Igunga: Jinsi wakala wa CHADEMA alivyouliwa...

Gharama ya mabadiliko ya kidemokrasia na mendeleo ya kweli hugharamikiwa na Damu..Mungu ibariki Tanzania

Ujumbe wangu kwa vijana wa Tanzania ni kuwa njia pekee ya nzuri ya kubadilisha serikali yeyote ni njia ya kura na kama njia hiyo ikizibwa au kuwa
rigged na wahusika basi wahusika wanakuwa wamewapa option moja tu nayo ni Revolution tu otherwise it will be wasting of time.
 
Napendekezachadema isimame kidete haya matukio mawili ya hujuma za tume ya uchaguzi pamoja na mauwaji ya kijana yachunguzwe na tume huru tupewe majibu . Watanzania tunataka kupata ukweli
 
Nimeisoma mpaka nikajisikia kutetemeka
Hivi kweli hawa waunngwana wana CCM wana hata chembe ya hofu ya Mungu
Kweli Kafumu anaweza kusimama mbele ya hadhara ya waumini wenzie akimshukuru Mungu ati kashinda ubunge kwa staili hii. Natamani kama Nape angenipa mwongozo katika hili. Jamani mimi nimeogopa na nitawachukia daima wana-CCM wote ndani na nje ya nchi maana tabia zao ni afadhali za yule joka wa zamani. Huu utawala wa kafara hautatufikisha mahali palipo salama hata kidogo
 
Hiyo Tindikali nadhani ni ile ambayo Magamba wameibakisha baada ya Kumwagia Kubenea na yule wakala wao kule Igunga.

Mimi nadhani sasa Magamba wanatamani kichapo. tumewavumilia sana kwenye maufisadi wanayotufanyia vya kutosha lakini naona sasa wanataka kutuingizia kidole machoni. Hizi ndo zinaitwa chokochoko kule kwetu visiwani. Magamba wameshindwa siasa sasa wanataka kuanzisha vurugu ili wavunje demokrasia. Waache waendelee nadhani wao wanahic wataishi milele.
 
kama maelezo haya ni ya kweli yapelekwe mahakamani sheria ichukue mkondo wake kwani trunakoelekea?
Taarifa rasmi inaeleza kuwa Marehemu Mbwana Masoud, aliekuwa Wakala wa CDM kutokea Ubungo DSM, alipotea tar 2/10/2011, siku ya uchaguzi, lakini ukweli ni kuwa siku hiyo ndiyo ilipogundulika kuwa amepotea baada kuhitajika kupelekwa kituoni kwake na kukosekana.

Hali halisi ni kuwa Mbwana Masoud usiku wa tar 1/10/2011 (Mkesha wa kuamkia siku ya uchaguzi) baada ya kula chakula cha jioni alitoka kunyoosha miguu, ingawa palitolewa Hali ya tahadhari lakini hali ilionekana iko shwari. Kumbe kulikuwa na kundi la mabaunsa wanne wa CCM wakimfuatilia, na inaelekea walikuwa wakiwasiliana kwa simu na gari lao, kwani mara walipomvamia, tena mbele za watu, gari hilo aina ya L/Cruiser Hardtop jeupe lenye namba T***ARD, mali ya CCM, Mara nyingi katika kipindi cha kampeni hizi lilikuwa likitoka usiku na mchana huwa linapaki, dereva wake ni yule alieshiriki kuwapiga mabapa ya mapanga wana CDM waliokuwa wakidai matokeo ya uchaguzi yatangazwe.

Ingawa Mbwana alijitahidi kujitetea asichukuliwe lakini alizidiwa nguvu, alijaribu kupiga kelele kuomba msaada lakini alipigwa kabari ya nguvu, kabla ya watu waliokuwa karibu hawajajua la kufanya (kwani tukio lenyewe lilifanywa kwa kasi, pia walijifanya kama ni watu wanaofahamiana ila wana mzozo fulani) walimtia kwenye gari Hilo na kuondoka nae kwa kasi kuelekea upande wa Mwanzugi.

Mafedhuli hao wa CCM, Mateso waliyomtesa Mbwana Masoud kabla ya kumtoa roho ni Mungu na wao wenyewe ndio wanajua, lakini kwa jinsi hali ya maiti yake ilivyokutwa baada ya kutupwa kwenye vichaka karibu na Magereza siku ya tar 9/10/2011 inaonesha dhahiri unyama aliofanyiwa hata huko Somalia walikozoea kuuana hakuna unyama wa aina hii.

Alikutwa na suruali tupu bila shati, SHINGO YAKE ILIKUWA IMEVUNJWA KWA NGUVU, MACHO YAKE YAMETOBOLEWA NA HAYAONEKANI, KICHWA CHAKE KIMEPASULIWA KWA NYUMA CHINI YA KISOGO, KIFUA CHAKE KIMEBABUKA KAMA VILE AMEMWAGIWA AINA FULANI YA TINDIKALI, mwili wake unaonesha alipigwa sana kabla kuuawa kinyama.

Kilichotushangaza ni kuwa mwili huo uliotupwa hapo unaonesha dhahiri hakuuliwa siku hiyo ya tar 9/10, lakini haukuwa umevimba Kama kawaida bali ulikuwa unaonesha dhahiri kuwa ulitiwa dawa ya kuhifadhia maiti, kwa vyovyote vile wauaji wake hawakuwa majambazi wa kawaida wa mtaani ambao huua na kuishia zao, bali ameuliwa na Organization kamili yenye motive ya kuua wakala wa CDM, ikumbukwe kwamba Serkali ya CCM awali ilitangaza kukataza mawakala kutoka nje ya jimbo, baada Wakili Tundu Lissu kwenda kumfundisha sheria Msimamizi wa Uchaguzi Igunga, ndipo wakaruhusiwa kwa shingo upande, lakini njiani walisumbuliwa sana na maaskari kwa maelekezo ya wakubwa w CCM.

Alitekwa ili kuwatisha mawakala wengine waogope kuwajibika, uongozi wa CDM ulitumia busara kutopiga kelele na badala yake kwenda kutoa taarifa Polisi kimyakimya, ingawa Polisi yenyewe haikuchukua hatua yoyote ya msako, mawakala wa CDM waliwajibika vilivyo vituoni na hakuna kura iliyoibiwa, ikabidi Serkali iisaidie CCM ishinde kwa nguvu kwa kuwazuia maelfu ya Vijana waliofika vituoni kupiga kura ingawa walipoteza shahada zao, kwa kujaza form No 17, mwanzo waliwaruhusu kupiga kura Kama sheria inavyotaka, lakini walipoona wanazidi kuwa wengi, ilipofika saa 4 asubuhi Mkurugenzi aliagiza wasiruhusiwe kupiga kura, wakafukuzwa, wengine hawakukuta majina yao kwenye daftari, wengine walikataliwa kupiga kura kwa kuwa waliorodheshwa kuwa wamekufa! Just imagine unaenda kituoni na shahada yako kupiga kura unazuiwa usipige kwa sababu wewe umeshakufa!

Haya; pamoja na kutumia vibaya mahindi ya msaada kama rushwa siku moja kabla uchaguzi, na kampeni potofu siku ya uchaguzi kuwa mgombea wa CDM amejitoa kwa hiyo haina haja kumpigia kura, ndiyo yalichangia ushindi kiduchu wa CCM.

Nirudi kwenye mada ya msingi ya mauaji, nisameheni najichanganya kwani Nina machungu mengi, Maiti ya Mbwana Masoud ilipookotwa, ilikutwa na kipande cha karatasi ambacho wauaji walitaka iaminike kuwa marehemu aliiandika baada ya kuuawa akitaja majina ya waliomuua, Polisi waliipuuza karatasi hiyo ingawa bado wanaishikilia, inazidi tu kuthibitisha kuwa wauaji wamejaribi kuficha kitendo chao na hivyo kukamilisha misingi ya First Degree Murder!

CCM Arusha iliua kwa kutumia Polisi wa serkali yake, lakini Igunga CCM imeua kwa kutumia Mungiki wake iliowalipa na kutumia gari lake, gharama zitokanazo na kodi zetu, Masoud akiwemo.

Salaam kwenu enyi Wauaji CCM, mnahubiri Amani na Utulivu majukwaani lakini Mikono yenu imetapakaa Damu ya wasio na Hatia, hakuna waliofanya hivyo wakafanikiwa mafanikio ya kudumu, mmepata Spasmodic Victory lakini Hakika mtaSuffer Eternal, Shameful Defeat!

Enyi wauaji CCM, Salaam kwenu kutoka kwa maelfu ya vijana wa Igunga waliodhulumiwa haki Yao ya kupiga kura kwa makusudi, Tunawaambia, Sukilizeni Vizuri enyi Mafedhuli, Haki itatendeka Igunga, however long it might take, lakini HAKI LAZIMA ITATENDEKA TU!

Tunajua hamuamini Mungu Enyi Wauaji na Wazinzi wa Wake za Watu, lakini Mungu alishasema " HAKI IKIDHIHIRI, BATILI HUJITENGA, HAKIKA BATILI NDIO HUJITENGA!" Kama mnajidai hamumuamini wala kumuogopa Mungu basi Hakika Mtakumbana na Nguvu za Umma ambazo ni Kubwa kuliko nguvu za Dola!

Umma wa Igunga una Hasira na Nyie Mafedhuli wakubwa, mnajua, Mbona hamkusherehekea vilivyo ushindi wenu hapa Igunga? Mlilipua fastafasta mkaenda kusherehekea Singida na Dar ambako mlifanya sherehe kubwa na maandamano ya kumpokea Mbunge wenu wa huko mliekuja kumtengenezea Igunga.
 
jamani jamani! hv hii damu inapotea hv hv ?kumbuka hawa jamaa walituahid kuwa watafanya kitu na wamefanya na yatakayotokea tusilalamike !, sasa yametokea je tuendelee kulalamika? hatuwezi kufanya kitu? hatuweki historia yeyote kwa hawa waliotuahid kutufanyia mbaya?kumbuka kijana mmoja tu wa tunisia ukombozi ukapatikana sembuse aliyeuliwa
 
Kama kuna kiongozi yeyote wa ngazi za juu wa CHADEMA naomba atusaidie yafuatayo
1.watoe taarifa juu ya kile kilichotokea Igunga,maana ukimya huu naona unajitokeza kwa mara ya pili maana baada ya uchaguzi mkuu chadema walificha ukweli fulani juu ya madudu ya serikali iliyoyafanya wakati wa uchaguzi ili jeyikei ashinde,sasa kwa jambo zito kama hili kulikalia kimya mimi roho inaniuma sana
2.pili wanachadema tuko tayari kuchanga ili mtuletee wapelelezi waliobobea kuchunguza jambo hili na ukweli uwekwe wazi
3.Naamini wana Igunga na wananchi wapenda haki na wanachama wa chadema na wapenda maendeleo watakuwa tayari kuunga mkono kutafuta njia ya kuwashughulikia hawa wauuaji,na iingefaa hiki ki Nape kituambie alikuwa na maana gani kutoa yale matamko.
bwana hii hali naona tulianzishe tu,hivi kumbe CCM wamezmua kufanya unyama huo?je wanadhani wakitushinda kwa kutumia dola na hao majambazi wao kujilipua nako tutashindwa?hivi kweli yamekuwa hayo,sawa Mungu haja lala,tumuombee marehe Masoud
 
Cnt believe ths,chama cha mafedhuli,chama cha mafisadi na chama cha murders?ur days are coming
 
chama cha majambazi(ccm)ww unategemea nn?hapa ni kuingia kitaa tu tufe wote tuone wataongoza mawe?
 
Masoud angezikwa kwa taratibu za CDM, mkutano mkubwa wa kumuaga na maandamano ya ukombozi! Mungu mrehemu Msoud aliyekufa kwa kutetea nchi yake, amina!
 
Kwa Tz lolote lawezekana manake jana nilisoma habari ya mauaji pale magomeni wiki jana. Raia mwema alimfuata mtu aliyeamini ndiye muuaji na alienda mpaka polisi magomeni lakini wakampuuza kuwa hawana gari.

Raia mwema alikodi pikipiki na kufuatilia daladala aliyopanda na baadaye akamwona muuaji akiongea na waliomtuma na kumlipa ujira wake. Alafu kamanda wa polisi anaulizwa nasema lazima watawasaka na kuwakamata wauaji.

Hiyo ndiyo TZ bana. Mungu awarehemu wote waliopoteza maisha!
 
Back
Top Bottom