IGP Sirro alalamikia unafiki ndani ya Jeshi la Polisi, Changamoto nyingine ni baadhi yetu kujihusisha na siasa

kiben10

JF-Expert Member
Apr 28, 2018
616
789
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro amwsema moja ya changamoto zinazolikabili jeshi hilo ni unafiki miongoni mwa askari wake. Sirro ameongea hayo leo Jumanne September 24, mwaka 2019 katika kikao kazi cha maafisa waandamizi wa jeshi hilo ambapo ameonekana kuwajibu Maafisa wa polisi wanaosema hatoshi katika nafasi hiyo.

"Tatizo linalotusumbua sisi Jeshi la Polisi pia ni unafiki. There is no way tukawa na IGP zaidi ya mmoja. Mimi sikujichagua. Kamanda wa polisi Kinondoni (Mussa Taibu) unanisikia? Kubali yaishe. Mimi sikujiteua mwenyewe, kwahiyo siwezi kujiona kama sitoshi katika nafasi hii. Aliyeniteua ndiye anaweza kuona kama natosha au sitoshi” amesema IGP Sirro.

Akijibu tuhuma hizo, Kamanda wa polisi Kinondoni ACP Mussa Taibu amesema IGP Sirro amemtaja yeye kama mfano lakini ujumbe huo haumhusu yeye. "Hiyo nondo ya IGP imepigwa mahususi kwa baadhi ya watu. Mimi nimetajwa tu kufikisha ujumbe"

Na case study yetu ni matukio ya Akwilina na Mwangosi, changamoto kubwa ambayo hujitokeza ni command (amri) inapokuwa weak (dhaifu) haya hutokea. Kilichotokea Kinondoni siwezi kusema lakini mnaweza kuwa mashuhuda, kuna mahali kama Jeshi la Polisi hatukutimiza wajibu wetu"



Zaidi soma...

Dar es Salaam. Inspekta Jenerali wa Polisi nchini Tanzania (IGP), Simon Sirro amesema kulingana na amri za jeshi hilo, askari atakayejihusisha na siasa lazima wenzake watamshangaa.

Ametoa kauli hiyo leo Jumanne Septemba 24, 2019 katika ufunguzi wa kikao cha siku tatu cha maofisa waandamizi wa polisi kinachofanyika jijini Dar es Salaam ambako ameeleza masuala mbalimbali yanayolikabili jeshi hilo, likiwemo la kujihusisha na siasa.

“Changamoto nyingine ni baadhi yetu kujihusisha na siasa, katiba iko wazi na police general order (kanuni za polisi) iko very clear (wazi kabisa) wala sio sifa, sisi Polisi wenzako tunakushangaa hata umma utakushangaa.”

“Watu wanataka kusikia unasema nini, wewe sio mwanasiasa unajiaibisha mwenyewe, tujikite kwenye majukumu yetu hayo unayofanya umeyatoa wapi,” amehoji Sirro.

Ameongeza, “Halafu unafanya hivyo kwa sababu uko kwenye nafasi hiyo tukikutoa hapo utaweza kufanyia nyumbani kwako? Si Pahala pa kufurahisha watu, wengine wanafanya vitu kutafuta umaarufu wa kisiasa tu, unamfurahisha nani?”
 
Huenda ikawa kweli maana kama tangu aingie madarakani jeshi limeajiri polisi 800 tu na wakati watangulize wake ilikua kila mwaka wana ajiri polisi sio chini ya 3000 kwa nini asiitwe hatoshi katika nafasi hiyo?
IGP hana uwezo wa kuajiri mtu atamlipa mawe?
.
Serikali ya awamu hii ajira sio kipaumbele chake kaa ufahamu.
CG wa Magereza ameomba hata hao 800 kanyimwa.

Anategemea utendaji unaendaje uko vituoni kama sio kuwaumiza wengine tu. Na awe makini maana hicho cheo kinatafutwa na wengi hata Magufuli anakitamani kwa kinywa chake mwenyewe alisha wahi kutamka "I wish I could be IGP"
Haya mimi simo
 
SEPTEMBER 24 2019

Inspekta Jenerali wa Polisi nchini Tanzania(IGP), Simon Sirro amesema tatizo linalolisumbua jeshi hilo ni unafiki, kusisitiza kuwa mwenye wadhifa kama wake yupo mmoja tu.

IGP Sirro ametoa kauli hiyo leo Jumanne Septemba 24, 2019 katika ufunguzi wa kikao kazi cha maofisa waandamizi wa polisi kinachofanyika jijini Dar es Salaam.

"Tatizo linalotusumbua sisi Jeshi la Polisi pia ni unafiki. There is no way tukawa na IGP zaidi ya mmoja, mimi sikujichagua.”

“Kamanda wa Kinondoni unanisikia (Mussa Taibu)? kubali yaishe, sikujiteua mwenyewe siwezi kujiona kama sitoshi katika nafasi hii,” amesema.

Katika ufafanuzi wake kuhusu kauli ya Sirro, kamanda huyo wa Kinondoni amesema, "Hiyo ni nondo kuwa watu (maofisa) waliopigwa hapo na kunitaja mimi (Sirro kumtaja) ilikuwa ni njia tu ya kufikisha ujumbe kwa baadhi ya watu."
 
Hivi ajira inatolewa na IGP?Kwani juzi yule aliyeomba kuajiri askari Magereza aliambiwa nini? IGP yupo vizuri basi tu binadamu tunatabia ya kusahau sana.Suala la ajira ni nyeti sana sidhani kama igp hapendi kuongezewa watendaji na kila sekta inaupungufu na hili ni boom
 
Huenda ikawa kweli maana kama tangu aingie madarakani jeshi limeajiri polisi 800 tu na wakati watangulize wake ilikua kila mwaka wana ajiri polisi sio chini ya 3000 kwa nini asiitwe hatoshi katika nafasi hiyo?

Anategemea utendaji unaendaje uko vituoni kama sio kuwaumiza wengine tu. Na awe makini maana hicho cheo kinatafutwa na wengi hata Magufuli anakitamani kwa kinywa chake mwenyewe alisha wahi kutamka "I wish I could be IGP"
Swala la ajira kwa hawamu hii wakulaumiwa ni rais mwenyewe hapo wengine hawana maamuzi hayo.

km wanaomba vibali vya ajira wanakataliwa wafanyaje sasa.

Juzi umemsikia mkuu amegoma kutoa ajira 800 zaidi askari magereza.
 
... kwani kuna mnyukano wa kugombea vyeo na madara Jeshi la Polisi? Mbona kauli ya IGP kana kwamba ina mwelekeo huo? Au ndio unafiki wenyewe?
 
Huenda ikawa kweli maana kama tangu aingie madarakani jeshi limeajiri polisi 800 tu na wakati watangulize wake ilikua kila mwaka wana ajiri polisi sio chini ya 3000 kwa nini asiitwe hatoshi katika nafasi hiyo?

Anategemea utendaji unaendaje uko vituoni kama sio kuwaumiza wengine tu. Na awe makini maana hicho cheo kinatafutwa na wengi hata Magufuli anakitamani kwa kinywa chake mwenyewe alisha wahi kutamka "I wish I could be IGP"
Hivi ubora wa IGP unapimwa kwa kuajiri askari wengi au tunaangalia amani na utulivu uliyopo Nchini?
 
"Tatizo linalotusumbua sisi Jeshi la Polisi pia ni unafiki. There is no way tukawa na IGP zaidi ya mmoja. Mimi sikujichagua. Kamanda wa polisi Kinondoni (Mussa Taibu) unanisikia? Kubali yaishe. Mimi sikujiteua mwenyewe, kwahiyo siwezi kujiona kama sitoshi katika nafasi hii. Aliyeniteua ndiye anaweza kuona kama natosha au sitoshi” amesema IGP Sirro.
 
Hii sijaipata mkuu kwamba haajiri magereza au nafasi atatoa lakini hazita zidi 800?
Swala la ajira kwa hawamu hii wakulaumiwa ni rais mwenyewe hapo wengine hawana maamuzi hayo.

km wanaomba vibali vya ajira wanakataliwa wafanyaje sasa.

Juzi umemsikia mkuu amegoma kutoa ajira 800 zaidi askari magereza.
 
Huenda ikawa kweli maana kama tangu aingie madarakani jeshi limeajiri polisi 800 tu na wakati watangulize wake ilikua kila mwaka wana ajiri polisi sio chini ya 3000 kwa nini asiitwe hatoshi katika nafasi hiyo?

Anategemea utendaji unaendaje uko vituoni kama sio kuwaumiza wengine tu. Na awe makini maana hicho cheo kinatafutwa na wengi hata Magufuli anakitamani kwa kinywa chake mwenyewe alisha wahi kutamka "I wish I could be IGP"
polisi wengi wa nini?,kazi kula mishahara ya bure tu na kuwabambikia watu kesi...........................hata hao waliopo ingefaa wapunguzwe tu,polisi imejaa rushwa
 
Inspekta Jenerali wa Polisi nchini Tanzania(IGP), Simon Sirro amesema tatizo linalolisumbua jeshi hilo ni unafiki, kusisitiza kuwa mwenye wadhifa kama wake yupo mmoja tu.

IGP Sirro ametoa kauli hiyo leo Jumanne Septemba 24, 2019 katika ufunguzi wa kikao kazi cha maofisa waandamizi wa polisi kinachofanyika jijini Dar es Salaam.
"Tatizo linalotusumbua sisi Jeshi la Polisi pia ni unafiki. There is no way tukawa na IGP zaidi ya mmoja, mimi sikujichagua.”

“Kamanda wa Kinondoni unanisikia (Mussa Taibu)? kubali yaishe, sikujiteua mwenyewe siwezi kujiona kama sitoshi katika nafasi hii,” amesema.

Katika ufafanuzi wake kuhusu kauli ya Sirro, kamanda huyo wa Kinondoni amesema, "Hiyo ni nondo kuwa watu (maofisa) waliopigwa hapo na kunitaja mimi (Sirro kumtaja) ilikuwa ni njia tu ya kufikisha ujumbe kwa baadhi ya watu."

Sirro aliyeteuliwa Mei 28, 2017 kuchukua nafasi ya mtangulizi wake, Ernest Mangu aliteuliwa kuwa Balozi amesema, “Natamani kumaliza nafasi yangu Jeshi la Polisi likiwa na heshima yake. Jeshi hili likiharibika tumeharibikiwa wote na mimi siwezi kumuwekea mtu kinyongo, mie sio wa aina hiyo kwa hiyo niwaombe ushirikiano.”
 
Back
Top Bottom