Igunga: Viongozi wa CCM wakamatwa kwa kuchoma bendera za CHADEMA

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
  • Makada wake wakamatwa kwa kuchoma bendera za Chadema
JESHI la Polisi Wilayani Igunga mkoani Tabora, linawashikilia kiongozi mmoja na kada mwingine wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kosa kuchoma mabango ya picha ya mgombea ubunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na kushusha bendera za chama hicho.

Waliotiwa mbaroni juzi jioni ni Katibu wa Msaidizi wa CCM ambaye pia ni Mhasibu wa CCM Wilaya ya Sikonge, Bw. Bakari Luasa na Bw. Rajabu Said ambao walikamatwa katika kijiji cha Chagana Kata ya Itumba.

Viongozi hao, walikamatwa saa 5:00 asubuhi juzi muda mfupi kabla ya msafara wa mgombea wa CCM, Dkt. Dalaly Kafumu na Katibu Mkuu wa chama hicho, Bw. Wilson Mukama na viongozi wengine kuwasili eneo hilo.

Bw. Mukama na msafara wake walikuta tafrani baada ya wafuasi wa Chadema kuwashikilia viongozi hao na kuwadhiti hadi walipowakabidhi kwa polisi.

Makada hao wa CCM walipandishwa kwenye gari la polisi aina ya Toyota Land Cruiser yenye namba za usajili PT 1946 hadi Kituo cha Polisi mjini Igunga ambako walikabidhiwa kwa Mkuu wa Kitengo cha Tathmini, Ufuatiliaji na Upelelezi wa Makosa ya Jinai katika uchaguzi huu, Bw. Isaya Mngulu.

Wakazi wa kijiji hicho wakiwamo wafuasi wa Chadema walikuwa na marungu, mapanga na mikuki ili kuwashughulikia, lakini jitihada zilizofanywa na kiongozi mmoja wa Chadema, Bw. Kibende Mwang'ombe ziliwatuliza.

Mwang'ombe aliiambia Majira kuwa waliokamatwa walifika katika eneo hilo kufanya uhalifu wakiwa na mtu mwingine ambaye jina lake halikufamika mara moja, lakini alikimbia baada ya ugomvi kuanza.

"Siku zote CCM wemekuwa mabingwa wa kueneza siasa za propaganda kwamba Chadema tunafanya fujo, nadhani ninyi wenyewe mmejionea. Jambo lililonifurahisha ni kwamba viongozi waandamizi wa CCM wamejionea wenyewe," alisema Mwang'ombe.

Mwenyekiti wa Wazazi CCM Wilaya ya Igunga, Bw. Selemani Majilanga, aliwaomba wananchi na wafuasi wa Chadema wasiwafanyie fujo wahalifu hao.

"Nawaomba ndugu zangu wananchi msifanye fujo kwa watu hao, wako mikononi mwa polisi, basi acheni sheria ichukue mkondo wake, watashughulikiwa kwa taratibu zote zinazostahili," alisema Majilanga.

Baada ya watuhumiwa kuondolewa, mkutano huo, uliendelea huku, Bw. Mukama akijinadi kwa wananchi kuwa ametumwa na Rais Jakata Kikwete kuwaomba wananchi hao kumpa kura za ndiyo mgombea wa CCM, Dkt. Kafumu ili awe mbunge wao.

Kwa upende wake, Mratibu wa Kampeni wa CCM ambaye pia ni Katibu wa Fedha na Uchumi, Bw. Mwigulu Nchemba aliwataka wananchi kutokuchagua wapinzani kwa sababu hawana serikali.

Katika mkutano huo, mwananchi mmoja alilipandisha dumu la maji machafu lita 20 na kumuuliza mgombea wa CCM, Dkt. Kafumu atachukua hatua gani kuondoa adha ya kukosa maji iliyodumu miaka mingi.

"Nimekuletea maji haya unayoone mwenyewe, sisi tunakunywa maji machafua kiasi hiki, je, ukipata ubunge utafanyaje ili tuondokane na aibu hii ambayo sasa imeonekana kuwa ya kawaida kila kukicha," alihoji mwananchi huyo.

SOURCE: MAJIRA
 
CCM na polisi wao bado wanafanya danganya toto kwa kuwakamata watu ambao hawana influence kwenye chama. wapo wahalifu wengi akiwepo Mukama, Msekwa, John komba lakini hawakamatwi.

Adhabu yao kwenye sanduku la kura.
 
Na Waandishi Wetu, Igunga, Dar

JESHI la Polisi Wilayani Igunga mkoani Tabora, linawashikilia kiongozi mmoja na kada mwingine wa
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kosa kuchoma mabango ya picha ya mgombea ubunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na kushusha bendera za chama hicho.

Waliotiwa mbaroni juzi jioni ni Katibu wa Msaidizi wa CCM ambaye pia ni Mhasibu wa CCM Wilaya ya Sikonge, Bw. Bakari Luasa na Bw. Rajabu Said ambao walikamatwa katika kijiji cha Chagana Kata ya Itumba.
Viongozi hao, walikamatwa saa 5:00 asubuhi juzi muda mfupi kabla ya msafara wa mgombea wa CCM, Dkt. Dalaly Kafumu na Katibu Mkuu wa chama hicho, Bw. Wilson Mukama na viongozi wengine kuwasili eneo hilo.

Bw. Mukama na msafara wake walikuta tafrani baada ya wafuasi wa Chadema kuwashikilia viongozi hao na kuwadhiti hadi walipowakabidhi kwa polisi.

Makada hao wa CCM walipandishwa kwenye gari la polisi aina ya Toyota Land Cruiser yenye namba za usajili PT 1946 hadi Kituo cha Polisi mjini Igunga ambako walikabidhiwa kwa Mkuu wa
Kitengo cha Tathmini, Ufuatiliaji na Upelelezi wa Makosa ya
Jinai katika uchaguzi huu, Bw. Isaya Mngulu.

Wakazi wa kijiji hicho wakiwamo wafuasi wa Chadema walikuwa na marungu, mapanga na mikuki ili kuwashughulikia, lakini jitihada zilizofanywa na kiongozi mmoja wa Chadema, Bw. Kibende Mwang’ombe ziliwatuliza.

Mwang’ombe aliiambia Majira kuwa waliokamatwa walifika katika
eneo hilo kufanya uhalifu wakiwa na mtu mwingine ambaye jina lake halikufamika mara moja, lakini alikimbia baada ya ugomvi kuanza.

“Siku zote CCM wemekuwa mabingwa wa kueneza siasa za
propaganda kwamba Chadema tunafanya fujo, nadhani ninyi
wenyewe mmejionea. Jambo lililonifurahisha ni kwamba viongozi waandamizi wa CCM wamejionea wenyewe,” alisema Mwang’ombe.

Mwenyekiti wa Wazazi CCM Wilaya ya Igunga, Bw. Selemani Majilanga, aliwaomba wananchi na wafuasi wa Chadema wasiwafanyie fujo wahalifu hao.

“Nawaomba ndugu zangu wananchi msifanye fujo kwa watu hao, wako
mikononi mwa polisi, basi acheni sheria ichukue mkondo wake, watashughulikiwa kwa taratibu zote zinazostahili,” alisema Majilanga.

Baada ya watuhumiwa kuondolewa, mkutano huo, uliendelea huku, Bw. Mukama akijinadi kwa wananchi kuwa ametumwa na Rais Jakata Kikwete kuwaomba wananchi hao kumpa kura za ndiyo mgombea
wa CCM, Dkt. Kafumu ili awe mbunge wao.

Kwa upende wake, Mratibu wa Kampeni wa CCM ambaye pia ni
Katibu wa Fedha na Uchumi, Bw. Mwigulu Nchemba aliwataka
wananchi kutokuchagua wapinzani kwa sababu hawana serikali.

Katika mkutano huo, mwananchi mmoja alilipandisha dumu la
maji machafu lita 20 na kumuuliza mgombea wa CCM, Dkt. Kafumu atachukua hatua gani kuondoa adha ya kukosa maji iliyodumu miaka mingi.

“Nimekuletea maji haya unayoone mwenyewe, sisi tunakunywa
maji machafua kiasi hiki, je, ukipata ubunge utafanyaje ili
tuondokane na aibu hii ambayo sasa imeonekana kuwa ya
kawaida kila kukicha,” alihoji mwananchi huyo.

Madai ya wanazuoni wa kiislamu

Chadema kimesema kuwa hakiko tayari kujibizana na wanazuoni wa kiislamu bali kinasubiri uamuzi wa mahakama utakaoamua iwapo Mkuu wa Wilaya ya Igunga, Bi. Fatma Kimario alivuliwa hijabu kwa makusudi alipokamatwa na wafuasi wa chama hicho.

Hatua hiyo ya Chadema imekuja siku moja baada ya Wanazuoni wa Kiislamu nchini (HAY AT) kukitaka chama hicho kulaani na kumuomba radhi Mkuu wa Wilaya ya Igunga, Bi. Fatma Kimario kwa kumvua sitaha yake na hivyo kumdhalilisha.

Akizungumza na wandishi wa habari Makao Makuu ya Chama hicho, Mjumbe Kamati Kuu ya CHADEMA Prof. Abdallah Safari alisema kuwa chama hicho hakiko tayari kujibizana na wanazuoni hao.

"Si vizuri kuzungumzia mambo ambayo yako mahakamani lakini mahakama itaamua kama DC Fatma alivuliwa hijabu na kama alivuliwa ni kwa makusudi gani, ni uamuzi wa mahakama pekee ndio utaokaomua," alisema Prof Safari.

Alisema kuwa Chadema haina sera ya udini kwa hiyo hakiwezi kushabikia mtu kuvuliwa hijabu kwa makusudi huku akionya viongozi wa dini kuacha kutoa taarifa zinazopotosha ukweli na zinazolenga kuvuruga mshikamano wa Watanzania.

Prof. Safari ambaye ni mwanasheria na mwanazuoni wa kiisalamu, alisema kauli hizo zina lengo la kufarakanisha umma wa waislamu na chama hicho ambacho kinalengo la kuwaondoa madarakani viongozi wanaodaiwa kunuka ufisadi wa CCM

Helkopta kukata anga

Wakati huo huo Chadema kinategemewa kuanza kutumia helkopta kurudia kampeni katika Kata zote 26, lengo likiwa ni kuwakumbusha wananchi na kuwahamasisha kukichagua chama hicho zikiwa zimebaki siku tisa kufika uchaguzi.

Nyumba ya Katibu CUF yachomwa

Nyumba ya Katibu Kata wa Kata ya Nyandekwa, Bw. Hamisi Makala imeteketea kwa moto na vitu vyote vilivyokuwemo ndani.

Mratibu wa CUF Kata ya Nyandekwa, Bw. Emmanuel Ezekiel alisema wakati akifungua mkutano wa kampeni za kumnadi mgombea wa chama hicho kuwa tukio linahusishwa na mambo ya kisiasa.

Kutoka na matukio ya kihalifu yanayoendelea katika jimbo la Igunga ambako kampeni za uchaguzi mdogo zikiendelea kushika kasi, CUF imewataka wananchi kuacha kujiingiza kwenye siasa za chuki.

Mjumbe wa Baraza Kuu Taifa wa CUF, Bw. Mbarara Maharagande akimwombea kura mgombea Ubunge wa chama hicho, Bw. Leopold Mahona alisema siasa za kumwaga damu zisipewe nafasi kwani zinajenga uhasama kwa wana Igunga wakati waliosababisha hayo wakitanua Dar es Salaam na familia zao.

Mkuu wa Polisi Wilaya ya Igunga alithibitisha kutokea tukio hilo la moto na kumwagiza Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya kufanya upelelezi haraka.

CHANZO: GAZETI LA MAJIRA
 
Yule aliyemtafuna mke wa kanda wenzake kafikishwa vyombo vya dola au yamemalizwa ki utu uzima?
 
Wanao sababisha amani kuvurugika katika kampeni za uchaguzi hapa tanzania ni;

(a)polisi wasio taka kutenda haki.
(b)wasimamizi wa uchaguzi na wakuu wa wilaya.
(c)viongozi wa ngazi za juu wano amuru polisi kufanya wanavyo taka na siyo polisi walivyo ona inafaaa.
(d)waroho wa madaraka wanaopendelea ccm kwa makusudi kwa matarajio ya kupandishwa vyeo.
 
  • Makada wake wakamatwa kwa kuchoma bendera za Chadema
JESHI la Polisi Wilayani Igunga mkoani Tabora, linawashikilia kiongozi mmoja na kada mwingine wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kosa kuchoma mabango ya picha ya mgombea ubunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na kushusha bendera za chama hicho.

Waliotiwa mbaroni juzi jioni ni Katibu wa Msaidizi wa CCM ambaye pia ni Mhasibu wa CCM Wilaya ya Sikonge, Bw. Bakari Luasa na Bw. Rajabu Said ambao walikamatwa katika kijiji cha Chagana Kata ya Itumba.

Viongozi hao, walikamatwa saa 5:00 asubuhi juzi muda mfupi kabla ya msafara wa mgombea wa CCM, Dkt. Dalaly Kafumu na Katibu Mkuu wa chama hicho, Bw. Wilson Mukama na viongozi wengine kuwasili eneo hilo.

Bw. Mukama na msafara wake walikuta tafrani baada ya wafuasi wa Chadema kuwashikilia viongozi hao na kuwadhiti hadi walipowakabidhi kwa polisi.

Makada hao wa CCM walipandishwa kwenye gari la polisi aina ya Toyota Land Cruiser yenye namba za usajili PT 1946 hadi Kituo cha Polisi mjini Igunga ambako walikabidhiwa kwa Mkuu wa Kitengo cha Tathmini, Ufuatiliaji na Upelelezi wa Makosa ya Jinai katika uchaguzi huu, Bw. Isaya Mngulu.

Wakazi wa kijiji hicho wakiwamo wafuasi wa Chadema walikuwa na marungu, mapanga na mikuki ili kuwashughulikia, lakini jitihada zilizofanywa na kiongozi mmoja wa Chadema, Bw. Kibende Mwang’ombe ziliwatuliza.

Mwang’ombe aliiambia Majira kuwa waliokamatwa walifika katika eneo hilo kufanya uhalifu wakiwa na mtu mwingine ambaye jina lake halikufamika mara moja, lakini alikimbia baada ya ugomvi kuanza.

“Siku zote CCM wemekuwa mabingwa wa kueneza siasa za propaganda kwamba Chadema tunafanya fujo, nadhani ninyi wenyewe mmejionea. Jambo lililonifurahisha ni kwamba viongozi waandamizi wa CCM wamejionea wenyewe,” alisema Mwang’ombe.

Mwenyekiti wa Wazazi CCM Wilaya ya Igunga, Bw. Selemani Majilanga, aliwaomba wananchi na wafuasi wa Chadema wasiwafanyie fujo wahalifu hao.

“Nawaomba ndugu zangu wananchi msifanye fujo kwa watu hao, wako mikononi mwa polisi, basi acheni sheria ichukue mkondo wake, watashughulikiwa kwa taratibu zote zinazostahili,” alisema Majilanga.

Baada ya watuhumiwa kuondolewa, mkutano huo, uliendelea huku, Bw. Mukama akijinadi kwa wananchi kuwa ametumwa na Rais Jakata Kikwete kuwaomba wananchi hao kumpa kura za ndiyo mgombea wa CCM, Dkt. Kafumu ili awe mbunge wao.

Kwa upende wake, Mratibu wa Kampeni wa CCM ambaye pia ni Katibu wa Fedha na Uchumi, Bw. Mwigulu Nchemba aliwataka wananchi kutokuchagua wapinzani kwa sababu hawana serikali.

Katika mkutano huo, mwananchi mmoja alilipandisha dumu la maji machafu lita 20 na kumuuliza mgombea wa CCM, Dkt. Kafumu atachukua hatua gani kuondoa adha ya kukosa maji iliyodumu miaka mingi.

“Nimekuletea maji haya unayoone mwenyewe, sisi tunakunywa maji machafua kiasi hiki, je, ukipata ubunge utafanyaje ili tuondokane na aibu hii ambayo sasa imeonekana kuwa ya kawaida kila kukicha,” alihoji mwananchi huyo.

SOURCE: MAJIRA

tia maji tia maji, CCM ZIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIII
 
"Kwa upende wake, Mratibu wa Kampeni wa CCM ambaye pia ni Katibu wa Fedha na Uchumi, Bw. Mwigulu Nchemba aliwataka wananchi kutokuchagua wapinzani kwa sababu hawana serikali".
Kumbe usipokuwa na serikali hupaswi kuchaguliwa?Sasa tunashirikisha vyama vya upinzani kwenye chaguzi kwa sababu zipi?
 
atafikishwa vyombo vya dola vipi wakati dola lenyewe ni la magamba??

kuzini na mke wa mtu hata kama wa rais hakuna jinai, kuna madai tu wakubwa.na mlalamikaji inabidi aende mahakamani kufungua kesi ya madai dhidi ya mwizi wake. Polisi hapo hawahusiki kabisaaaaa
 
Kweli nguvu ya CDM si mchezo wana washikilia viongozi hao wa magamba na kuwakabidhi polisi? Basi magamba hawana watu wa kuwaunga mkono na madhambi yao safari yao kwenda mapumzikoni( akhera) imewadia
 
"....Bw. Mukama na msafara wake walikuta tafrani baada ya wafuasi wa Chadema kuwashikilia viongozi hao na kuwadhiti hadi walipowakabidhi kwa polisi.Makada hao wa CCM walipandishwa kwenye gari la polisi aina ya Toyota Land Cruiser yenye namba za usajili PT 1946 hadi Kituo cha Polisi mjini Igunga ambako walikabidhiwa kwa Mkuu wa Kitengo cha Tathmini, Ufuatiliaji na Upelelezi wa Makosa ya Jinai katika uchaguzi huu, Bw. Isaya Mngulu." Kama hli lina ukweli basi Polisi mwezi huu wapunguziwe mishahara, yani walikuwa wapi hadi Makamanda wa CDM wanakamata wezi halafu waje na LandCruiser tu kuwachukua? hakika hawastahili kulipwa salary hawa, labda sisiemu chama cha The walking Corpse kiwalipe wao....
 
CCM na polisi wao bado wanafanya danganya toto kwa kuwakamata watu ambao hawana influence kwenye chama. wapo wahalifu wengi akiwepo Mukama, Msekwa, John komba lakini hawakamatwi.

Adhabu yao kwenye sanduku la kura.

Very true.!
 
*Makada wake wakamatwa kwa kuchoma bendera za Chadema
*Mukama awaangukia wananchi, adai ametumwa na Kikwete
*Prof. Safari awajibu wanazuoni wa kiislamu kuhusu DC
*Nyumba ya Katibu Kata wa CUF Nyandekwe yachomwa moto


Na Waandishi Wetu, Igunga, Dar

JESHI la Polisi Wilayani Igunga mkoani Tabora, linawashikilia kiongozi mmoja na kada mwingine wa
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kosa kuchoma mabango ya picha ya mgombea ubunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na kushusha bendera za chama hicho.

Waliotiwa mbaroni juzi jioni ni Katibu wa Msaidizi wa CCM ambaye pia ni Mhasibu wa CCM Wilaya ya Sikonge, Bw. Bakari Luasa na Bw. Rajabu Said ambao walikamatwa katika kijiji cha Chagana Kata ya Itumba.
Viongozi hao, walikamatwa saa 5:00 asubuhi juzi muda mfupi kabla ya msafara wa mgombea wa CCM, Dkt. Dalaly Kafumu na Katibu Mkuu wa chama hicho, Bw. Wilson Mukama na viongozi wengine kuwasili eneo hilo.

Bw. Mukama na msafara wake walikuta tafrani baada ya wafuasi wa Chadema kuwashikilia viongozi hao na kuwadhiti hadi walipowakabidhi kwa polisi.

Makada hao wa CCM walipandishwa kwenye gari la polisi aina ya Toyota Land Cruiser yenye namba za usajili PT 1946 hadi Kituo cha Polisi mjini Igunga ambako walikabidhiwa kwa Mkuu wa
Kitengo cha Tathmini, Ufuatiliaji na Upelelezi wa Makosa ya
Jinai katika uchaguzi huu, Bw. Isaya Mngulu.

Wakazi wa kijiji hicho wakiwamo wafuasi wa Chadema walikuwa na marungu, mapanga na mikuki ili kuwashughulikia, lakini jitihada zilizofanywa na kiongozi mmoja wa Chadema, Bw. Kibende Mwang’ombe ziliwatuliza.

Mwang’ombe aliiambia Majira kuwa waliokamatwa walifika katika
eneo hilo kufanya uhalifu wakiwa na mtu mwingine ambaye jina lake halikufamika mara moja, lakini alikimbia baada ya ugomvi kuanza.

“Siku zote CCM wemekuwa mabingwa wa kueneza siasa za
propaganda kwamba Chadema tunafanya fujo, nadhani ninyi
wenyewe mmejionea. Jambo lililonifurahisha ni kwamba viongozi waandamizi wa CCM wamejionea wenyewe,” alisema Mwang’ombe.

Mwenyekiti wa Wazazi CCM Wilaya ya Igunga, Bw. Selemani Majilanga, aliwaomba wananchi na wafuasi wa Chadema wasiwafanyie fujo wahalifu hao.

“Nawaomba ndugu zangu wananchi msifanye fujo kwa watu hao, wako
mikononi mwa polisi, basi acheni sheria ichukue mkondo wake, watashughulikiwa kwa taratibu zote zinazostahili,” alisema Majilanga.

Baada ya watuhumiwa kuondolewa, mkutano huo, uliendelea huku, Bw. Mukama akijinadi kwa wananchi kuwa ametumwa na Rais Jakata Kikwete kuwaomba wananchi hao kumpa kura za ndiyo mgombea
wa CCM, Dkt. Kafumu ili awe mbunge wao.

Kwa upende wake, Mratibu wa Kampeni wa CCM ambaye pia ni
Katibu wa Fedha na Uchumi, Bw. Mwigulu Nchemba aliwataka
wananchi kutokuchagua wapinzani kwa sababu hawana serikali.

Katika mkutano huo, mwananchi mmoja alilipandisha dumu la
maji machafu lita 20 na kumuuliza mgombea wa CCM, Dkt. Kafumu atachukua hatua gani kuondoa adha ya kukosa maji iliyodumu miaka mingi.

“Nimekuletea maji haya unayoone mwenyewe, sisi tunakunywa
maji machafua kiasi hiki, je, ukipata ubunge utafanyaje ili
tuondokane na aibu hii ambayo sasa imeonekana kuwa ya
kawaida kila kukicha,” alihoji mwananchi huyo.

Madai ya wanazuoni wa kiislamu

Chadema kimesema kuwa hakiko tayari kujibizana na wanazuoni wa kiislamu bali kinasubiri uamuzi wa mahakama utakaoamua iwapo Mkuu wa Wilaya ya Igunga, Bi. Fatma Kimario alivuliwa hijabu kwa makusudi alipokamatwa na wafuasi wa chama hicho.

Hatua hiyo ya Chadema imekuja siku moja baada ya Wanazuoni wa Kiislamu nchini (HAY AT) kukitaka chama hicho kulaani na kumuomba radhi Mkuu wa Wilaya ya Igunga, Bi. Fatma Kimario kwa kumvua sitaha yake na hivyo kumdhalilisha.

Akizungumza na wandishi wa habari Makao Makuu ya Chama hicho, Mjumbe Kamati Kuu ya CHADEMA Prof. Abdallah Safari alisema kuwa chama hicho hakiko tayari kujibizana na wanazuoni hao.

"Si vizuri kuzungumzia mambo ambayo yako mahakamani lakini mahakama itaamua kama DC Fatma alivuliwa hijabu na kama alivuliwa ni kwa makusudi gani, ni uamuzi wa mahakama pekee ndio utaokaomua," alisema Prof Safari.

Alisema kuwa Chadema haina sera ya udini kwa hiyo hakiwezi kushabikia mtu kuvuliwa hijabu kwa makusudi huku akionya viongozi wa dini kuacha kutoa taarifa zinazopotosha ukweli na zinazolenga kuvuruga mshikamano wa Watanzania.

Prof. Safari ambaye ni mwanasheria na mwanazuoni wa kiisalamu, alisema kauli hizo zina lengo la kufarakanisha umma wa waislamu na chama hicho ambacho kinalengo la kuwaondoa madarakani viongozi wanaodaiwa kunuka ufisadi wa CCM

Helkopta kukata anga

Wakati huo huo Chadema kinategemewa kuanza kutumia helkopta kurudia kampeni katika Kata zote 26, lengo likiwa ni kuwakumbusha wananchi na kuwahamasisha kukichagua chama hicho zikiwa zimebaki siku tisa kufika uchaguzi.

Nyumba ya Katibu CUF yachomwa

Nyumba ya Katibu Kata wa Kata ya Nyandekwa, Bw. Hamisi Makala imeteketea kwa moto na vitu vyote vilivyokuwemo ndani.

Mratibu wa CUF Kata ya Nyandekwa, Bw. Emmanuel Ezekiel alisema wakati akifungua mkutano wa kampeni za kumnadi mgombea wa chama hicho kuwa tukio linahusishwa na mambo ya kisiasa.

Kutoka na matukio ya kihalifu yanayoendelea katika jimbo la Igunga ambako kampeni za uchaguzi mdogo zikiendelea kushika kasi, CUF imewataka wananchi kuacha kujiingiza kwenye siasa za chuki.

Mjumbe wa Baraza Kuu Taifa wa CUF, Bw. Mbarara Maharagande akimwombea kura mgombea Ubunge wa chama hicho, Bw. Leopold Mahona alisema siasa za kumwaga damu zisipewe nafasi kwani zinajenga uhasama kwa wana Igunga wakati waliosababisha hayo wakitanua Dar es Salaam na familia zao.

Mkuu wa Polisi Wilaya ya Igunga alithibitisha kutokea tukio hilo la moto na kumwagiza Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya kufanya upelelezi haraka.
 
Wakazi wa kijiji hicho wakiwamo wafuasi wa Chadema walikuwa na marungu, mapanga na mikuki ili kuwashughulikia, lakini jitihada zilizofanywa na kiongozi mmoja wa Chadema, Bw. Kibende Mwang’ombe ziliwatuliza.

Nimepapenda hapa, nadhani CCM wataanza kuwa na adabu, yaani ingependeza kama wangecharangwa mapanga wageuzwe visusio
 

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom