na Korea ya Kaskazini. Mwezi wa nane tarehe mbili rais trump alisign na kuifanya kuwa sheria.

Kuiwekea Iran vikwazo nadhani mnakumbuka ni kinyume na JCPOA , Wakati utawala wa Trump ukitangaza kwamba wameridhika baada ya kuthibitisha Iran inafuata makubaliano ya mkataba huo. Sasa marekani anaweka vikwazo kwa maadui wake na kuijumuisha Iran. Yaani inakiuka mktaba wa JCPOA.
Maamuzi hayo ya Bunge yalikuwa mabaya kwa Iran kwani inairudisha katika mdororo wa kiuchumi , naibu waziri wa mambo ya nje wa Iran Abbas Araqchi alisema kwamba “kwa mtazamo wetu ni kuwa mkataba wa nyuklia umekiukwa” na katika mkutano wa UN Septemba 2017 maraisi wan chi hizo mbili walitoa mitazamo inayopingana juu ya mkataba wa JCPOA.

Kufikia mwezi wa tano waka 2018 , Rais Donald Trump aliamua kujitoa katika mkataba wa JCPOA na kutangaza ataweka vikwazo vya kiuchumi kwa Iran kuanzia tarehe 4 mwezi November 2018. Kwa upande wa Iran Rais Hassan Rouhani naye akasema anaweza kuanza kutengeneza Nyuklia bila kizuizi chochote. Tarehe 5 mwezi wa saba Iran ikatishia kufunga Strait of Hormuz kama marekani itawawekea vikwazo katika biashara ya OIL baada ya kujitoa katika JCPOA.

Strait (mkondo bahari) ni sehemu nyembamba ya maji inayounganisha bahari mbili au maziwa, naweza kuita mkondo wa maji kwa Kiswahili kama sijakosea, hivyo strait of Hormuz inaunganisha Ghuba ya Oman na Ghuba ya Persia. Ni miongoni mwa sehemu muhimu Zaidi kimkakati duniani , kijeshi sehemu za namna hiyo zinaitwa “Choke Points”, hizi sehemu zinafaa Zaidi kwa ambush, lakini pia kwa hii kufungwa ingezuia meli kutoka ghuba ya Oman. Mfano ni mkondo bahari wa Gibraltar unaounganisha bahari ya Mediterranean na Bahari ya Atlantiki.
Nimeweka picha hapo chini unaweza kujuionea eneo hilo.

Kwa leo hapa inatosha , maadam tumefika kwa trump basi twende nae mdogo mdogo……………………………………………………………………………..

SEHEMU YA KUMI NA TANO POST #261



Screenshot_20200123-205046_WhatsApp.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
SEHEMU YA KUMI NA NNE
Mbaguzi wa rangi, Mnyanyasaji wa kijinsia, Kibaraka wa Urusi , Mwizi wa Demokrasia, Aliyeoa kahaba, Mbaguzi wa kidini na mbabe, Hayo ni baadhi ya majina yaliyotumika na wapinzani wake kumtaja rais wa 45 wa marekani Donald Trump.

Akiwa na wiki moja tu tangu aapishwe kuwa Rais wa marekani alikuja na Executive order 13769 nyaraka yenye kichwa kinachosema “Protecting the Nation from Foreign Terrorist Entry into the United States” naweza kutafsiri kwa kusema “kulilinda taifa kwa kuzuia magaidi kutoka nchi za nje kuingia marekani” , hii wanasiasa walikuwa wakiitafsiri kama “katazo hilo ni kwa ajili ya waislamu” wengine wakisema katazo hilo ni kupunguza wasafiri wanaoingia marekani .

Waliokumbwa na “travel ban” hiyo ni Iran pamoja na nchi zingine zilizohusishwa na ugaidi, hapa kama ni mfuatiliaje wa taarifa hizi nadhani utakumbuka kipindi kile marekani anaorodhosha nchi zitakazoathiriwa na ban hii , nchi hizo ni Iran, Iraq, Libya , Somalia , Sudan, Syria na Yemen, wasafiri Zaidi ya 700 walizuiwa kuingia marekani na VISA Zaidi ya 60000 zilikataliwa.

Hiyo ilikuwa 27 January 2017. Serikali ya marekani hairuhusu mtu yeyote ambaye ni raia au anayeshukiwa kuwa ni raia wa Iran kuingia marekani labda awe anapita kama njia, yaani zile ndege zinaenda nchi fulani basi lazima zipitie nchi fulani kujaza mafuta au kuongeza abiria. Abiria wote na wafanyakazi wa ndege zinazoingia marekani kutoka nchi yoyote ile lazima wahakikishe hawana VISA za Iran katika Passport zao yaani muhuri wa kuingia Iran usiwepo kwenye passport zao. Vilevile hakuna ndege ya moja kwa moja kutoka Iran kwenda marekani hivyo safari zote lazima zipitie katika nchi nyingine, Zaidi ya hayo hakuna ndege yoyote ya Iran inayoruhusiwa kupita katika anga la marekanin.

Katika harakati za kuidhoofisha Iran utawala wa rais Trump umeonekana kuingia katika njia ya kuimarisha umoja usio rasmi kati ya Saudi Arabia, Israel, U.A.E na mataifa mengine ya katika ghuba ya kisunni.

Kipindi cha kampeni za uchaguzi Trump aliwahi kunukuliwa akilaani JCPOA (Iran deal) kwa kusema ni dili la hovyo kabisa kuwahi kujadiliwa na linaweza kupelekea madhara makubwa Zaidi ya nguvu za nyuklia duniani, lakini katika hali ya kustaajabisha mwezi wan ne 2017 iliweka hadharani kwamba Iran bado inatimiza makubaliano ya JCPOA , Nadhani bado mnakumbuka ahadi ya Iran katika dili hilo kwamba haitomiliki , kujaribu kumiliki ama kutengeneza silaha za nyuklia.

Mgogoro huu unatumika sana kisiasa nchini Iran na marekani kama moja wapo ya sera za kumuingiza mtu ikulu, kama ulivyo umaskini nchi za afrika. Wenzetu wameendelea kidogo kwani wengi wao wanatumia sana mitandao ya kijamii kama Twitter , kutoka January hadi July pekee mwaka 2017 Twitter walitambua na kuzifungia account bandia Zaidi ya 7000.

Mchezo huo wa accounts bandia unatumika sana kwa wenzetu na ni katika level za kimataifa, accounts nyingi zilionekana kuwepo urusi na Iran na zililenga kutoa taarifa za uongo juu ya mgogoro huu au habari nyingine za siasa nchini marekani kwa ajili ya kuathiri uchaguzi ujao wa nchi hiyo,

yaani ni kama watanzania tuwachezee wakenya mchezo huu tukitaka aingie madarakani rais tunaemtaka sisi. Mfano kuwe na account Zaidi ya 100 kama za kigogo_14 halafu kumbe sio za Tanzania , wamekaa nchini kwao mfano (Rwanda) wanacheka tu namna waziri akijibizana nae kama ni mtanzania kumbe yupo Kigali na analipwa na serikali ya huko (NIMETOA MFANO, MSINI-QUOTE vibaya).

Mwezi huo huo July wabunge wengi wa Congress kutoka republican na democratic walipigia kura za ndio muswada wa CAATSA (Countering America’s Adversaries Through Sanctions Act) yaani kukabiliana na maadui wa marekani kupitia vikwazo. Maadui hao wakubwa ni Iran, Urusi na Korea ya Kaskazini. Mwezi wa nane tarehe mbili rais trump alisign na kuifanya kuwa sheria.

Kuiwekea Iran vikwazo nadhani mnakumbuka ni kinyume na JCPOA , Wakati utawala wa Trump ukitangaza kwamba wameridhika baada ya kuthibitisha Iran inafuata makubaliano ya mkataba huo. Sasa marekani anaweka vikwazo kwa maadui wake na kuijumuisha Iran. Yaani inakiuka mktaba wa JCPOA.
Maamuzi hayo ya Bunge yalikuwa mabaya kwa Iran kwani inairudisha katika mdororo wa kiuchumi , naibu waziri wa mambo ya nje wa Iran Abbas Araqchi alisema kwamba “kwa mtazamo wetu ni kuwa mkataba wa nyuklia umekiukwa” na katika mkutano wa UN Septemba 2017 maraisi wan chi hizo mbili walitoa mitazamo inayopingana juu ya mkataba wa JCPOA.

Kufikia mwezi wa tano waka 2018 , Rais Donald Trump aliamua kujitoa katika mkataba wa JCPOA na kutangaza ataweka vikwazo vya kiuchumi kwa Iran kuanzia tarehe 4 mwezi November 2018. Kwa upande wa Iran Rais Hassan Rouhani naye akasema anaweza kuanza kutengeneza Nyuklia bila kizuizi chochote. Tarehe 5 mwezi wa saba Iran ikatishia kufunga Strait of Hormuz kama marekani itawawekea vikwazo katika biashara ya OIL baada ya kujitoa katika JCPOA.

Strait (mkondo bahari) ni sehemu nyembamba ya maji inayounganisha bahari mbili au maziwa, naweza kuita mkondo wa maji kwa Kiswahili kama sijakosea, hivyo strait of Hormuz inaunganisha Ghuba ya Oman na Ghuba ya Persia. Ni miongoni mwa sehemu muhimu Zaidi kimkakati duniani , kijeshi sehemu za namna hiyo zinaitwa “Choke Points”, hizi sehemu zinafaa Zaidi kwa ambush, lakini pia kwa hii kufungwa ingezuia meli kutoka ghuba ya Oman. Mfano ni mkondo bahari wa Gibraltar unaounganisha bahari ya Mediterranean na Bahari ya Atlantiki.
Nimeweka picha hapo chini unaweza kujuionea eneo hilo.

Kwa leo hapa inatosha , maadam tumefika kwa trump basi twende nae mdogo mdogo……………………………………………………………………………..View attachment 1332332

Sent using Jamii Forums mobile app
Aah babu kubwa 👏👊💯
 
SEHEMU YA KUMI NA NNE
Mbaguzi wa rangi, Mnyanyasaji wa kijinsia, Kibaraka wa Urusi , Mwizi wa Demokrasia, Aliyeoa kahaba, Mbaguzi wa kidini na mbabe, Hayo ni baadhi ya majina yaliyotumika na wapinzani wake kumtaja rais wa 45 wa marekani Donald Trump.

Akiwa na wiki moja tu tangu aapishwe kuwa Rais wa marekani alikuja na Executive order 13769 nyaraka yenye kichwa kinachosema “Protecting the Nation from Foreign Terrorist Entry into the United States” naweza kutafsiri kwa kusema “kulilinda taifa kwa kuzuia magaidi kutoka nchi za nje kuingia marekani” , hii wanasiasa walikuwa wakiitafsiri kama “katazo hilo ni kwa ajili ya waislamu” wengine wakisema katazo hilo ni kupunguza wasafiri wanaoingia marekani .

Waliokumbwa na “travel ban” hiyo ni Iran pamoja na nchi zingine zilizohusishwa na ugaidi, hapa kama ni mfuatiliaje wa taarifa hizi nadhani utakumbuka kipindi kile marekani anaorodhosha nchi zitakazoathiriwa na ban hii , nchi hizo ni Iran, Iraq, Libya , Somalia , Sudan, Syria na Yemen, wasafiri Zaidi ya 700 walizuiwa kuingia marekani na VISA Zaidi ya 60000 zilikataliwa.

Hiyo ilikuwa 27 January 2017. Serikali ya marekani hairuhusu mtu yeyote ambaye ni raia au anayeshukiwa kuwa ni raia wa Iran kuingia marekani labda awe anapita kama njia, yaani zile ndege zinaenda nchi fulani basi lazima zipitie nchi fulani kujaza mafuta au kuongeza abiria. Abiria wote na wafanyakazi wa ndege zinazoingia marekani kutoka nchi yoyote ile lazima wahakikishe hawana VISA za Iran katika Passport zao yaani muhuri wa kuingia Iran usiwepo kwenye passport zao. Vilevile hakuna ndege ya moja kwa moja kutoka Iran kwenda marekani hivyo safari zote lazima zipitie katika nchi nyingine, Zaidi ya hayo hakuna ndege yoyote ya Iran inayoruhusiwa kupita katika anga la marekanin.

Katika harakati za kuidhoofisha Iran utawala wa rais Trump umeonekana kuingia katika njia ya kuimarisha umoja usio rasmi kati ya Saudi Arabia, Israel, U.A.E na mataifa mengine ya katika ghuba ya kisunni.

Kipindi cha kampeni za uchaguzi Trump aliwahi kunukuliwa akilaani JCPOA (Iran deal) kwa kusema ni dili la hovyo kabisa kuwahi kujadiliwa na linaweza kupelekea madhara makubwa Zaidi ya nguvu za nyuklia duniani, lakini katika hali ya kustaajabisha mwezi wan ne 2017 iliweka hadharani kwamba Iran bado inatimiza makubaliano ya JCPOA , Nadhani bado mnakumbuka ahadi ya Iran katika dili hilo kwamba haitomiliki , kujaribu kumiliki ama kutengeneza silaha za nyuklia.

Mgogoro huu unatumika sana kisiasa nchini Iran na marekani kama moja wapo ya sera za kumuingiza mtu ikulu, kama ulivyo umaskini nchi za afrika. Wenzetu wameendelea kidogo kwani wengi wao wanatumia sana mitandao ya kijamii kama Twitter , kutoka January hadi July pekee mwaka 2017 Twitter walitambua na kuzifungia account bandia Zaidi ya 7000.

Mchezo huo wa accounts bandia unatumika sana kwa wenzetu na ni katika level za kimataifa, accounts nyingi zilionekana kuwepo urusi na Iran na zililenga kutoa taarifa za uongo juu ya mgogoro huu au habari nyingine za siasa nchini marekani kwa ajili ya kuathiri uchaguzi ujao wa nchi hiyo,

yaani ni kama watanzania tuwachezee wakenya mchezo huu tukitaka aingie madarakani rais tunaemtaka sisi. Mfano kuwe na account Zaidi ya 100 kama za kigogo_14 halafu kumbe sio za Tanzania , wamekaa nchini kwao mfano (Rwanda) wanacheka tu namna waziri akijibizana nae kama ni mtanzania kumbe yupo Kigali na analipwa na serikali ya huko (NIMETOA MFANO, MSINI-QUOTE vibaya).

Mwezi huo huo July wabunge wengi wa Congress kutoka republican na democratic walipigia kura za ndio muswada wa CAATSA (Countering America’s Adversaries Through Sanctions Act) yaani kukabiliana na maadui wa marekani kupitia vikwazo. Maadui hao wakubwa ni Iran, Urusi na Korea ya Kaskazini. Mwezi wa nane tarehe mbili rais trump alisign na kuifanya kuwa sheria.

Kuiwekea Iran vikwazo nadhani mnakumbuka ni kinyume na JCPOA , Wakati utawala wa Trump ukitangaza kwamba wameridhika baada ya kuthibitisha Iran inafuata makubaliano ya mkataba huo. Sasa marekani anaweka vikwazo kwa maadui wake na kuijumuisha Iran. Yaani inakiuka mktaba wa JCPOA.
Maamuzi hayo ya Bunge yalikuwa mabaya kwa Iran kwani inairudisha katika mdororo wa kiuchumi , naibu waziri wa mambo ya nje wa Iran Abbas Araqchi alisema kwamba “kwa mtazamo wetu ni kuwa mkataba wa nyuklia umekiukwa” na katika mkutano wa UN Septemba 2017 maraisi wan chi hizo mbili walitoa mitazamo inayopingana juu ya mkataba wa JCPOA.

Kufikia mwezi wa tano waka 2018 , Rais Donald Trump aliamua kujitoa katika mkataba wa JCPOA na kutangaza ataweka vikwazo vya kiuchumi kwa Iran kuanzia tarehe 4 mwezi November 2018. Kwa upande wa Iran Rais Hassan Rouhani naye akasema anaweza kuanza kutengeneza Nyuklia bila kizuizi chochote. Tarehe 5 mwezi wa saba Iran ikatishia kufunga Strait of Hormuz kama marekani itawawekea vikwazo katika biashara ya OIL baada ya kujitoa katika JCPOA.

Strait (mkondo bahari) ni sehemu nyembamba ya maji inayounganisha bahari mbili au maziwa, naweza kuita mkondo wa maji kwa Kiswahili kama sijakosea, hivyo strait of Hormuz inaunganisha Ghuba ya Oman na Ghuba ya Persia. Ni miongoni mwa sehemu muhimu Zaidi kimkakati duniani , kijeshi sehemu za namna hiyo zinaitwa “Choke Points”, hizi sehemu zinafaa Zaidi kwa ambush, lakini pia kwa hii kufungwa ingezuia meli kutoka ghuba ya Oman. Mfano ni mkondo bahari wa Gibraltar unaounganisha bahari ya Mediterranean na Bahari ya Atlantiki.
Nimeweka picha hapo chini unaweza kujuionea eneo hilo.

Kwa leo hapa inatosha , maadam tumefika kwa trump basi twende nae mdogo mdogo……………………………………………………………………………..View attachment 1332332

Sent using Jamii Forums mobile app
Adhuhuri inaisha mpk mda huu ni kimyaaa...
 
SEHEMU YA KUMI NA TANO
Wakati watu wa international politics tukiendelea kujadili Marekani kutaka kutuwekea vikwazo katika utoaji wa viza acha tuendelee kusoma historia hii pia, wenzetu hawa tunaamini wana mfumo bora wa maisha kule kwao hivyo tukipewe visa lazima tupitilize muda wa kukaa huko.

Mwishoni mwa mwezi wa saba 2018 wakati rais wa marekani akiendelea kutupiana vitisho na rais wa Iran, meli kubwa inayopeperusha bendera ya Saudi Arabia ikisafirisha Oil kwenda Egypt ilishambuliwa katika mkongo bahari wa Bab-el-Mandeb na waasi wa Yemen wanaojiita Houthi, inaaminika kuwa kikundi hichi cha waasi kinafadhiliwa na Iran kijeshi na kifedha.

Tukio hilo la kushambuliwa kwa meli hiyo lilipelekea Saudi Arabia kuacha kutumia mkondo huo, tukio hilo lilikuja baada ya taarifa kuwa marekani alikuwa katika mpango wa kuchochea vikundi vya upinzani nchini Iran.

Mwezi wa nane tarehe 13 2018 Kiongozi mkuu wa Iran Ayatollah Khamenei alizuia mazungumzo ya moja kwa moja na serikali ya marekani kwa kuzingatia kushindikana kwa majadiliano yaliyopita , maneno yake yalikuwa kama ifuatavyo “Hakutakuwa na vita , wala mzungumzo na marekani, na hata lisilowezekana ikitokea tukazungumza na marekani haitokuwa na utawala wa sasa wa marekani”.

Aliongeza kwamba , marekani haiwi rafiki wa lengo la msingi katika majadiliano ambalo ni kutoa na kupokea . yeye huvutia kwake tu , baada ya majadiliano ya mwezi wa kumi na moja 2018 vikwazo vyote vilivyoondolewa na kwa Iran 2015 vilirudishwa tena na utawala wa Trump.

Mwezi wa tatu 2019, Kaimu balozi wa marekani katika umoja wa mataifa Mr Jonathan Cohen, alituma barua kwa katibu mkuu wa UN Antonio Guterres akishinikiza UN iwawekee vikwazo vipya Iran kutokana na shughuli zake mpya za kutengeneza makombora.

Serikali ya Marekani imekuwa ikipingana na Jeshi la mapinduzi la Iran (IRGC) kutokana na jinsi kikundi hicho kinavyozidi kujihusisha nchini Iraq na Afghanistan katika kusaidia vikundi vyenye msimamo mkalali katika mashariki ya kati, manamo tarehe nane mwezi wan ne mwaka 2019 (8 April 2019) marekani iliweka hadharani nia yake ya kulitaja jeshi la Kimapinduzi la Iran IRGC kama kikundi cha kigadi (Foreign Terrorist Organization FTO) rasmi kuanzia April 15.

Bunge la Iran lilijibu mapigo kwa kuridhia kutaja “ makundi yote ya jeshi la marekani na washirika wake waliopo magharibi ya Asia” ni vikundi vya kigaidi na msaada wowote kwao ni kitendo cha kigaidi, Maafisa wanaofanya kazi na Khamenei walienda mbali Zaidi na kutaja serikali ya marekani kuwa ninserikali ya kigaidi na CENTCOM ni kikundi chake kikuu cha ugaidi, CENTCOM (United States Central Command also USCENTCOM) Ni sehemu ya jeshi la marekani katika kitengo cha ulinzi kinachofanya kazi mashariki ya kati (Egypt na Asia ya kati ikihusisha Afghanistan na Iraq).

IRGC ikawekwa katika list ya FTO kwa ushawishi wake na kusaidia uasi nchini Iraq uliosababisha vifo kwa wanajeshi wa marekani. Inadaiwa Jeshi hilo lililokuwa chini ya Meja Jenerali Soleimani ilifanya kazi kupitia ketego maalum QUDS FORCE katika nchi za Asia ya kati kwa kushirikiana na vikundi vya kigaidi kama Hezbollah.
US state department (Maalum kwa sera za mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa) iliionya IRGC kwa kuzidi kujihusisha na mgogoro wa Syria.

“Tunaamini huu ni mwendelezo wa tahadhari, kutokana na uchunguzi wa karibu tukitathmini mazingira ya shughuli za ugaidi duniani. Kwa kuongezea, bila shaka , ni kujiigiza Zaidi kwa Iran na Hezbollah katika kupambana na kuua kwa niaba ya utawala wa Assad nchini Syria, kujihusisha huko kunazidi kuukomaza mgogoro huo na kutishia kuenea kwa mashambulizi.

Hezbollah na uongozi wa Iran wanashabihiana kwa mitazama na mikakati na wanatazamia kutumia hali ya sitofahamu katika eneo hilo kwa manufaa yao. Njama hizo zimeongeza mvutano na migogoro na zinadizi kuzorotesha harakati za kutafuta Amani katika eneo hilo.”
Hili lilikuwa tamko la US department of State.

Tarehe 10 April Katibu mkuu wa Hezbollah Hassan Nasrallah alijibu mapigo katika hotuba iliyorushwa na runinga kutoka Beirut kama ifuatavyo

“Upumbavu na uzembe wa marekani umevuka mipaka kwa kulitaja Jeshi la mapinduzi la Iran IRGC kama kikundi cha kigaidi, Jeshi hilo limejitoa muhanga kupambana dhidi ya marekani na Israel,Sisi tunalaani maamuzi ya marekani na tunatangaza kuunga mkono marafiki zetu wa IRGC.”

Hali ya hofu ilikuwepo kwa viongozi wa marekani kwa kuhofia hatua za IRGC, na haiwezekani kutofautisha shughuli za IRGC na uongozi mkuu wa Iran , IRGC walitishia kushambulia kambi za marekani. Baadhi ya wanadiplomasia walionya kuwa ukuta kati ya mataifa haya mawili unazidi kuwa mpana na mrefu Zaidi.

Hii ilikuwa ni mara ya kwanza kwa kikundi halali cha kijeshi cha nchi inayojitawala kutajwa katika list ya vikundi vya kigaidi vinavyopigwa vita. Pia marekani ilitishia kuziwekea vikwazo nchi zinazoendelea kununua mafuta kutoka Iran.

Tukirudi nyuma kidogo niligusia Choke point ya strait of Hormutz , Rais Rouhani wa Iran alitangaza mwezi wa kumi na mbili 2018 kwamba “Kama siku watazuia mafuta ya Iran kusafirishwa basi hakuna mafuta yoyote yatakayosafirishwa kutoka katiika ghuba ya Persia”
April 2019, marekani ilizidi kuliandama Jeshi la mapinduzi la Iran IRGC kwa kulitaja kuwa ni kikundi cha kigaidi kinachohitaji kutizamwa Zaidi na State department. Maamuzi hayo yalikuwa yakipingana na CIA na DoD (Departmant of Defense) .

Mvutano kati ya marekani na Iran ulizidi kukomaa may 2019, kwa marekani kuongeza majeshi yao katika Ghuba ya Persia baada ya taarifa za kiintelijensia kuonyesha kuwa Iran na washirika wake kutishia vikosi vya marekani na usafirishaji wa mafuta katika Strait of Hormutz.

Maafisa wa marekani waliweza kuona hatari katika biashara ya mafuta na shambulio kwa majeshi ya marekani yaliyoko Iraq kutoka kwa Iran na washirika wake. Zaidi ya hayo ripoti za kiintelijensia zilijumuisha picha za makombora yaliyohifadhiwa katika majahazi na boti ndogo maeneo ya ghuba ya Persia, Makombora hayo yamewekwa maalum na paramilitary forces za Iran (nilielezea mwanzo maana yake), hivyo Marekani ikahofia kuwa vikosi vyake vya majini vitashambuliwa.

Itaendelea………………………………………………………………………………………………

SEHEMU YA KUMI NA SITA POST #264

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom