Chikaka Sumuni
JF-Expert Member
- May 16, 2013
- 1,337
- 770
Mkuu wa Jeshi la polisi IGP Saidi Mwema amesema kwamba Jeshi la polisi litamhoji Naibu katibu mkuu wa CCM MWIGULU MCHEMBA, juu ya kauli yake alioitoa Katika kata ya Kimandolu wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani jijini Arusha.
Katika mkutano huo Mwigulu aliwaambia Wananchi waliokua wakimsikiliza kuwa wasipoichagua CCM watakufa.na baada ya siku moja tangia atoe kauli hiyo kweli watu waliuwawa kwa bomu.
IGP Mwema pia alilaani tukio hilo na kusema kwamba wote wenye taarifa na watu waliohusika na tukio hilo wamtumie ujumbe kwa simu no 0754785557 na majina yao yatafichwa.
Kinachonishangaza ni kuwa hadi sasa walio nyuma ya tukio hili la Kurusha Bomu katika Mkutano wa CHADEMA wanajulikana kuwa waliratibiwa na MWIGULU. Sio hivyo tu hata majeruhi wengi wa tukio lile hawakujeruhiwa na Bomu bali na Risasi zilizokua zikirushwa na Jeshi la polisi.
Ushauri wangu kwa IGP MWEMA, aweke kwanza pembeni swala la Siasa na afanye kazi kwa mujibu wa sheria na katiba ya nchi. Mwigulu na wenzake wakamatwe kama wahalifu wengine wowote, na Askari polisi wote waliokua sehemu ile ilipotokea tukio lile pia wakamatwe. Baada ya hawa kukamatwa kwanza ndipo upelelezi ukishirikisha vyombo huru vya uchunguzi uanzie hapo.
Kama tungekuwa tunajuzwa kiini cha mahojiano tungeamini amini hivyo. Ila yawezekekana watu wakakaa kupiga gahawa ili kuwaridhisha watanzania. Dawa iundeni Tume huru ya Kijaji ambayo watu wote watahusika kama kweli hakuna janja janja. Mahojiano mema.