Mzito Kabwela
JF-Expert Member
- Nov 28, 2009
- 18,857
- 7,615
WAKATI vuguvugu la siasa jimboni Igunga mkoani Tabora likiendelea kushika kasi, mgombea ubunge mteule wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), Dk. Moses Edward, amejitoa kuwania nafasi hiyo ya ubunge kupitia chama hicho.
Akizungumuza na waandishi wa habari jana katika ofisi za chama hicho jimboni humo alisema ameamua kujitoa kutokana na kukabiliwa na ukata huku zoezi hilo likihitaji nguvu kubwa.
Alisema hata makao makuu ya chama hicho yameshindwa kuonyesha msaada wowote hadi sasa huku mbio za kampeni zikitarajiwa kuanza hivi karibuni.
Nimefikia maamuzi haya hasa baada ya makao makuu ya chama changu kushindwa kunipa msaada wowote huku kukiwa hakuna mwelekeo wa kuniunga mkono, alisema.
Alisema alipitishwa na chama hicho bila kupingwa na kufanya idadi ya wagombea wanaowania nafasi hiyo kufikia wagombea saba.
Alitoa wito kwa wanachama wa chama hicho kuhakikisha wanaunga mkono chama watakachoona kinafaa kulingana na hoja za mchakato huo utakavyokwenda.
Mpaka sasa katika Jimbo la Igunga hali ya kisiasa inazidi kuchukua sura mpya, hasa mji huo kukusanya wanasiasa mbalimbali ambao wanahakikisha wanaibuka na ushindi.
Hadi sasa ni wagombea sita wamejitokeza na kuchukua fomu ya serikali ya kuwania ubunge kupitia vyama vyao.
Vyama hivyo ni CHADEMA inayowakilishwa na Joseph Mwandu, Chama cha Wananchi (CUF), Leopard Mahona, huku Chama cha Sauti (SAU), kikimteua John Maguma, Said Makeni (DP), Lazalo Ndegaya (UMD) na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kikiwakilishwa na Dk. Peter Kafumu.
source: http://freemedia.co.tz/daima/habari.php?id=34036
MY TAKE. Hivi vyama vya DP, UMD na SAU vinanipa maswali mengi kuliko majibu. Ni vyama shindani kweli au vya msimu?
Akizungumuza na waandishi wa habari jana katika ofisi za chama hicho jimboni humo alisema ameamua kujitoa kutokana na kukabiliwa na ukata huku zoezi hilo likihitaji nguvu kubwa.
Alisema hata makao makuu ya chama hicho yameshindwa kuonyesha msaada wowote hadi sasa huku mbio za kampeni zikitarajiwa kuanza hivi karibuni.
Nimefikia maamuzi haya hasa baada ya makao makuu ya chama changu kushindwa kunipa msaada wowote huku kukiwa hakuna mwelekeo wa kuniunga mkono, alisema.
Alisema alipitishwa na chama hicho bila kupingwa na kufanya idadi ya wagombea wanaowania nafasi hiyo kufikia wagombea saba.
Alitoa wito kwa wanachama wa chama hicho kuhakikisha wanaunga mkono chama watakachoona kinafaa kulingana na hoja za mchakato huo utakavyokwenda.
Mpaka sasa katika Jimbo la Igunga hali ya kisiasa inazidi kuchukua sura mpya, hasa mji huo kukusanya wanasiasa mbalimbali ambao wanahakikisha wanaibuka na ushindi.
Hadi sasa ni wagombea sita wamejitokeza na kuchukua fomu ya serikali ya kuwania ubunge kupitia vyama vyao.
Vyama hivyo ni CHADEMA inayowakilishwa na Joseph Mwandu, Chama cha Wananchi (CUF), Leopard Mahona, huku Chama cha Sauti (SAU), kikimteua John Maguma, Said Makeni (DP), Lazalo Ndegaya (UMD) na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kikiwakilishwa na Dk. Peter Kafumu.
source: http://freemedia.co.tz/daima/habari.php?id=34036
MY TAKE. Hivi vyama vya DP, UMD na SAU vinanipa maswali mengi kuliko majibu. Ni vyama shindani kweli au vya msimu?