mshale21
JF-Expert Member
- Apr 8, 2021
- 2,050
- 4,904
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro, amewataka Askari wa Jeshi hilo kutimiza wajibu wao ili kuweza kukabiliana na matukio ya uhalifu na wahalifu pamoja na vitendo vingine vya uvunjifu wa amani vinavyojitokeza kwenye jamii.
IGP Sirro amesema hayo leo wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya medani za kivita katika kambi ya Kambapori iliyopo West Kilimanjaro, wilayani Siha ambapo Askari wa kozi ya cheo cha Mkaguzi Msaidizi wa Polisi ambayo mafunzo yake yanahitimishwa leo Oktoba 8, 2021.
"Wahalifu wanafanya kazi kama timu ili kuwashinda ni lazima tufanye kazi yetu kama timu, na mimi nimetimiza wajibu wangu, kilichobaki ninyi mtimize wajibu wenu, uwezo mnao, majambazi wanachukua silaha na kunyang'anya watanzania huwa nawaambia uwezo hawana, wangekuwa wanaona silaha na mafunzo mliyonayo wasingethubutu,”amesema IGP.
IGP Sirro amesema hayo leo wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya medani za kivita katika kambi ya Kambapori iliyopo West Kilimanjaro, wilayani Siha ambapo Askari wa kozi ya cheo cha Mkaguzi Msaidizi wa Polisi ambayo mafunzo yake yanahitimishwa leo Oktoba 8, 2021.
"Wahalifu wanafanya kazi kama timu ili kuwashinda ni lazima tufanye kazi yetu kama timu, na mimi nimetimiza wajibu wangu, kilichobaki ninyi mtimize wajibu wenu, uwezo mnao, majambazi wanachukua silaha na kunyang'anya watanzania huwa nawaambia uwezo hawana, wangekuwa wanaona silaha na mafunzo mliyonayo wasingethubutu,”amesema IGP.