Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,339
- 51,880
Herehoa!
Kesi inayomkabili Sebaya vyovyote itakavyoisha, iwe Kwa kushinda Kwake au kushindwa kwake lakini imetoa funzo kubwa Kwa wenye mamlaka hasa Wale wanaopewa Amri na kuifuata.
Katika maelezo ya Sebaya, alisema kuwa mambo aliyokuwa anayafanya alikuwa akiagizwa na wakubwa wake. Hata hivyo utaratibu wa kazi za Serikalini unafahamika kuwa kazi yoyote ya kiofisi inapaswa iende Kwa maandishi.
Sasa Sebaya anakazi mbili, mosi kuthibitisha kuwa alikuwa akiagizwa na wakubwa wake, na pili, kujitetetea yeye Kama yeye mbali na HAO wakubwa waliomtuma.
IGP Siro baada ya kupokea Oda kutoka Kwa Waziri Gwajima kuwa wamtie nguvuni Askofu Gwajima ili ajibu na athibitishe madai yake. IGP Siro ameuona mtego huo, ndio maana akasema anasubiri Barua Rasmi itakayotoa maelekezo ya kumkamata huyo mtuhumiwa.
Hata hivyo maelezo ya IGP Siro sio tuu anahitaji Barua lakini ndani ya hiyo barua iwe na maelezo yanayojiyosheleza ya kumkamata Askofu Gwajima.
Hii inatuambia nini?
Hii inatoa funzo Kwa watu wengine kuwa, Mkubwa akikutuma hasa ishu za kikazi ni vizuri utaratibu ufuatwe, mambo ya kufanya kazi kienyeji huko mbeleni likitokea lakutokea unashangaa jumba bovu linakuangukia wewe pekeako.
Wanaosema, kuwa kwa nini IGP Siro Raundi hii kwenye sakata la Gwajima na Shemeji yake ndio kataka Barua Rasmi, na sio baadhi ya vipindi vilivyopita hasa kuwakamata wapinzani. Jibu kinaweza kuwa, kila siku watu wanajifunza. Kuna kujifunza Kwa njia rahisi na kujifunza Kwa njia ngumu.
Kuna kujifunza wewe mwenyewe na kujifunza kupitia wengine.
Wito: kila Mmoja afuate taratibu za kazi yake. Haki, upendo na sheria zifuatwe.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Morogoro
Kesi inayomkabili Sebaya vyovyote itakavyoisha, iwe Kwa kushinda Kwake au kushindwa kwake lakini imetoa funzo kubwa Kwa wenye mamlaka hasa Wale wanaopewa Amri na kuifuata.
Katika maelezo ya Sebaya, alisema kuwa mambo aliyokuwa anayafanya alikuwa akiagizwa na wakubwa wake. Hata hivyo utaratibu wa kazi za Serikalini unafahamika kuwa kazi yoyote ya kiofisi inapaswa iende Kwa maandishi.
Sasa Sebaya anakazi mbili, mosi kuthibitisha kuwa alikuwa akiagizwa na wakubwa wake, na pili, kujitetetea yeye Kama yeye mbali na HAO wakubwa waliomtuma.
IGP Siro baada ya kupokea Oda kutoka Kwa Waziri Gwajima kuwa wamtie nguvuni Askofu Gwajima ili ajibu na athibitishe madai yake. IGP Siro ameuona mtego huo, ndio maana akasema anasubiri Barua Rasmi itakayotoa maelekezo ya kumkamata huyo mtuhumiwa.
Hata hivyo maelezo ya IGP Siro sio tuu anahitaji Barua lakini ndani ya hiyo barua iwe na maelezo yanayojiyosheleza ya kumkamata Askofu Gwajima.
Hii inatuambia nini?
Hii inatoa funzo Kwa watu wengine kuwa, Mkubwa akikutuma hasa ishu za kikazi ni vizuri utaratibu ufuatwe, mambo ya kufanya kazi kienyeji huko mbeleni likitokea lakutokea unashangaa jumba bovu linakuangukia wewe pekeako.
Wanaosema, kuwa kwa nini IGP Siro Raundi hii kwenye sakata la Gwajima na Shemeji yake ndio kataka Barua Rasmi, na sio baadhi ya vipindi vilivyopita hasa kuwakamata wapinzani. Jibu kinaweza kuwa, kila siku watu wanajifunza. Kuna kujifunza Kwa njia rahisi na kujifunza Kwa njia ngumu.
Kuna kujifunza wewe mwenyewe na kujifunza kupitia wengine.
Wito: kila Mmoja afuate taratibu za kazi yake. Haki, upendo na sheria zifuatwe.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Morogoro