Igunga: Mgombea ubunge wa TLP ajitoa

Mzito Kabwela

JF-Expert Member
Nov 28, 2009
18,857
7,615
WAKATI vuguvugu la siasa jimboni Igunga mkoani Tabora likiendelea kushika kasi, mgombea ubunge mteule wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), Dk. Moses Edward, amejitoa kuwania nafasi hiyo ya ubunge kupitia chama hicho.

Akizungumuza na waandishi wa habari jana katika ofisi za chama hicho jimboni humo alisema ameamua kujitoa kutokana na kukabiliwa na ukata huku zoezi hilo likihitaji nguvu kubwa.

Alisema hata makao makuu ya chama hicho yameshindwa kuonyesha msaada wowote hadi sasa huku mbio za kampeni zikitarajiwa kuanza hivi karibuni.

“Nimefikia maamuzi haya hasa baada ya makao makuu ya chama changu kushindwa kunipa msaada wowote huku kukiwa hakuna mwelekeo wa kuniunga mkono,” alisema.

Alisema alipitishwa na chama hicho bila kupingwa na kufanya idadi ya wagombea wanaowania nafasi hiyo kufikia wagombea saba.

Alitoa wito kwa wanachama wa chama hicho kuhakikisha wanaunga mkono chama watakachoona kinafaa kulingana na hoja za mchakato huo utakavyokwenda.

Mpaka sasa katika Jimbo la Igunga hali ya kisiasa inazidi kuchukua sura mpya, hasa mji huo kukusanya wanasiasa mbalimbali ambao wanahakikisha wanaibuka na ushindi.

Hadi sasa ni wagombea sita wamejitokeza na kuchukua fomu ya serikali ya kuwania ubunge kupitia vyama vyao.

Vyama hivyo ni CHADEMA inayowakilishwa na Joseph Mwandu, Chama cha Wananchi (CUF), Leopard Mahona, huku Chama cha Sauti (SAU), kikimteua John Maguma, Said Makeni (DP), Lazalo Ndegaya (UMD) na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kikiwakilishwa na Dk. Peter Kafumu.

source: http://freemedia.co.tz/daima/habari.php?id=34036

MY TAKE. Hivi vyama vya DP, UMD na SAU vinanipa maswali mengi kuliko majibu. Ni vyama shindani kweli au vya msimu?
 
vyama vya misimu ni matatizo ndio maana mrema wafuasi wake wanasema ajihuzuru ili wapatiakane vijana wenye akili mpya na endelevu ndani ya chama
 
MY TAKE. Hivi vyama vya DP, UMD na SAU vinanipa maswali mengi kuliko majibu. Ni vyama shindani kweli au vya msimu?
Vyama vingine vinashiriki ili kurushiwa makombo yatakayodondoshwa na baba lao magamba TLP imenusa hakuna makapi safari hii, hata mbwa anajua jalala lipi lina unafuu.
 
Nnawapongea TLP kwa kuona kuwa huko ni maji marefu yaliyowazidi kimo. Haya hao wana TLP wachache wapeni kura zenu CCM kwani magwanda si mmeshawaona siasa zao ni kufata na kuongelea watu badili ya kufata na kuo ngelea maendeleo.
 
WAKATI vuguvugu la siasa jimboni Igunga mkoani Tabora likiendelea kushika kasi, mgombea ubunge mteule wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), Dk. Moses Edward, amejitoa kuwania nafasi hiyo ya ubunge kupitia chama hicho.

Akizungumuza na waandishi wa habari jana katika ofisi za chama hicho jimboni humo alisema ameamua kujitoa kutokana na kukabiliwa na ukata huku zoezi hilo likihitaji nguvu kubwa.

Alisema hata makao makuu ya chama hicho yameshindwa kuonyesha msaada wowote hadi sasa huku mbio za kampeni zikitarajiwa kuanza hivi karibuni.

"Nimefikia maamuzi haya hasa baada ya makao makuu ya chama changu kushindwa kunipa msaada wowote huku kukiwa hakuna mwelekeo wa kuniunga mkono," alisema.

Alisema alipitishwa na chama hicho bila kupingwa na kufanya idadi ya wagombea wanaowania nafasi hiyo kufikia wagombea saba.

Alitoa wito kwa wanachama wa chama hicho kuhakikisha wanaunga mkono chama watakachoona kinafaa kulingana na hoja za mchakato huo utakavyokwenda.

Mpaka sasa katika Jimbo la Igunga hali ya kisiasa inazidi kuchukua sura mpya, hasa mji huo kukusanya wanasiasa mbalimbali ambao wanahakikisha wanaibuka na ushindi.

Hadi sasa ni wagombea sita wamejitokeza na kuchukua fomu ya serikali ya kuwania ubunge kupitia vyama vyao.

Vyama hivyo ni CHADEMA inayowakilishwa na Joseph Mwandu, Chama cha Wananchi (CUF), Leopard Mahona, huku Chama cha Sauti (SAU), kikimteua John Maguma, Said Makeni (DP), Lazalo Ndegaya (UMD) na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kikiwakilishwa na Dk. Peter Kafumu.

source: http://freemedia.co.tz/daima/habari.php?id=34036

MY TAKE. Hivi vyama vya DP, UMD na SAU vinanipa maswali mengi kuliko majibu. Ni vyama shindani kweli au vya msimu?

Mkuu hivyo vyama vimesimamishwa na CCM kwa mawazo kwamba watapunguza kura za CHADEMA, kumbe wanajidanganya. wagombea wa hivyo vyama hata hela ya gharama za kampeni hawana, wanalipiwa na magamba
 
Nnawapongea TLP kwa kuona kuwa huko ni maji marefu yaliyowazidi kimo. Haya hao wana TLP wachache wapeni kura zenu CCM kwani magwanda si mmeshawaona siasa zao ni kufata na kuongelea watu badili ya kufata na kuo ngelea maendeleo.

sijajua kama wewe ni bonge la mwanamke. juzi nimekuona vizuri
 
mazingaombwe yashaanza! naye alipojiingiza alikuwa anategemea msaada wa aina gani kwa mfano?
ff,angekua kajtoa wa chama mwenza hapo labda ila tlp sijui kama wanaunga mkono sana magamba. ila usiwe na wasiwasi, sera ya magamba ni kupindua daima (whatever..)
 
Nnawapongea TLP kwa kuona kuwa huko ni maji marefu yaliyowazidi kimo. Haya hao wana TLP wachache wapeni kura zenu CCM kwani magwanda si mmeshawaona siasa zao ni kufata na kuongelea watu badili ya kufata na kuo ngelea maendeleo.
Wachache wepi wakati alikuwa peke yake.
 
Mkuu hivyo vyama vimesimamishwa na CCM kwa mawazo kwamba watapunguza kura za CHADEMA, kumbe wanajidanganya. wagombea wa hivyo vyama hata hela ya gharama za kampeni hawana, wanalipiwa na magamba
<br />
<br />
Una ushahidi?? Thibitisha.
 
Nnawapongea TLP kwa kuona kuwa huko ni maji marefu yaliyowazidi kimo. Haya hao wana TLP wachache wapeni kura zenu CCM kwani magwanda si mmeshawaona siasa zao ni kufata na kuongelea watu badili ya kufata na kuo ngelea maendeleo.
Maendeleo yepi hayo Faiza Fox??????????Unaota nini au unaishi nchi gani??????
 
tujadili hoja ya msingi! hivi hicho chama hakina ruzuku, kuna haja ya kupitisha sheria ya kupunguza idadi ya vyama vya siasa maana vingine vipo kama havipo!
 
TLP INA MBUNGE 1 AGUSTINOR LYATONGER MREMER NAYE NI ZAID YA HASARA ACHILIA MBALI KUMPIGIA KURA NANI ATATHUBUTU HT KURUSHA MGUU KWNYE MKUTANO WA MGOMBEA WA TLP? mi nampongeza sbb amesoma alama za nyakati bd ccm.
 
Back
Top Bottom