IGP Sirro: Hatujafikia hatua ya kufunga mipaka ya nchi kutokana na ugonjwa wa Corona

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
4,572
26,868
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania (IGP) Simon Sirro amesema jeshi hilo limejipanga imara kwenye mipaka ili kuhakikisha kwamba watu wanaoingia nchini wanafuata utaratibu na endapo wakibainika kuwa na viashiria vya virusi vya Corona basi hatua zinachukuliwa kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa.

Akizungumza na ITV Online IGP Sirro amesema kwa sasa hakuna haja ya kufungwa kwa mipaka lakini kama kutakuwa na sababu ya moja kwa moja vyombo vya usalama vilivyopo katika mipaka vitashauri lakini kutokana na Intelijensia walizozipata hakuna tishio kubwa kiasi hicho mpaka kufikia kufungwa mipaka.

"Sasa elimu tumeshaipata kilichobaki ni sisi watanzania kutekeleza hiyo elimu ambayo tumeipata, manaake ukiipata hiyo elimu, usipoitumia hiyo elimu ukabaki kufanya mambo yako ya zamani mwisho wa siku utaangamiza jamii ya Watanzania" Alisema.


Credit: ITV
 
China chanzo korona, tangu 10 March wageni wote lazima wafikie guarantee in kwa siku 14! Viongozi wetu wapate uzoefu na kufanya maamuzi kwa wakati.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kitu hatari zaidi kufanya sasa ni kuendelea kukaa na kuomba Serikali ifunge mipaka.. Ni kupoteza muda wa kujiokoa mwenyewe...

Watu wanadhan suala la kutofunga mipaka tu ndio linatusumbua, mimi mpaka sasa kitendo cha Serikal kuweka Karantini nzila karibu na nyumbani kilinipa mawazo hatari...

Nikajiuliza visiwa tulivyonavyo vya kazi gani ?

We all know corona ni hatari kwa watu wenye precondition na nzila wapo kibao, why pale?

Kwann tuweke Karantini almost katikati ya mji?

Najua siwez pata majibu sahihi, ukizingatia suala la kufunga mipaka tu nongwa...

Je, niendelee kujiuliza maswali na kulalama kitu fulani hakijafanyika...?

Kweli Serikali naomba inisamehe kwa usumbufu wa kelele za kufunga mipaka... Yah unapotoa ushauri and nobody responds ni kelele...

Nimeamua kuachana na kutegemea Serikal na kuwa full responsible na afya yangu na ya ndugu zangu..

Nimeshapoteza muda inatosha, siwezi kuwa mjinga kuendelea kupoteza muda.

Nchi yenye square km 900,000+(Rwanda 36+), safe option ni kuendelea kulalama kwann serikal haijafunga mipaka tu..!! Tuamke tutengeneze mipaka yetu tujifungie.. Hii mipaka ya kufungwa na dona kantri haielewek.

Bad enough tuliambiwa ikiingia, we can't handle as a country... Ndio ishaingia.. handle it by yourself.
 
IGP Sirro:Hatujafikia hatua hiyo ya kufunga mipaka.https://www.youtube.com/watch?v=mIALkuGuD1E&feature=youtu.be
Umaskini ni mbaya sana hii yote ni kuzuga kupata pesa za watalii (ambao ki uhalisia wanakimbia korona huko kwao). Siku ikishika vizuri ndio mtajua mtu aliye sema kinga ni bora kuliko tiba alikua ana maanisha nini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
IGP Sirro:Hatujafikia hatua hiyo ya kufunga mipaka.https://www.youtube.com/watch?v=mIALkuGuD1E&feature=youtu.be

Huyu naye ameshakuwamsemaji wa wizara ya afya?
Huu usahii wa killa mtu anatoa tamko utakuja kutuletea madhara kwa taifa. Nilisikia sehemu fulani akisema wapewe taarifa ya wagonjwa wa corona alafu yeye atatuma vijana wake kusaidia.
Anafikiri corona inadhibitiwa nabunduki, mabomu ya machozi na maji ya kuwasha washa?

AACHE WATAALAMU WASEME
 
Back
Top Bottom