Igunga: Mnyika, Prof Safari kutua Igunga leo

mndeme

JF-Expert Member
Sep 2, 2008
323
57
Baada ya kurejea kutoka nchini Zambia alikokuwa mwangalizi wa kimataifa wa uchaguzi huo kupitia Jumuiya ya madola leo hii Mbunge wa Ubungo John Mnyika akiambatana na Mwanasheria na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CDM wanategemea kutinga Igunga mapema leo kwa ajili ya kuendeleza harakati za kulinyakua jimbo la Igunga.

Hakuna kulala mpaka kieleweke.
 
Baada ya kurejea kutoka nchini Zambia alikokuwa mwangalizi wa kimataifa wa uchaguzi huo kupitia Jumuiya ya madola leo hii Mbunge wa Ubungo John Mnyika akiambatana na Mwanasheria na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CDM wanategemea kutinga Igunga mapema leo kwa ajili ya kuendeleza harakati za kulinyakua jimbo la Igunga.

Hakuna kulala mpaka kieleweke.

Hizi siku nne zilizobaki kufikia siku ya uchaguzi tutashuhudia kampeni ambazo hatujawahi kuzishuhudia mahalim popote katika historia ya nchi hii.

Bila shaka baada ya uchaguzi huu wa igunga watu watakuwa nyaka nyaka!! Kila la kheri wapiganaji.
 
Prof kawape somo juu ya madai ya Uislam najua unajua kujenga hoja na kamalize issue kabisa .Mnyika kawaeleze jinsi Zambia ilivyo fanya maajabu a vyombo vya dola kubakia kulinda usalama na si kuigilia siasa .
 
Mungu awatangulie jamni, nchi hii inatakiwa mbadiliko makubwa sana. Natamni kama watu wa Igunga wangeweza kuelewa, hawa CCM hawana msaada yaani baada ya uchaguzi hawatawaikia tena
 
Makamanda tunawategemea kwa ukombozi wa nchi yetu kwani ccm walidhani haima mbadala wake
 
Wanaigunga inabidi watambue Baada ya Uchaguzi kama magamba watashinda basi Bajeti yao ya mwaka Mzima itakuwa wameshatumia katika kupewa fulana za bure, wasitegemee maendeleo Mengine
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom