Na Maggid Mjengwa,
Ndugu zangu,
Wahehe wana msemo unasema: ‘Isenga imbofu na isenga indenyeefu'. Maana yake, ng'ombe kipofu ni sawa tu na ng'ombe aliyevunjika mguu. Wote watakufa njaa. Ng'ombe kipofu hawezi kuyaona majani, na yule aliyevunjika mguu naye hawezi kujikokota kwenda kutafuta nyasi za kula.
Ndugu zangu, Kuna uchaguzi mdogo wa kiti cha ubunge utafanyika jimbo la Igunga. Kuna mengi yanatokea kule Igunga. Tafsiri yangu ; Igunga ni kielelezo cha uendawazimu wetu. Maana, haijapata kutokea katika historia ya nchi hii kwa kiti kimoja cha ubunge kikalifanya taifa zima lizizime. Leo njia zote zinaelekea Igunga.
Msomaji wangu mwuza samaki katika soko la Igunga ananiambia kuwa, Igunga sasa imevamiwa na wageni wengi na biashara yake ya samaki haijapata kuwa nzuri kama ilivyo sasa. Lakini anajua, kuwa baada ya Oktoba 3 biashara yake ya samaki itarudi kuwa ya kusuasua kama zamani.
Na ajabu ya Igunga ni hii; kuwa chanzo chake ni falsafa ya kujivua gamba. Rostam Aziz anasemwa kuwa ni mmoja wa magamba ndani ya chama chake. Akajiuzulu. Kiti cha ubunge kikawa wazi. Na Rostam ' gamba' akarudi Igunga kumwombea kura mgombea wa chama chake. Kioja. Rostam Aziz ametusaidia kutupambanulia zaidi tukajua; kuwa kama taifa tuna gamba tunalopaswa kujivua. Ona kule Igunga, kiti kile cha ubunge kimekuwa chanzo cha kupandikiza chuki zaidi miongoni mwetu Watanzania.
Tunaona kule Igunga; viongozi wa dini wanashiriki siasa za vyama huku wakijua kuwa waumini wao wana tofauti za kiitikadi. Tunaona watendaji wa Serikali wakishiriki kampeni huku wakijua wanaamsha manung'uniko kwa wafuasi wa vyama.
Tunaona vitendo vya kujichukulia sheria mikononi na hata kuwapiga raia, viongozi wa vyama na watendaji wa Serikali vikifanywa na wafuasi wa vyama. Tumeona jinsi uchaguzi wa Igunga ulivyovigawa vyombo vya habari na wanahabari. Tumeona hata kiongozi wa kisiasa akisimama jukwaani akiomba kura akiwa na bastola kiunoni. Tulipofikia ni pabaya sana.
Tumeona, kuwa mabilioni ya shilingi yanatumika kwenye kampeni na huku rushwa ya kuhonga wapiga kura na hata kununua shahada za kupigia kura ikifanyika. Yote haya ni katika kuwania kiti kimoja cha ubunge wa jimbo moja kati ya majimbo zaidi ya mia mbili ya nchi hii. Huu ni
uendawazimu.
Na ajabu ni kuwa uchaguzi wa Igunga ulikuja na sura ya kupambana na ufisadi. Tunachokiona Igunga sasa ni zaidi ya ufisadi. Ni janga. Tuna lazima ya kutafuta namna nyingine ya kuendesha mambo yetu kistaarabu na kulinda hadhi na maslahi ya taifa.
Tuna lazima ya kukaa chini kama taifa na kutafakari mustakabali wetu. Nchi yetu haijaishiwa watu wenye hekima na busara. Maana Inahusu ufisadi uliotamalaki. Na juzi hapa nilimsikia Jaji Mkuu Mstaafu Barnabas Samatta kwenye kipindi hicho cha ' Enzi Hizo' kwenye TBC. Jaji Mkuu Mstaafu Samatta aliongea jambo la hekima sana. Alisema; " Kamwe, umma usikubali kelele dhidi ya rushwa zififie, bali ziongezeke".
Vita inayopiganwa sasa Igunga huenda haina maana yeyote kwetu. Maana, kuna cha kujifunza kutoka kwenye ngano ya mazungumzo baina ya Mfalme Pyrrhic na mpambe wake Cineas. Miaka mingi iliyopita alitokea Mfalme wa Epilus aliyeitwa Pyrrhic.
Mfalme huyu aliamua kuingia vitani kulikabili jeshi kubwa na lenye nguvu nyingi, ni jeshi la Warumi. Lakini kabla ya Mfalme kuingia baharini na vikosi vyake kuitafuta Italia ya Warumi, msaidizi wake wa karibu, Cineas, aliomba mazungumzo ya faragha na Mfalme. Alitaka kumwuliza maswali na kumshauri.
Cineas alimtamkia Mfalme; " E bwana Mfalme, Warumi wanasadikika kuwa na jeshi kubwa , lenye nguvu na lenye mashujaa wengi. Ndio maana wameteka nchi nyingi. Je, Mungu akitusaidia, tukaja kuwashinda Warumi, tutafanya nini na ushindi wetu? Mfalme akajibu: " Mbona hilo ni swali jepesi sana. Mara tutakapowashinda Warumi, hakutatokea jeshi kutoka mji wowote wa Italia litakaloweza kupambana nasi."
Cineas alitulia kidogo, kisha akamwuliza Mfalme: " Tukishaikamata Italia ya Warumi, kipi kitafuatia?"
Mfalme akajibu: Sicily ni kisiwa chenye hazina za thamani kubwa, itakuwa rahisi sana kukiteka kisiwa hicho."
Cineas aliendelea kuuliza: " Bwana Mfalme unaongea juu ya mambo ya kusadikika, lakini una maana kukitwaa kisiwa cha Sicily kutakuwa na maana ya kukoma kwa vita?" Mfalme akajibu: " Hapo tutakuwa tumeikaribia Afrika. Na tukishaikamata Afrika ni nani hapa duniani atathubutu kutukabili kivita?"
" Hakuna" Alijibu Cineas, kisha akauliza; " Na baada ya hapo tutafanya nini?"
Mpaka hapo Mfalme hakujua Cineas alikuwa anampeleka wapi kwa lojiki ya kifikra. Mfalme akajibu: " Baada ya hapo, tutapumzika, tutakula raha. Tutakula na kunywa . Tutabaki tukichekeshana na kucheka, siku nzima."
Kama ni hivyo, alisema Cineas; " Ni kitu gani kinachotuzuia kufanya hayo yote sasa bila kwenda vitani?
Mfalme hakuielewa mantiki ya Cineas. Akakaidi ushauri.
Akavipeleka vikosi vyake kupambana na Warumi. Baada ya vita ngumu, jeshi la mfalme liliwashinda Warumi. Hata hivyo lilipata hasara kubwa ya kupoteza watu na kuwa na majeruhi wengi. Jeshi lake likadhohofika sana. Likajaribu kuitwaa Sparta, likashindwa vibaya sana. Mfalme aliwindwa na hatimaye akakakamatwa na kuuawa kwa kupigwa mawe kwenye mitaa ya Argos. "Isenga imbofu na isenga indenyeefu." Ng'ombe kipofu ni sawa tu na ng'ombe aliyevunjika mguu, wote watakufa njaa. Nahitimisha.
0712 95 61 31 / 0788 111 765/ 0754 678 252
http://mjengwablog.com
Ndugu zangu,
Wahehe wana msemo unasema: ‘Isenga imbofu na isenga indenyeefu'. Maana yake, ng'ombe kipofu ni sawa tu na ng'ombe aliyevunjika mguu. Wote watakufa njaa. Ng'ombe kipofu hawezi kuyaona majani, na yule aliyevunjika mguu naye hawezi kujikokota kwenda kutafuta nyasi za kula.
Ndugu zangu, Kuna uchaguzi mdogo wa kiti cha ubunge utafanyika jimbo la Igunga. Kuna mengi yanatokea kule Igunga. Tafsiri yangu ; Igunga ni kielelezo cha uendawazimu wetu. Maana, haijapata kutokea katika historia ya nchi hii kwa kiti kimoja cha ubunge kikalifanya taifa zima lizizime. Leo njia zote zinaelekea Igunga.
Msomaji wangu mwuza samaki katika soko la Igunga ananiambia kuwa, Igunga sasa imevamiwa na wageni wengi na biashara yake ya samaki haijapata kuwa nzuri kama ilivyo sasa. Lakini anajua, kuwa baada ya Oktoba 3 biashara yake ya samaki itarudi kuwa ya kusuasua kama zamani.
Na ajabu ya Igunga ni hii; kuwa chanzo chake ni falsafa ya kujivua gamba. Rostam Aziz anasemwa kuwa ni mmoja wa magamba ndani ya chama chake. Akajiuzulu. Kiti cha ubunge kikawa wazi. Na Rostam ' gamba' akarudi Igunga kumwombea kura mgombea wa chama chake. Kioja. Rostam Aziz ametusaidia kutupambanulia zaidi tukajua; kuwa kama taifa tuna gamba tunalopaswa kujivua. Ona kule Igunga, kiti kile cha ubunge kimekuwa chanzo cha kupandikiza chuki zaidi miongoni mwetu Watanzania.
Tunaona kule Igunga; viongozi wa dini wanashiriki siasa za vyama huku wakijua kuwa waumini wao wana tofauti za kiitikadi. Tunaona watendaji wa Serikali wakishiriki kampeni huku wakijua wanaamsha manung'uniko kwa wafuasi wa vyama.
Tunaona vitendo vya kujichukulia sheria mikononi na hata kuwapiga raia, viongozi wa vyama na watendaji wa Serikali vikifanywa na wafuasi wa vyama. Tumeona jinsi uchaguzi wa Igunga ulivyovigawa vyombo vya habari na wanahabari. Tumeona hata kiongozi wa kisiasa akisimama jukwaani akiomba kura akiwa na bastola kiunoni. Tulipofikia ni pabaya sana.
Tumeona, kuwa mabilioni ya shilingi yanatumika kwenye kampeni na huku rushwa ya kuhonga wapiga kura na hata kununua shahada za kupigia kura ikifanyika. Yote haya ni katika kuwania kiti kimoja cha ubunge wa jimbo moja kati ya majimbo zaidi ya mia mbili ya nchi hii. Huu ni
uendawazimu.
Na ajabu ni kuwa uchaguzi wa Igunga ulikuja na sura ya kupambana na ufisadi. Tunachokiona Igunga sasa ni zaidi ya ufisadi. Ni janga. Tuna lazima ya kutafuta namna nyingine ya kuendesha mambo yetu kistaarabu na kulinda hadhi na maslahi ya taifa.
Tuna lazima ya kukaa chini kama taifa na kutafakari mustakabali wetu. Nchi yetu haijaishiwa watu wenye hekima na busara. Maana Inahusu ufisadi uliotamalaki. Na juzi hapa nilimsikia Jaji Mkuu Mstaafu Barnabas Samatta kwenye kipindi hicho cha ' Enzi Hizo' kwenye TBC. Jaji Mkuu Mstaafu Samatta aliongea jambo la hekima sana. Alisema; " Kamwe, umma usikubali kelele dhidi ya rushwa zififie, bali ziongezeke".
Vita inayopiganwa sasa Igunga huenda haina maana yeyote kwetu. Maana, kuna cha kujifunza kutoka kwenye ngano ya mazungumzo baina ya Mfalme Pyrrhic na mpambe wake Cineas. Miaka mingi iliyopita alitokea Mfalme wa Epilus aliyeitwa Pyrrhic.
Mfalme huyu aliamua kuingia vitani kulikabili jeshi kubwa na lenye nguvu nyingi, ni jeshi la Warumi. Lakini kabla ya Mfalme kuingia baharini na vikosi vyake kuitafuta Italia ya Warumi, msaidizi wake wa karibu, Cineas, aliomba mazungumzo ya faragha na Mfalme. Alitaka kumwuliza maswali na kumshauri.
Cineas alimtamkia Mfalme; " E bwana Mfalme, Warumi wanasadikika kuwa na jeshi kubwa , lenye nguvu na lenye mashujaa wengi. Ndio maana wameteka nchi nyingi. Je, Mungu akitusaidia, tukaja kuwashinda Warumi, tutafanya nini na ushindi wetu? Mfalme akajibu: " Mbona hilo ni swali jepesi sana. Mara tutakapowashinda Warumi, hakutatokea jeshi kutoka mji wowote wa Italia litakaloweza kupambana nasi."
Cineas alitulia kidogo, kisha akamwuliza Mfalme: " Tukishaikamata Italia ya Warumi, kipi kitafuatia?"
Mfalme akajibu: Sicily ni kisiwa chenye hazina za thamani kubwa, itakuwa rahisi sana kukiteka kisiwa hicho."
Cineas aliendelea kuuliza: " Bwana Mfalme unaongea juu ya mambo ya kusadikika, lakini una maana kukitwaa kisiwa cha Sicily kutakuwa na maana ya kukoma kwa vita?" Mfalme akajibu: " Hapo tutakuwa tumeikaribia Afrika. Na tukishaikamata Afrika ni nani hapa duniani atathubutu kutukabili kivita?"
" Hakuna" Alijibu Cineas, kisha akauliza; " Na baada ya hapo tutafanya nini?"
Mpaka hapo Mfalme hakujua Cineas alikuwa anampeleka wapi kwa lojiki ya kifikra. Mfalme akajibu: " Baada ya hapo, tutapumzika, tutakula raha. Tutakula na kunywa . Tutabaki tukichekeshana na kucheka, siku nzima."
Kama ni hivyo, alisema Cineas; " Ni kitu gani kinachotuzuia kufanya hayo yote sasa bila kwenda vitani?
Mfalme hakuielewa mantiki ya Cineas. Akakaidi ushauri.
Akavipeleka vikosi vyake kupambana na Warumi. Baada ya vita ngumu, jeshi la mfalme liliwashinda Warumi. Hata hivyo lilipata hasara kubwa ya kupoteza watu na kuwa na majeruhi wengi. Jeshi lake likadhohofika sana. Likajaribu kuitwaa Sparta, likashindwa vibaya sana. Mfalme aliwindwa na hatimaye akakakamatwa na kuuawa kwa kupigwa mawe kwenye mitaa ya Argos. "Isenga imbofu na isenga indenyeefu." Ng'ombe kipofu ni sawa tu na ng'ombe aliyevunjika mguu, wote watakufa njaa. Nahitimisha.
0712 95 61 31 / 0788 111 765/ 0754 678 252
http://mjengwablog.com