IGP Sirro asema muda si mrefu atatoa majibu mauaji mkoani Pwani

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,498
9,279
Dar es Salaam. Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Simon Sirro amesema muda si mrefu atatoa majibu ya suala la mauaji yanayotokea mkoani Pwani.

IGP Sirro amesema hayo leo (Julai 5) wakati wa makabidhiano ya magari manne ya polisi yaliyotolewa msaada na Kampuni ya Great Wall Motors and Haval.

"Si kawaida yangu kusemasema ila muda si mrefu nitatoa majibu ya mauaji ya Pwani. Sisi Watanzania hatujazoea mambo ya fujo fujo, wale waliotumwa kwa ubaya ubaya sisi tunawajibu vibaya vibaya," amesema IGP Sirro.

Tangu Mei mwaka jana yalipoibuka mauaji ya kutumia risasi katika wilaya za Kibiti, Mkuranga na Rufiji mkoani Pwani, takriban watu 37 wameuawa wakiwamo askari polisi na viongozi wa Serikali za Mitaa.

Kamishina wa Polisi Kitengo cha Fedha na Usafirishaji, Albert Nyamuhanga amesema magari hayo yenye thamani ya Sh120 milioni kila moja, yatasaidia kupambana na uhalifu nchini.

"Kupatikana kwa magari haya kumeokoa fedha nyingi katika bajeti ya Serikali, hivyo wadau hawa wameunga mkono juhudi za polisi kukabiliana na uhalifu," amesema.

Mkurugenzi Mkuu wa Great Wall Motors and Haval, Jianguo Liu amesema magari hayo ni pongezi kwa kazi inayofanywa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na Jeshi la Polisi.

"Tunaunga mkono juhudi za polisi za kutunza amani na usalama wa raia," amesema Liu.

Chanzo:
mwananchi
 
Dar es Salaam. Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Simon Sirro amesema muda si mrefu atatoa majibu ya suala la mauaji yanayotokea mkoani Pwani.

IGP Sirro amesema hayo leo (Julai 5) wakati wa makabidhiano ya magari manne ya polisi yaliyotolewa msaada na Kampuni ya Great Wall Motors and Haval.

"Si kawaida yangu kusemasema ila muda si mrefu nitatoa majibu ya mauaji ya Pwani. Sisi Watanzania hatujazoea mambo ya fujo fujo, wale waliotumwa kwa ubaya ubaya sisi tunawajibu vibaya vibaya," amesema IGP Sirro.

Tangu Mei mwaka jana yalipoibuka mauaji ya kutumia risasi katika wilaya za Kibiti, Mkuranga na Rufiji mkoani Pwani, takriban watu 37 wameuawa wakiwamo askari polisi na viongozi wa Serikali za Mitaa.

Kamishina wa Polisi Kitengo cha Fedha na Usafirishaji, Albert Nyamuhanga amesema magari hayo yenye thamani ya Sh120 milioni kila moja, yatasaidia kupambana na uhalifu nchini.

"Kupatikana kwa magari haya kumeokoa fedha nyingi katika bajeti ya Serikali, hivyo wadau hawa wameunga mkono juhudi za polisi kukabiliana na uhalifu," amesema.

Mkurugenzi Mkuu wa Great Wall Motors and Haval, Jianguo Liu amesema magari hayo ni pongezi kwa kazi inayofanywa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na Jeshi la Polisi.

"Tunaunga mkono juhudi za polisi za kutunza amani na usalama wa raia," amesema Liu.

Chanzo:
mwananchi
Isije kuwa ni zawadi kama zile za yule wa ESCROW.
 
Wanatumia mbinu za kizamani kupambana na changamoto mpya
wasambaze picha za wahusika tuwasaidie kuwasaka
 
Kila la kheri kamanda sirro na usisite kusema kama kuna mkono wa wanasiasa.
 
MAJIBU MAKINI. TUSISIKIE KIONGOZI AU ASKARI KUUWAWA, NA WAUWAJI KUTOKOMEA KUSIKOJULIKANA.
 
Asianze tu na danganya toto kama bashite.Atutangazie kwa awamu mwishowe unasikia mbowe,Lowassa na sumaye"Kama namwona
 
Sirro ajitahidi kuwa na subira na akiba ya maneno!!! Ni hilo tu!! Aombe Sana awe na maamuzi ya busara muda woote wa utendaji wake pale kama IGP.....itamsaidia sanaa
 
Back
Top Bottom