IGP Simon Sirro ana wajibu wa kutueleza Chama cha Siasa kilichopanga kuchoma vituo vya kuuza mafuta Nchini

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,880
Leo IGP Simon Sirro katika taarifa yake kwenye kikao chake na NEC ameeleza umma kuwa kipo Chama cha Siasa kilichopanga kuvuruga Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu 2020 kwa kupanga kuchoma vituo vya kuuza mafuta aina ya diesel na petrol nchini.

Kwa kuzingatia cheo alicho nacho kwa nchi, hizi mi tuhuma nzito na hazihitaji kuelezwa juu juu bali lazima kuwe na taarifa na ushahidi wa kueleweka.

Kuchoma vituo vya mafuta ni sawa na kutangaza vita, siyo jambo dogo hivyo taarifa isiyo ya juu juu inapaswa kutolewa na hatua zinazokusudiwa kuchukuliwa. Chama cha Siasa kujihusisha na vitu vya aina hii ni sawa na ugaidi. Tunahitaji taarifa ila isiwe na mawaa.
 
Uchaguzi wa mwaka huu, Mungu atusaidie, maana kuna wanasiasa ambao hawaamini kua chama tawala kitakubaliana na matokeo ya kwenye sanduku la kura, na chama tawala kinaamini kuwa hatakama matokeo yatatangazwa na vyama vya upinzani vikakataa kuridhia, wafuasi na viongozi wa vyama hivyo, watakaa kimya.
 
Siro muongo anataka kutuletea zile za IGP MAHITA na CUF kuwa CUF wamebeba majambia kwenye MaContainer. Kama kuna njama za kuchoma vituo za mafuta basi watakuwa ni CCM wakilindwa na Polisi halafu wasingizie Opposition.

This time wameshikwa pabaya. Tendeni haki ili msije mkapelekwa The Hague au mkafungwa hapa hapa nchini kwa makosa ya kutumia vyeo vyenu vibaya
 
Siro muongo anataka kutuletea zile za IGP MAHITA na CUF kuwa CUF wamebeba majambia kwenye MaContainer. Kama kuna njama za kuchoma vituo za mafuta basi watakuwa ni CCM wakilindwa na Polisi halafu wasingizie Opposition. This time wameshikwa pabaya. Tendeni haki ili msije mkapelekwa The Hague au mkafungwa hapa hapa nchini kwa makosa ya kutumia vyeo vyenu vibaya

Ccm hawajaingia uwanjani ili mlinganishe mziki mnaanza kutamba na vimifereji eti mafuriko. Hivi kuna nyomi zaidi ya ile ya 2010 au 2015-watu walideki lami bila kusahau myomi ya 1995
 
19 Agosti 2020
Moshi, Tanzania

MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO AMTAKA DC SABAYA KUMPA TAARIFA MSAFARA WA LISSU KUSHAMBULIWA




Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira, ametoa kauli rasmi ya serikali kuhusiana na vurugu zilizotokea katika mji wa Bomang'ombe wilaya ya Hai wakati mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Tundu Lissu alipofika wilayani humo kutafuta wadhamini.

Katika taarifa hiyo rasmi aliyoitoa leo Agosti 19, 2020, mkuu huyo wa mkoa ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa huo, amemtaka mkuu wa wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya, kumpatia taarifa ya maandishi ya namna alivyoshughulikia suala hilo.

Source:
Mwananchi digita
 
Huyo Sirro nae keshakuwa mwanasiasa, siku hizi hata sihangaiki kutafakari kauli zake.
 
Kweli nyie ni Nyumbu wa ajabu sana. Ccm hawajaingia uwanjani ili mlinganishe mziki mnaanza kutamba na vimifereji eti mafuriko. Hivi kuna nyomi zaidi ya ile ya 2010 au 2015-watu walideki lami bila kusahau myomi ya 1995
Wakikujibu Nitag
 
Leo IGP Simon Sirro katika taarifa yake kwenye kikao chake na NEC ameeleza umma kuwa kipo chama cha siasa kilichopanga kuvuruga uchaguzi mkuu wa mwaka huu 2020 kwa kupanga kuchoma vituo vya kuuza mafuta aina ya diesel na petrol nchini...
Hata IGP Mahita aliwai sema kuna kontena la visu la CUF lakn Leo kachoka yupo kwake anabaki kuonja chumvi kwe mboga tu
 
19 Agosti 2020
Moshi, Tanzania

MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO AMTAKA DC SABAYA KUMPA TAARIFA MSAFARA WA LISSU KUSHAMBULIWA



Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira, ametoa kauli rasmi ya serikali kuhusiana na vurugu zilizotokea katika mji wa Bomang'ombe wilaya ya Hai wakati mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Tundu Lissu alipofika wilayani humo kutafuta wadhamini.

Katika taarifa hiyo rasmi aliyoitoa leo Agosti 19, 2020, mkuu huyo wa mkoa ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa huo, amemtaka mkuu wa wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya, kumpatia taarifa ya maandishi ya namna alivyoshughulikia suala hilo.
Source : Mwananchi digita
Ha ha ha ha ha patamu hapo
 
Defensive mechanisim ya matukio ya kuchoma ofisi za Chadema Bila kutolea ufafanuzi huo anakuja na counter atack dhidi ya chama kilichoonewa!!!

Kabisa, bado kamanda Sirro anadhani watanzania tuko zama za giza za majambia ya Mahita enzi za CUF ngunguri. Na hata huu uchomaji wa ofisi za cdm huenda atakuwa anajua vizuri. Namshauri Siro arudi tu studio akaendelea kumalizia ile episode ya kutekwa kwa Mo. Na manunuzi ya yale magari ya polisi kule bandarini.
 
19 August 2020
Mbeya, Tanzania

OFISI YA CHADEMA YACHOMWA MOTO MBEYA, MWENYEKITI MKOA AFUNGUKA MAZITO FOMU ZA UBUNGE WA JOSEPH MBILINYI, UDIWANI....



OFISI YA CHADEMA MKOANI MBEYA IMECHOMWA MOTO, NA KATIKA TUKIO HILO BAADHI YA NYARAKA ZIMEUNGUA HASA FOMU ZA MADIANI AMABAZO KWA MUJIBU WA MWAMBIGIJA MWENYEKITI WA MKOA, AMESEMA WALIPANGA KUZIREJESHA LEO.

Source: JORDAN MEDIA
 
Back
Top Bottom