Mpasuajipu
JF-Expert Member
- Oct 22, 2010
- 836
- 49
Kanali Muommar Gadhafi miaka 68- alipata madaraka katika mapinduzi yasiyo ya kumwaga damu mwaka 1969- alimpindua aliyekuwa mfalme wa Libya wakati huo Mfalme Idris.
Watoto wa Gadhafi
1. Muhammad
Mtoto wa kwanza wa Gadhafi na mkewe wake wa kwanza, Fatiha waliyetengana naye miezi sita tu baada ya ndoa yao.
Muhammad ni kiongozi wa kamati ya olimpiki na ni mwenyekiti wa shirika la Posta na mawasiliano-telecom co.
2. Saif al-Islam
Heir apparent Saif al-Islam has a PHd. From the London School of Economics
Mtoto wa pili wa Dhadafi - umri miaka 38, and Phd katika masuala ya Uchumi.
Kwa kutumia Charity organization ya baba yake, alitoa misaada mingi sana kipindi kile haiti ilipoharibiwa na tetemeko la ardhi.
Walibya wengi wanadhani ni mtu mwadilifu anayefaa hata kuiongoza Libya baada ya baba yake. Hata hivyo, ukweli ni kwamba ni fisadi mdogo anayemiliki hisa nyingi ktk makampuni ya mafuta yaliyowekeza Libya. Pia anapenda wanawake, na katika tukio moja, inasadikika kuwa aliwahi kumlipa Mariah Carey dola za kimarekani millioni moja ili kuonyesha tamasha la muziki.
Hivi karibuni, wakati waandamanaji wakijitokeza kwa wingi kumpinga baba yake, alitokea kwenye televisheni ya taifa na kuwaita waandamanaji walevi, watumia dawa za kulevya na magaidi.
3. Saadi Gadhafi
Saadi Gadhafi- A senior Engineer and Former pro soccer player with a troubled past
Saadi ni mtoto wa tatu wa kiume wa Gadhafi mwenye historia mbaya ya maisha kwa ujumla, ikiwa ni pamoja na kupambana na polisi katika nchi kadhaa za ulaya hasa Italia kuhusiana na matumizi ya pombe na madawa ya kulevya. Aliwahi kuwa mcheza soka wa kulipwa huko Italia lakini akafukuzwa katika kikosi kwa kutumia dawa za kulevya.
4. Muatassim
Mtoto wa nne wa kiume wa Gadhafimwenye ushindani mkubwa na Saif katika kutaka kurithi biashara ya familia ya Gadhafi.
Alikosana na baba yake na kulazimika kwenda kuishi maisha ya kikimbizi nchini Misri mwaka 1990 . Aliruhusiwa kurudi nyumbani mwaka 2006 na kuchaguliwa kuwa mashauri wa mambo ya kiusalama. Mwaka 2009, alitembelea washington na kubahatika kukutana na mkuu wa wa Idara ya mambo ya nje ya Marekani Bi. Hillary Rodham Clinton kitendo ambacho kilimkasirisha sana Saif. Muatassim inadaiwa pia aliwahi kumlipa mamilioni ya dola za kimarekani Beyonce na Usher katika party moja ya mwaka mpya huko St. Barts.
5. Hannibal
Ni mtoto wa tano wa kiume wa Gadhafi. Inashukiwa pia kuwa aliwahi kumpiga mkewe Aline mara kwa mara. Aliwahi kufukuzwa katika hoteli moja huko London baada ya kumpiga mkewe na kumjeruhi usoni. Hali hii ilimlazimu mtoto wa kike wa Gadhafi, Aisha (ambaye alikuwa mja mzito karibia na kuzaa) kwenda London kusuluhisha ugomvi huo na kudanganya kuwa Aline aliumia katika ajali.
Hannibal alikuwa pia anatabia isiyo ya kawaida na alijihusisha na matukio mengi ya ajabu ajabu huko ulaya. Inasemekana kuwa, mwaka 2001 katika hoteli ya Rome aliwashambulia polisi watatu kwa kutumia gasi ya kuzimia moto Fire extinguisher na pia aliwahi kufanya shambulizi kwa wafanyakazi wake wapambe huko Geneva mwaka 2008. Alikamatwa na polisi na kufunguliwa mashitaka, hata hivyo aliachiwa baada ya siku mbili tu. Kwa tukio hilo, Libya ilizuia uingizaji wa bidhaa zote za Switzerland, ikazuia utoaji viza kwa raia wa Switzerland na kulazimisha makampuni yote ya nchi hiyo kufunga offisi zake huko Libya.
6.Khamis
Ni mtoto wa sita wa kiume wa Gadhafi ambaye hajulikani sana.
Ni kamanda wa kivita anayeheshimika sana katika vikosi maalum na mtetezi mkubwa wa sera za baba yake.
Amepata mafunzo ya kijeshi Russia na ana PhD katika millitary sciences aliyopipata mwaka 2007.
Anaongoza kikosi cha 32 Brigedi ambayo inajulikana kama ni mojawapo ya vikosi madhubuti sana chenye mafunzo ya hali ya juu na na vifaa vya kisasa kabisa katika jeshi la Libya. Kikosi hiki kinaaminika kuwa ndicho kimeshiriki sana katika kuwashambulia waandamanaji wanaoipinga serikali ya Bwana Gadhafi.
7.Aisha Gadhafi
Aisha Gadhafi is a trained lawyer who served on Saddam Husseins defence team.
Mtoto pkee wa Kike wa Gadhafi ambaye anaaminika kama ndiye shauri wa familia yenye matatizo ya Gadhafi.
Aisha, alichochea kwa kiasi kikubwa mzozo kati ya Libya na Uswisi kufuatia kukamatwa kwa kaka yake Hannibal na hivyo kuongeza hasira ya baba yake katika mzozo huo. Aisha alilikuza tatizo hilo kiasi ambacho ilishindikana kupatikana kwa suluhisho kati ya nchi hizo mbili
8.Saif al-Arab
Mtoto wa nane wa Gadhafi anayeishi Ujerumani katika mji wa Munich.
Inasemekana anafanya biashara sizizohalali na anamatumizi makubwa katika kujimwaga yaani party.
Serikali ya Uerumani imeanza kumnyooshea kidole dogo huyu na ni jambo la muda tu kila kitu serikali itachukua hatua kwa kufuatia mwenendo hali wa mzozo unaoendelea Libya kwa baba yake.
Hiyo ndiyo orodha ya watoto WATUKUTU WA MFALME GADHAFI KAMA ANAVYOJIITA YEYE.
KWELI MTOTO WA NYOKA NI NYOKA TU
Watoto wa Gadhafi
1. Muhammad
Mtoto wa kwanza wa Gadhafi na mkewe wake wa kwanza, Fatiha waliyetengana naye miezi sita tu baada ya ndoa yao.
Muhammad ni kiongozi wa kamati ya olimpiki na ni mwenyekiti wa shirika la Posta na mawasiliano-telecom co.
2. Saif al-Islam
Heir apparent Saif al-Islam has a PHd. From the London School of Economics
Mtoto wa pili wa Dhadafi - umri miaka 38, and Phd katika masuala ya Uchumi.
Kwa kutumia Charity organization ya baba yake, alitoa misaada mingi sana kipindi kile haiti ilipoharibiwa na tetemeko la ardhi.
Walibya wengi wanadhani ni mtu mwadilifu anayefaa hata kuiongoza Libya baada ya baba yake. Hata hivyo, ukweli ni kwamba ni fisadi mdogo anayemiliki hisa nyingi ktk makampuni ya mafuta yaliyowekeza Libya. Pia anapenda wanawake, na katika tukio moja, inasadikika kuwa aliwahi kumlipa Mariah Carey dola za kimarekani millioni moja ili kuonyesha tamasha la muziki.
Hivi karibuni, wakati waandamanaji wakijitokeza kwa wingi kumpinga baba yake, alitokea kwenye televisheni ya taifa na kuwaita waandamanaji walevi, watumia dawa za kulevya na magaidi.
3. Saadi Gadhafi
Saadi Gadhafi- A senior Engineer and Former pro soccer player with a troubled past
Saadi ni mtoto wa tatu wa kiume wa Gadhafi mwenye historia mbaya ya maisha kwa ujumla, ikiwa ni pamoja na kupambana na polisi katika nchi kadhaa za ulaya hasa Italia kuhusiana na matumizi ya pombe na madawa ya kulevya. Aliwahi kuwa mcheza soka wa kulipwa huko Italia lakini akafukuzwa katika kikosi kwa kutumia dawa za kulevya.
4. Muatassim
Mtoto wa nne wa kiume wa Gadhafimwenye ushindani mkubwa na Saif katika kutaka kurithi biashara ya familia ya Gadhafi.
Alikosana na baba yake na kulazimika kwenda kuishi maisha ya kikimbizi nchini Misri mwaka 1990 . Aliruhusiwa kurudi nyumbani mwaka 2006 na kuchaguliwa kuwa mashauri wa mambo ya kiusalama. Mwaka 2009, alitembelea washington na kubahatika kukutana na mkuu wa wa Idara ya mambo ya nje ya Marekani Bi. Hillary Rodham Clinton kitendo ambacho kilimkasirisha sana Saif. Muatassim inadaiwa pia aliwahi kumlipa mamilioni ya dola za kimarekani Beyonce na Usher katika party moja ya mwaka mpya huko St. Barts.
5. Hannibal
Ni mtoto wa tano wa kiume wa Gadhafi. Inashukiwa pia kuwa aliwahi kumpiga mkewe Aline mara kwa mara. Aliwahi kufukuzwa katika hoteli moja huko London baada ya kumpiga mkewe na kumjeruhi usoni. Hali hii ilimlazimu mtoto wa kike wa Gadhafi, Aisha (ambaye alikuwa mja mzito karibia na kuzaa) kwenda London kusuluhisha ugomvi huo na kudanganya kuwa Aline aliumia katika ajali.
Hannibal alikuwa pia anatabia isiyo ya kawaida na alijihusisha na matukio mengi ya ajabu ajabu huko ulaya. Inasemekana kuwa, mwaka 2001 katika hoteli ya Rome aliwashambulia polisi watatu kwa kutumia gasi ya kuzimia moto Fire extinguisher na pia aliwahi kufanya shambulizi kwa wafanyakazi wake wapambe huko Geneva mwaka 2008. Alikamatwa na polisi na kufunguliwa mashitaka, hata hivyo aliachiwa baada ya siku mbili tu. Kwa tukio hilo, Libya ilizuia uingizaji wa bidhaa zote za Switzerland, ikazuia utoaji viza kwa raia wa Switzerland na kulazimisha makampuni yote ya nchi hiyo kufunga offisi zake huko Libya.
6.Khamis
Ni mtoto wa sita wa kiume wa Gadhafi ambaye hajulikani sana.
Ni kamanda wa kivita anayeheshimika sana katika vikosi maalum na mtetezi mkubwa wa sera za baba yake.
Amepata mafunzo ya kijeshi Russia na ana PhD katika millitary sciences aliyopipata mwaka 2007.
Anaongoza kikosi cha 32 Brigedi ambayo inajulikana kama ni mojawapo ya vikosi madhubuti sana chenye mafunzo ya hali ya juu na na vifaa vya kisasa kabisa katika jeshi la Libya. Kikosi hiki kinaaminika kuwa ndicho kimeshiriki sana katika kuwashambulia waandamanaji wanaoipinga serikali ya Bwana Gadhafi.
7.Aisha Gadhafi
Aisha Gadhafi is a trained lawyer who served on Saddam Husseins defence team.
Mtoto pkee wa Kike wa Gadhafi ambaye anaaminika kama ndiye shauri wa familia yenye matatizo ya Gadhafi.
Aisha, alichochea kwa kiasi kikubwa mzozo kati ya Libya na Uswisi kufuatia kukamatwa kwa kaka yake Hannibal na hivyo kuongeza hasira ya baba yake katika mzozo huo. Aisha alilikuza tatizo hilo kiasi ambacho ilishindikana kupatikana kwa suluhisho kati ya nchi hizo mbili
8.Saif al-Arab
Mtoto wa nane wa Gadhafi anayeishi Ujerumani katika mji wa Munich.
Inasemekana anafanya biashara sizizohalali na anamatumizi makubwa katika kujimwaga yaani party.
Serikali ya Uerumani imeanza kumnyooshea kidole dogo huyu na ni jambo la muda tu kila kitu serikali itachukua hatua kwa kufuatia mwenendo hali wa mzozo unaoendelea Libya kwa baba yake.
Hiyo ndiyo orodha ya watoto WATUKUTU WA MFALME GADHAFI KAMA ANAVYOJIITA YEYE.
KWELI MTOTO WA NYOKA NI NYOKA TU