Ijengwe nidhamu ya kujibu masuala ya nchi Kimataifa. Kila mtu amekuwa msemaji wa Serikali

Tulimumu

JF-Expert Member
Mar 11, 2013
14,305
12,968
Kuna tatizo kubwa limejitokeza sasa hivi kama nchi ambapo kila tuhuma inayoihusu nchi wanaibuka watu kujibu kama wasemaji wa serikali na nchi wakati wasemaji wapo. Kila mmoja anatafuta kuwa mtetezi wa serikali. Na katika kufanya hivi ndipo makosa yatokea zaidi.

Angalia sasa mfano wa matukio mawili ya hivi sasa la Zitto na benki ya Dunia na hili la Marekani na Makonda. Wameibuka watu wanatangaza hadharani tena wakiwa kwenye mihimili ya nchi kuwa Zitto auwawe. Mwingine kaamka alikoamkia kaandika barua kuijibu Marekani na eti kapeleka nakala kwa rais. Unajiuliza je rais alimtuma? Hivi waziri wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa atafanya kazi gani kama kila mtu ni msemaji wa serikali.

Kila mtu anaongea. Sasa tumsikilize nani na nani yupo sahihi? Hawa wasemaji wa kujitolea ni vizuri wapigwe pini wanaiaibisha serikali na kuifanya dhalili. Wanatafuta sifa na vyeo matokeo yake wanatupoteza. Miluzi mingi ilimpoteza mbwa!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukisikia watu wanasema "serikali dhaifu" hii ndo maana yake. Uliona wapi serikali ya nchi haina uwezo badala yake imekaa kutegemea itetewe na "wanaharakati"!
Mnyonge ndio anayepaswa kutetewa, na mtetezi ni lazima awe na uwezo/nguvu zaidi au inayolingana na muonevu.

Mtu kama Misiba au Msando wanatambua udhaifu wa serikali hii na kwa hiyo wameamua"kujitoa muhanga" dhidi ya waonevu. Kujitoa muhanga maana yake ni kwamba wanajitambua kuwa ingawa wajitolea kuitetea serikali, bado na wao hawana nguvu/uwezo unaolingana au kuwashinda wale wanoionea serikali na kwa maana hiyo lolote baya linaweza kuwapata katika "harakati" zao za "kuitetea" serikali.
 
Ukisikia watu wanasema "serikali dhaifu" hii ndo maana yake. Uliona wapi serikali ya nchi haina uwezo badala yake imekaa kutegemea itetewe na "wanaharakati"!
Mnyonge ndio anayepaswa kutetewa, na mtetezi ni lazima awe na uwezo/nguvu zaidi au inayolingana na muonevu.

Mtu kama Misiba au Msando wanatambua udhaifu wa serikali hii na kwa hiyo wameamua"kujitoa muhanga" dhidi ya waonevu. Kujitoa muhanga maana yake ni kwamba wanajitambua kuwa ingawa wajitolea kuitetea serikali, bado na wao hawana nguvu/uwezo unaolingana au kuwashinda wale wanoionea serikali na kwa maana hiyo lolote baya linaweza kuwapata katika "harakati" zao za "kuitetea" serikali.
 
Uko sahihi mkuu. Ndiyo maana kila sehemu ina msemaji wake maana huwezi kuongelea kitu ambacho hukifahamu. Mfano wasemaji huwa wanaongea yale ambayo yamejadiliwa na wakubwa wao katika sehemu walizopo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe unaunga mkono kitu ambacho wala hujui! Nani kakudanganya kuwa maoni binafsi ya raia mitaani ni majibu ya serikali? Nani kakuambia hiyo barua ni majibu ya serikali? Haya siyo majibu ya serikali bali ni maoni binafsi ya mtu na hata wewe ukitaka andika. Ndiyo uhuru wa kujieleza huo!
 
Ni ushamba uliosababishwa na tabia ya jiwe kutaka kusifiwa. Waimba mapambio wanapigana vikumbo kuwa wa kwanza kusifu na ndio asili ya vituko vinavyoendelea leo.
Watanzania tunaaibishwa hasa na serikali hii. Imesababisha wote tunaonekane kuwa washamba huko nje.
 
Mtu aliyefumaniwa na Giggy Money leo ndio kawa msemaji wa serikali kimataifa !
Na wewe usiwe chini ya kiwango namna hii ndugu! Serikali imesema ndiyo imemtuma kujibu? Unajifanya kuwa hujui kama serikali ina channels zake maalum za kutoa matamko? Ile barua ni mtu kaamua kutumia fursa ya kutoa mawazo (au ukitaka kuwa sahihi zaidi unaweza kusema ni mtu ameona kuna fursa ya kupalilia ''shamba'' lake akitegemea ''mvua'' itanyesha muda wowote.
 
Kuna tatizo kubwa limejitokeza sasa hivi kama nchi ambapo kila tuhuma inayoihusu nchi wanaibuka watu kujibu kama wasemaji wa serikali na nchi wakati wasemaji wapo. Kila mmoja anatafuta kuwa mtetezi wa serikali. Na katika kufanya hivi ndipo makosa yatokea zaidi.

Angalia sasa mfano wa matukio mawili ya hivi sasa la Zitto na benki ya Dunia na hili la Marekani na Makonda. Wameibuka watu wanatangaza hadharani tena wakiwa kwenye mihimili ya nchi kuwa zitto auwawe. Mwingine kaamka alikoamkia kaandika barua kuijibu Marekani na eti kapeleka nakala kwa rais. Unajiuliza je rais alimtuma? Hivi waziri wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa atafanya kazi gani kama kila mtu ni msemaji wa serikali.

Kila mtu anaongea. Sasa tumsikilize nani na nani yupo sahihi? Hawa wasemaji wa kujitolea ni vizuri wapigwe pini wanaiaibisha serikali na kuifanya dhalili. Wanatafuta sifa na vyeo matokeo yake wanatupoteza. Miluzi mingi ilimpoteza mbwa!

Sent using Jamii Forums mobile app
Uhuru wa kujieleza ni uhuru wa msingi wa kikatiba.

Usiwanyime watu uhuru wao.

Serikali ina wasemaji wake, ikitaka kujibu jibu rasmi itawatumia.

Wananchi wakijieleza wanatumia uhuru wao wa kujieleza ambao upo katika katiba.

Au katiba hujaisoma?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna tatizo kubwa limejitokeza sasa hivi kama nchi ambapo kila tuhuma inayoihusu nchi wanaibuka watu kujibu kama wasemaji wa serikali na nchi wakati wasemaji wapo. Kila mmoja anatafuta kuwa mtetezi wa serikali. Na katika kufanya hivi ndipo makosa yatokea zaidi.

Angalia sasa mfano wa matukio mawili ya hivi sasa la Zitto na benki ya Dunia na hili la Marekani na Makonda. Wameibuka watu wanatangaza hadharani tena wakiwa kwenye mihimili ya nchi kuwa zitto auwawe. Mwingine kaamka alikoamkia kaandika barua kuijibu Marekani na eti kapeleka nakala kwa rais. Unajiuliza je rais alimtuma? Hivi waziri wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa atafanya kazi gani kama kila mtu ni msemaji wa serikali.

Kila mtu anaongea. Sasa tumsikilize nani na nani yupo sahihi? Hawa wasemaji wa kujitolea ni vizuri wapigwe pini wanaiaibisha serikali na kuifanya dhalili. Wanatafuta sifa na vyeo matokeo yake wanatupoteza. Miluzi mingi ilimpoteza mbwa!

Sent using Jamii Forums mobile app
Huyu Bulembo, Binti yake si aliolewa na Zitto, imekuwaje?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna tatizo kubwa limejitokeza sasa hivi kama nchi ambapo kila tuhuma inayoihusu nchi wanaibuka watu kujibu kama wasemaji wa serikali na nchi wakati wasemaji wapo. Kila mmoja anatafuta kuwa mtetezi wa serikali. Na katika kufanya hivi ndipo makosa yatokea zaidi.

Angalia sasa mfano wa matukio mawili ya hivi sasa la Zitto na benki ya Dunia na hili la Marekani na Makonda. Wameibuka watu wanatangaza hadharani tena wakiwa kwenye mihimili ya nchi kuwa zitto auwawe. Mwingine kaamka alikoamkia kaandika barua kuijibu Marekani na eti kapeleka nakala kwa rais. Unajiuliza je rais alimtuma? Hivi waziri wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa atafanya kazi gani kama kila mtu ni msemaji wa serikali.

Kila mtu anaongea. Sasa tumsikilize nani na nani yupo sahihi? Hawa wasemaji wa kujitolea ni vizuri wapigwe pini wanaiaibisha serikali na kuifanya dhalili. Wanatafuta sifa na vyeo matokeo yake wanatupoteza. Miluzi mingi ilimpoteza mbwa!

Sent using Jamii Forums mobile app

Uhuru wa kuongea uheshimiwe. Ha ha ha ha
 
Uhuru wa kujieleza ni uhuru wa msingi wa kikatiba.

Usiwanyime watu uhuru wao.

Serikali ina wasemaji wake, ikitaka kujibu jibu rasmi itawatumia.

Wananchi wakijieleza wanatumia uhuru wao wa kujieleza ambao upo katika katiba.

Au katiba hujaisoma?

Sent using Jamii Forums mobile app
Uhuru huu huu ndio ameutumia Zitto, lakini wengine wanataka auawe. Hapo inakuwaje?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inashangaza mno maana hata hao waliokwenda kushitaki huko nje sidhani kama tuliwatuma, ni vihere here vyao tu na kutafuta sifa.
 
Back
Top Bottom