IGP Simon Sirro arejea toka Rwanda, ziara ya kikazi imegundua mengi kuhusu Tanzania

bagamoyo

JF-Expert Member
Jan 14, 2010
21,239
24,099

10 September 2021​

IGP SIRRO AFUNGUKA KUHUSU UGAIDI, ATAJA ALIYOYAKUTA RWANDA "KIKOSI MAALUM, VYUONI, MADRASA"



Baada ya Inspector General of Police (IGP) Dan Munyuza wa Rwanda kukutana na IGP Simon Sirro wamefanya mapitio ya taarifa za kiintelejensia zilizokusanywa kuhusu makosa yanayovuka mipaka ya nchi kama vile madawa ya kulevya, biashara haramu ya kusafirisha binadamu, silaha pia ugaidi kufuatia operesheni ya majeshi ya Rwanda na Tanzania katika jimbo la Cabo Delgado nchini Mozambique.

Operesheni ya hiyo imewezesha kupata taarifa za nyingi za kiintelejensia za watu mbalimbali wanaojihusisha na ugaidi katika jimbo la kaskazini la Mozambique la Cabo Delgado lakini wanatokea sehemu mbalimbali za Tanzania na Rwanda pamoja na nchi zingine.

Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, IGP Simon Sirro amesema kufuatia ugunduzi huo watawashirikisha viongozi wa Kidini kwa ajili ya kupitia mafunzo ya Dini wanayofundishwa watoto kuanzia Chekechea, Sunday schools, Madrasa, Shule za Sekondari hadi Vyuoni kuonana pia na maaskofu na masheikh ili Kudhibiti vichocheo vya Ugaidi. Vyombo hivyo vya usalama vitataka kujua Je mafunzo wanayotoa viongozi wa dini kwa watoto na vijana ni kwa ajili ya kujenga utaifa na uzalendo au ni kwa ajili ya kubomoa taifa.

IGP Simon Sirro ametoa rai kwa wazazi, walezi wa watoto na vijana pia bila kusahau watu wenye wenzi wao, marafiki na majirani kutoa taarifa Polisi wanapoona kuna vitendo visivyo vya kawaida katika jamii zao ili vyombo vya usalama viweze kudhibiti matukio yanayoweza kuvuruga usalama wa nchi.

IGP Sirro ameyasema hayo leo katika uwanja Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere mara baada ya kumaliza ziara ya kikazi nchini Malawi ambapo amesema katika nchi hiyo kuna kikosi maalum cha kufuatilia maeneo hayo ya Elimu.

10 September 2021​

Kigali, Rwanda

Rwanda, Tanzania police forces hold bilateral talks​


Rwanda National Police (RNP) and Tanzania Police Force (TPF) held a bilateral meeting in Kigali, on Tuesday, September 7, which mainly focused on strengthening cooperation against cross-border crimes especially terrorism.

The bilateral meeting held at the RNP General Headquarters in Kacyiru was co-chaired by Inspector General of Police (IGP) Dan Munyuza and his counterpart of Tanzania, Gen. Simon Nyakoro Sirro.

Sirro and his delegation are in Rwanda since Monday for a four-day visit aimed at further strengthening ties between the two friendly Police institutions.

The meeting followed another one held in Tanzania in May.

While speaking during the bilateral meeting, Munyuza thanked his counterpart for honouring the invitation, which he described as a “sign of mutual trust and existing friendship between our two countries.”

He commended the existing cooperation framework especially in information flow on terror activities in the region and particularly in Cabo Delgado, Mozambique, which lies on the border with Tanzania in the south.

“During the course of the operations against terrorists in Cabo Delgado, in which forces of our two countries are involved, we have collected information on ground, either from captured terrorists or those killed in action, which we have been sharing with you as we endeavour to devise strategies to secure our region against violent terrorists that continue to kill innocent people in our region and make thousands homeless and refugees in their own countries,” Munyuza said.

As the terrorists continue to lose ground in Mozambique, Munyuza said, there is need to carefully establish networks in the region and share timely information on their next course of action.

“More than ever before, we need to work together to update our approaches, especially in controlling our borders against movement of radical Muslims and be able to detect movement of likely terror materials in our region. Terrorists fleeing from their hideouts in Mozambique may infiltrate our borders and establish cells in our countries or in neighbouring countries” Munyuza said.

This struggle against terrorism, he said, should be at the top of the agenda for the Eastern Africa Police Chiefs Cooperation Organization (EAPCCO) to simplify operational information exchange and conduct joint operations against terrorists to address and avoid the gap between terrorist threat and the collective response to defeat terrorists.

Tanzania is the current chair of the 14-member regional bloc.
Munyuza reiterated Rwanda National Police commitment and closer cooperation with Tanzania Police Force and the region in combatting other cross-border and transnational crimes.

On his part, IGP Sirro said: “We have a challenge of terrorism; it is high time we deal with it. We must always be alert. Whenever we get information from Rwanda, we immediately act on it. I can assure you that through the information from Rwanda, we have managed to arrest many suspects.”

The bilateral meeting is in line with the Memorandum of Understanding signed between Rwanda National Police (RNP) and Tanzania Police Force (TPF) in 2012 to cooperate and collaborate in security related matters, including joint exercises, operations, training and timely exchange of security information.
Source : Rwanda, Tanzania police forces hold bilateral talks
 
Yanaweza kuwapo japo si kwa kiwango husika. Pia, wingi wa raslimali unaweza kuchochea mataifa au makundi kutaka kuvuruga amani ili kupata uchochoro wa kupata mali kwa bei rahisi kama ambavyo imekuwa ikiendelea nchini DRC. Pia kuna baadhi ya dini zinaharibu akili za vijana wetu kwa kuwafundisha kujikana na kudharau mila zao kiasi cha kujiona kama watu fulani ambao si wao.
 
Yanaweza kuwapo japo si kwa kiwango husika. Pia, wingi wa raslimali unaweza kuchochea mataifa au makundi kutaka kuvuruga amani ili kupata uchochoro wa kupata mali kwa bei rahisi kama ambavyo imekuwa ikiendelea nchini DRC.
Ugaidi ni neno pana . Ugaidi si sawa na uasi .. Twende kwenye chimbuko la neno Ugaidi kwanza ndio ujue kuna kitu kinalengwa au wanakitaka
 
8 Sept 2021

IGP SIMON SIRRO ALIVYOTUA NCHINI RWANDA



Mkuu wa Polisi Tanzania IGP Simon Sirro alipokuwa ziarani nchini Rwanda ambapo pamoja na mambo mengine, walijadili pamoja na IGP wa Rwanda namna ya kukabiliana na Ugaidi
Binago TV
 
Ugaidi ni neno pana . Ugaidi si sawa na uasi .. Twende kwenye chimbuko la neno Ugaidi kwanza ndio ujue kuna kitu kinalengwa au wanakitaka
kikubwa sitaki kunyumbua neno ugaidi naelewa unacho kiwaza lakini kumbuka hao wanaoitwa magaida kama ni kweli au uwongo wapendwa wao wa karibu hawatahusika na madhara yoyote lakini hohehaye mimi na wewe na ndugu zetu tutateseka sana.

Kikubwa tumwombe Mungu uwe ugaidi wa kisiasa usiwe ugaidi halisi.
 
Ugaidi unafadhiliwa sehemu kubwa na viongozi wa kiafrika. Ushahidi Ni vipi haya makundi wapate silaha wakati majeshi na vikosi vya usalama vimejaa kila Kona kulinda mipaka
 
Haya mambo ya uagaidi yameanzia wapi kwenye hizi nchi zetu au kuna kitu wana kitafuta ?
Hakuna kitu kweli kuna kitu wanakipika.....ugaidi upo zaidi miaka 30 walikuwa wapi kubadilishana uzpefu majirani miaka yote wanafanya hivyo pia interpol ipo leo ndio aje story za kupika hizo.....hakuna kitu hapo siasa tu hizo
 
Back
Top Bottom