MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,011
- 16,748
Huwa kanakuwa njia panda ya Kawe pale Maringo na kuna muda huwa anakuwa njia panda ya Kawe pale Lugalo na wakati mwingine anakuwa Mbezi Beach Tangi Bovu.
Ni Trafiki ambaye mara kwa mara nimeona Watu wakimsifia kwa Kufanya Mbwembwe zake huku akiongoza Magari na nadhani huenda hili ndilo linamfanya hata akichukua Rushwa asijulikane na asijadiliwe Mitandaoni.
Leo kwa macho yangu mida ya 9 Kasorobo huyu Trafiki ila mwenye Mbwembwe jirani kabisa na ilipo Benki ya NBC Tangi Bovu akiwa anakagua Gari ya Dada Mmoja hivi iliyogongana na nyingine aliisimamisha Gari aina ya Canter ( Kenta ) iliyobeba Mbao kisha akawahi kwa Dereva na akapewa Tsh 5,000/= ambayo aliikunja Kiustadi na kuitumbukiza Mfukoni na kuendelea na Maisha.
Huku nikidhani kuwa huenda Tukio hilo la Kipumbavu na Kinyume na Maadili ya Kipolisi niliona peke yangu kumbe hata baadhi ya Madereva Bodaboda baadhi Jirani waliona na Kunishangaa huku wakisema kuwa Mimi ni Mgeni wa huyo Trafiki kwani Wao wameshamzoea na kwamba kwa Siku akikosakosa mno Pesa kuanzia Asubuhi hadi Jioni hakosi kati ya Tsh 50,0000/= hadi 75,000/=
Najua Maisha sasa ni Magumu hivyo kuna muda Mtu anaamua Kujiongeza kwa namna namna ila basi Staha itumike pamoja na Umakini.
Yaani kwa namna alivyoichukua ile Pesa ( Rushwa ) kiukweli imeonyesha kuwa haogopi, anajiamini na anaidharau ile Uniform yake na hata Jeshi la Polisi.
Mwisho IGP ikikupendeza kwa nia njema tu muonye huyu Kijana wako ( Trafiki ) aachane mno na tabia yake ya Kupenda tu Kutongoza hovyo Wanawake ambao huwa anasimamisha Gari zao ama Kuzikagua au kwa Makosa kweli ya barabarani.
Mdhibitini upesi sana asipende Rushwa.
Ni Trafiki ambaye mara kwa mara nimeona Watu wakimsifia kwa Kufanya Mbwembwe zake huku akiongoza Magari na nadhani huenda hili ndilo linamfanya hata akichukua Rushwa asijulikane na asijadiliwe Mitandaoni.
Leo kwa macho yangu mida ya 9 Kasorobo huyu Trafiki ila mwenye Mbwembwe jirani kabisa na ilipo Benki ya NBC Tangi Bovu akiwa anakagua Gari ya Dada Mmoja hivi iliyogongana na nyingine aliisimamisha Gari aina ya Canter ( Kenta ) iliyobeba Mbao kisha akawahi kwa Dereva na akapewa Tsh 5,000/= ambayo aliikunja Kiustadi na kuitumbukiza Mfukoni na kuendelea na Maisha.
Huku nikidhani kuwa huenda Tukio hilo la Kipumbavu na Kinyume na Maadili ya Kipolisi niliona peke yangu kumbe hata baadhi ya Madereva Bodaboda baadhi Jirani waliona na Kunishangaa huku wakisema kuwa Mimi ni Mgeni wa huyo Trafiki kwani Wao wameshamzoea na kwamba kwa Siku akikosakosa mno Pesa kuanzia Asubuhi hadi Jioni hakosi kati ya Tsh 50,0000/= hadi 75,000/=
Najua Maisha sasa ni Magumu hivyo kuna muda Mtu anaamua Kujiongeza kwa namna namna ila basi Staha itumike pamoja na Umakini.
Yaani kwa namna alivyoichukua ile Pesa ( Rushwa ) kiukweli imeonyesha kuwa haogopi, anajiamini na anaidharau ile Uniform yake na hata Jeshi la Polisi.
Mwisho IGP ikikupendeza kwa nia njema tu muonye huyu Kijana wako ( Trafiki ) aachane mno na tabia yake ya Kupenda tu Kutongoza hovyo Wanawake ambao huwa anasimamisha Gari zao ama Kuzikagua au kwa Makosa kweli ya barabarani.
Mdhibitini upesi sana asipende Rushwa.