Uchaguzi 2020 IGP Sirro: Kukaa na kulinda kura ni dalili ya kufanya vurugu, baada ya kupiga kura rudini nyumbani

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Simon Sirro amewataka Wananchi kujitokeza kwa wingi na kupiga kura kesho akiwashauri warudi nyumbani na kuendelea na shughuli zao.

Ameeleza kuwa, baadhi ya viongozi wamekuwa wakihamasisha wapiga kura walinde kura, kitendo ambacho amesema ni dalili ya kufanya fujo.

Amesema kwa mujibu wa Sheria zilizowekwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) wanaolinda kura ni Mawakala ambao kila Chama imepeleka.

Amesema, "Kuna Vyama vinajiona vimeshashindwa kwahiyo malengo na nia iliyopo ni kufanya fujo. Niwaombe sana Viongozi wa Siasa, wakati huu si wakati wa kufanya fujo"

Kuhusu Zanzibar, Sirro amesema karibu watu 42 wamekamatwa Pemba kwa madai ya kuwashambulia Polisi waliokuwa wakisambaza masanduku ya kura jana

Ameeleza kuwa, mpaka sasa hakuna taarifa ya vifo na hatarajii kuwe na vifo vyovyote, akisisitiza wasingependa Uchaguzi ambao unasababisha maisha ya watu kupotea

 
Wala hakuna haja ya kukaa kituoni kulinda Kura kwasababu vituo vya kura vipo kwenye makazi ya watu hata camera za nyumba za jirani zitalinda Kura hata Mimi kwangu natazama kituo Cha kupiga kura dirishani kila kitu kinachoendelea naangalizia dirishani kwangu yaani hii technology ni shida Sana.
 
Magufuli wako yupo kwenye taratibu za kuanza kuchunguzwa na ICC pamoja na kutolewa hati ya kukamatwa.
Tumeshasema kama mtaweza tuuweni tu wote, tulizaliwa siku moja na sote siku moja tutakufa. Kesho tunapiga kura na kuzilinda, full stop
Nimependa ufafanuzi..
Tuwashauri jamaa na ndugu zetu.. tupige kura turudi majumbani..

Magufuli anapeta na tano tena
 
Wala hakuna haja ya kukaa kituoni kulinda Kura kwasababu vituo vya kura vipo kwenye makazi ya watu hata camera za nyumba za jirani zitalinda Kura hata Mimi kwangu natazama kituo Cha kupiga kura dirishani kila kitu kinachoendelea naangalizia dirishani kwangu yaani hii technology ni shida Sana.
Utopia,
 
Hao polisi waliomwaga kila kona nchi hii kwanini wasingepewa kazi ya kuzuia hizo dalili kwenye hivyo vituo? wakae na hao wanaolinda kura halafu tuone kama patakuwa na vurugu.
 
Je, kama mkitii sheria bila shurti hamtapata kibali?. Watanzania sio wajinga wanajua wakumpa kura zao. Chama cha Mbowe kipo hoi bin taabani.
 
Back
Top Bottom