Igunga: $100 kwa Nape. tik tak tok....

Afisa wa juu wa chama cha siasa chenye serikali anafanya kazi hiyo kama hobby???
huyu jamaa hana akili kabisa.
Anafanya nini nje ya hiyo hobby ya ukatibu itikadi na uenezi??
Au kimjini mjini, halafu siasa za ccm ndo hobby??!!
 
hahahahahahaha! majibu ya nape kama ya wale wachekeshaji wa FUTUHI! dah! Nyambala hela yako imebaki salama, nape hairambi ng'o, zaidi atasema hapelekwi igunga kwa hela za Nyambala, ndo utakuwa utetezi wake huu.[/QUOTE

Bado siku moja mkuu, ngoja tusubiri maana aliahidi bila kushurutishwa.
 
Kwa wana JF kwanza hongereni kwa kumrekebisha huyo mzee wa "Hobby".

@ KWAME ,KAKA AHSANTE KWA MANENO YAKO YA BUSARA SANA.


HEBU TUANGALIE MAANA HALISI YA NENO HOBBY

HOBBY=an activity engaged in for pleasure and relaxation during spare time

Kwa kweli Bora amesema mwenyewe kuwa siasa ni Hobby kwani HAYUKO KWA AJILI YA KUJITOLEA KWA WANANCHI NA KUCHUKULIA SIASA NI WITO NA KUJITOLEA KUSAIDIA NCHI NA HASWA WANANCHI WENYE KIU YA MAENDELEO TOKA KUJULIKANA KWA TAIFA HILI.

AENDE AKAFANYE KAZI ZAKE SIASA AWAACHIE WATU WENYE SIFA STAHILI.

LONGLIVE JF ,LONGLIVE JF,LONGLIVE JF
 

Kwa hiyo basi kama nilivyoahidi na kumthibitisha kwamba nilikuwa na nipo serious na ahadi yangu namtumia invisible hela hiyo in few hours tyme. Ikiwa Nape hatakwenda basi tutaipeleka hiyo hela kwenye charity yeyote of our choosing!!!!!!!!!!!
Mkuu nyambala angalia asije kukupiga chenga ya mwili akadai hakwenda makusudi ili pesa uliyotoa ikasaidie hizo charity org...si unawajua magamba.
 
Jamani,msisumbue akili kutafakari juu ya huyu jamaa.CCM lao ni moja,wanafanana.Huwezi kua kwao na una msimamo tofauti na ukaendelea kubaki.Ni wanafki,wanajua kuigiza.Nape mmoja wao,ni walewale.Juzi juz facebuk kakoment juu ya Picha ya Dr na JK eti kwamba "Unafiki mwingine bwana...." watu wakamponda sana akabadilisha na kuandika "Hapa mnacheka,nje mnamwagiana tindikali" nape ni mnafiki.Kasema Magamba 3 watafukuzwa in 90 days,saivi cjui siku ya 130.Porojo tu.

Ukweli ni kwamba CCM inatamani kubadilika na ipate mvuto lakini haiwezi tena.Tatizo kubwa ni JK Mwenyewe,uwezo ndo tatizo kwake
 
Hivi katibu mweneze, si ndio msemaji wa chama, na anatakiwa awe ndio mpiga kampeni mkuu! huyu kijana vipi? hata Makamba J, yupo igunga huyu Nape vipi?
 
Mkuu can we make this local pls? I mean just for this bet! Siku hazikwisha bado kuna kesho, Nape ni member humu nadhani hahitaji kusemewa bali he can come out himself as he has alwayz been!!!!!!!
Nyambala,
Chunguza posts za Nape zinavyopokelewa humu. Zilinganishe na zile za Dr Slaa au Zitto na mapokeo yake. Simsemei Nape na najua asingependa hata kukutana nami. Namfahamu kidogo sana kwa visiku hivi vichache alivyojitokeza kwenye siasa. Jina na haiba ya baba vimechangia kumtambua haraka ndani ya CCM. Tujaribu kumpa nafasi na heshima kidogo angalau. Ni nini cha mno IGUNGA? Ni lazima kila mtu aende?
 
Nyambala,
Chunguza posts za Nape zinavyopokelewa humu. Zilinganishe na zile za Dr Slaa au Zitto na mapokeo yake. Simsemei Nape na najua asingependa hata kukutana nami. Namfahamu kidogo sana kwa visiku hivi vichache alivyojitokeza kwenye siasa. Jina na haiba ya baba vimechangia kumtambua haraka ndani ya CCM. Tujaribu kumpa nafasi na heshima kidogo angalau. Ni nini cha mno IGUNGA? Ni lazima kila mtu aende?

si kila mtu lazima aende Igunga, lakini sio kwa KAtibu mwenezi wa Chama (Ambaye ndio msemaji wa chama)
Hii ni picha dhairi kuwa bila ufahamu wowote NApe ameingizwa kwenye siasa uchwara za CCM bila yeye kujijua, siasa alizoambiwa hazihubiri hazifai Igunga na wala yeye hatakiwi Igiunga
kwa kifupi hawezi kwenda Igunga
 
Nyambala,
Chunguza posts za Nape zinavyopokelewa humu. Zilinganishe na zile za Dr Slaa au Zitto na mapokeo yake. Simsemei Nape na najua asingependa hata kukutana nami. Namfahamu kidogo sana kwa visiku hivi vichache alivyojitokeza kwenye siasa. Jina na haiba ya baba vimechangia kumtambua haraka ndani ya CCM. Tujaribu kumpa nafasi na heshima kidogo angalau. Ni nini cha mno IGUNGA? Ni lazima kila mtu aende?

WildCard
hapo kwene red ni kua Igunga kuna uchaguzi wa ubunge wenye mchuano mkali ambapo Nape ni muhimu kushiriki japo si lazima. kufuatia makala ya Mwanahalisi kwa madai ya Wilson mkama ni kwamba hawamtaki Nape Igunga maana atawaharibia uchaguzi. Nape alikanusha na akasema mwenyewe kua wiki hii ataenda igunga ndipo Nyambala akabet $100. kama uko makini utagundua kua Nape anaangamizwa kisiasa na labda anajua ama hataki kujua au anajinyima kuona hilo. Jana awe championi wa kujivua gamba na leo anyimwe kwenda kupiga kampeni na chama chake. kwa mantiki hiyo wale walioitwa magamba leo ni bora kuliko Nape. maana nyingine ugonjwa ni bora kuliko tiba????
 
si kila mtu lazima aende Igunga, lakini sio kwa KAtibu mwenezi wa Chama (Ambaye ndio msemaji wa chama)
Hii ni picha dhairi kuwa bila ufahamu wowote NApe ameingizwa kwenye siasa uchwara za CCM bila yeye kujijua, siasa alizoambiwa hazihubiri hazifai Igunga na wala yeye hatakiwi Igiunga
kwa kifupi hawezi kwenda Igunga
CCM wamekwenda wengi mno Igunga. Kwa nini mnataka Nape aende ambaye mnajua kabisa ametusaidia kumwondoa RA kwenye nafasi hiyo? Mchango wake huo hamuuthamini? Naibu Katibu Mkuu wa CCM bara naye sijamsikia huko. Mbona yeye hamuulizi?
 
hii inatusaidia kujua ni kwa nini sisi ni maskini. Mtu kama huyu akisema amerithi elimu sio kweli na ina maana elimu yake ni VOID, au basi hiyo elimu ni ile ya '1+1=11' ambapo kama una hata vitabu vyenye theories kama hizi kwenye shelf zako inabidi uvitoe na kuvichoma moto
Afisa wa juu wa chama cha siasa chenye serikali anafanya kazi hiyo kama hobby???
huyu jamaa hana akili kabisa.
Anafanya nini nje ya hiyo hobby ya ukatibu itikadi na uenezi??
Au kimjini mjini, halafu siasa za ccm ndo hobby??!!
 
Hata ungemwahidi $10000! hataenda labda aende usiku nakurudi tena avae baibui,la sivyo Kina Mukama watamshughulikia fasta,hiyo pesa invicible jiandae tu kuipeleka kwenye any charity Nape kabaki kama Zombe anaetishia kujinyonga CHADEMA ikishika dola.
 
Nyambala,
Chunguza posts za Nape zinavyopokelewa humu. Zilinganishe na zile za Dr Slaa au Zitto na mapokeo yake. Simsemei Nape na najua asingependa hata kukutana nami. Namfahamu kidogo sana kwa visiku hivi vichache alivyojitokeza kwenye siasa. Jina na haiba ya baba vimechangia kumtambua haraka ndani ya CCM. Tujaribu kumpa nafasi na heshima kidogo angalau. Ni nini cha mno IGUNGA? Ni lazima kila mtu aende?

Si lazima kila mtu aende you are right! Lakini ni yeye mwenyewe aliahidi baada ya watu kusoma kwenye vyombo vya habari kwamba amekatazwa kwenda huko. Infact mimi sina bifu naye na sina sababu ya kufanya hivyo lakini nachojaribu kukifanya ni kuweka wazi jinsi gani watu kama Nape wanaendelea ku-hoodwink watanzania kwamba wako pamoja nao wakati hawawezi kustand on principles! Ni hilo tu, mfano baada ya kutolewa hii allegation kwamba amekatazwa kwenda Igunga angekaa kimya nisingekuwa na sababu ya kubet.

Lakini unapomuona ameenda huko Igunga kwa kujificha ficha halafu baadae natamba humu JF na Facebook kwamaba amethubutu, ameweza na amesonga mbele ni ushahidi tosha kwamba ni kweli alikatazwa! Sasa inakuwaje kwa cheo chake asionekane kwenye mkutano hata mmoja? Hiki cheo hakuanza nacho yeye, waliomtangulia siku zote tumewaona kwenye hizi kampeni. Mbaya zaidi amewahi kuisingizia JF indirectly kwamba inatumiwa na mafisadi alio nao huko huko CCM kuhujumu majukumu yake!
 
Walio karibu nae wanasema atakwenda siku ya kufunga kampeni. Mjue tu kwamba Igunga wanadhani yeye na Chiligati ndio waliomkomalia mbunge wao kipenzi RA. Busara za kawaida tu zinahitajika kuisoma hali hii. Naamini Nape hajabadili msimamo wake juu ya mafisadi kwa kuwa wao hawatamsamehe milele.
 
Tunampa nafasi Nape atoe maoni yake kama tunavyofanya kwa viongozi wengine wa kisiasa walio ma-member humu kama Dr Slaa, Zitto, Mnyika,...., au ni kumshambulia kila anapoonyesha pua yake humu. Ninachokiamini kwa huyu kijana ni kuwa anapambana na mambo mazito sana ndani ya CCM. Kila akijaribu kutoka apate maoni na michango yenu mnamtoa mkuku humu. Mnamhesabia dhambi zooote za CCM hata zilizotendeka kabla hajazaliwa! Tutake tusitake CCM tunayo kwa kipindi kirefu tu kijacho hadi itakapopasuka na kumpata Sata wetu.

Labda kama anatumia Ids nyingi ambazo hatuzijui, lakini kama anaingia kwa Id yake tunayoifahamu ya Nnauye Jr. huwa anapata nafasi ya kutosha kujibu hoja hapa JF.

Tatizo tunaloliona kwa nape ni kwamba hana uvumilivu kama walivyo wengtine kama Dr.Slaa, Mnyika na Zitto ambao hawapati shida sana kuja kwenye forum kushiriki mijadala na wadau. Hata pale wanaposhambuliwa bado hawaachi kuingia JF.

Sasa Nape amefikia hatua ya kubadilisha muda wa kuingia JF, anaonekana mara nyingi anaingia JF usiku wa manane anachagua topic ya kuchangia na bahati mbaya hachangii mambo ya maana yanayoendana na wadhifa wake. Anaweka taarabu tu na kuondoka. Majigambo ndiyo usisema.

Kwahiyo hakuna mtu anayemshambulia nape ama kumchukia, isipokuwa yeye mwenyewe ndio anajisababishia maisha magumu hapa JF. Akifahamu ukubwa wa nafasi yake ndani ya chamam chake atajitahidi kuwa na majibu ya kueleweka na ataacha kuropokka na kuimba taarabu.
 
Walio karibu nae wanasema atakwenda siku ya kufunga kampeni. Mjue tu kwamba Igunga wanadhani yeye na Chiligati ndio waliomkamalia mbunge wao kipenzi RA. Busara za kawaida tu zinahitajika kuisoma hali hii. Naamini Nape hajabadili msimamo wake juu ya mafisadi kwa kuwa wao hawatamsamehe milele.

Sio kwamba wanadhani, siku gamba kuu linajivua ubunge na uNEC lilibainisha waziwazi kwamba nape na chiligati ndio wamesababisha ajivue gamba kwa sababu ya gutter politics.

Hata kama nape hajabadili msimamo wake dhidi ya mafisadi bado atalazimika kukubali yaishe kwakuwa anaonekana vita anayoipigana hana support ya kutosha.
 
Sio kwamba wanadhani, siku gamba kuu linajivua ubunge na uNEC lilibainisha waziwazi kwamba nape na chiligati ndio wamesababisha ajivue gamba kwa sababu ya gutter politics.

Hata kama nape hajabadili msimamo wake dhidi ya mafisadi bado atalazimika kukubali yaishe kwakuwa anaonekana vita anayoipigana hana support ya kutosha.
Kama tunaelewa hivyo, kumshinikiza aende mnatafuta cha kuandika humu akizomewa au kurushiwa mawe? Labda niulize kama alivyouliza Mwanakijiji. Mbona CHADEMA hawamtaji RA kuwa alikuwa fisadi na kwamba ufisadi wake ndio umesababisha kadhia yote hii ya uchaguzi mdogo? Au Dr Slaa anakuwa na nguvu hizo akiwa MwembeYanga tu?!
 
Sasa kama wewe umeachiwa urithi wa elimu, na unadai siasa unafanya kama hobby; dah unanichanganya...hiyo ni elimu gani ulorithishwa wewe ambayo inakuruhusu kufanya siasa za nchi kama hobby?

sasa naeza kuona kwa nini mtu alikuita "Nje Cup"

Nilishawaambia wakuu jamani, huyu jamaa hana kitu kichwani, hafai hata kuwa class rep, ni mweupe mno kichwani.
 
Tunampa nafasi Nape atoe maoni yake kama tunavyofanya kwa viongozi wengine wa kisiasa walio ma-member humu kama Dr Slaa, Zitto, Mnyika,...., au ni kumshambulia kila anapoonyesha pua yake humu. Ninachokiamini kwa huyu kijana ni kuwa anapambana na mambo mazito sana ndani ya CCM. Kila akijaribu kutoka apate maoni na michango yenu mnamtoa mkuku humu. Mnamhesabia dhambi zooote za CCM hata zilizotendeka kabla hajazaliwa! Tutake tusitake CCM tunayo kwa kipindi kirefu tu kijacho hadi itakapopasuka na kumpata Sata wetu.
Kunwa wakati unaeleweka, kuna wakati ambao ninaamini hata wewe mwenyewe unakuwa hujielewi.
BOLD: kwani hawa wanapewa nafasi ya kujieleza? si wajajieleza wenyewe kama viongozi. Nape huwa anaingia humu badala ya kutoa maelezo kama kiongozi, yeye anapayuka na kuropoka mipasho yake isoyo na mbele wala nyuma.
Sasa ameambiwa eleza, kwa nini huendi Igunga? kuna taarifa kwamba umepigwa stop, yeye badala ya kuja hapa kama kijana na kiongozi mwenye cheo kikubwa kwenye chama chake, anaingia kama vile anakuja ''kumsuta'' mtu. Ridiculous!!!

RED: Naona unamsemea sasa, hajawahi kusema kama kiongozi kijana anapambana na mambo mazito, anachosema ni kwamba wamejipanga kama chama kuwavua baadhi ya wanachama wao magamba.....hajawahi kuingia humu kutaka kupata mawazo ya vijana.
Nape alikuwa anaingia humu zamani kama kijana shupavu, anatoa hoja nzito, anakosoa, anakosolewa na maisha yanaenda mbele, sasa hivi hata huko face book ni kejeli tupu. Unampa vipi mtu wa namna hiyo mawazo??

BLUE: hapa unatulazimisha tukubaliane na mawazo yako, ambayo ndio haswa huwa nayashangaa sana.
 
9 Reactions
Reply
Back
Top Bottom