IGP Mwema, jibu maswali yafuatayo

Nzagabulu

Member
Jan 3, 2013
60
8
Kufuatia matumizi ya nguvu unayowaamrisha polisi wako na baadaye kukamata viongozi wa chama cha Demokrasia na maendeleo na kuwafikisha mbele ya mahakama, nina maswali matano ya kukuuliza ndugu IGP Mwema.

1. Ni kesi ngapi walizofunguliwa viongozi wa Chadema wakiwa kwenye mikutano munayoiita haina kibali? naomba
ufafanue vizuri, mfano, Mbowe ana kesi ngapi, Slaa,Zitto, Lema, Lissu, na wengine

2.Ni kesi ngapi zilizotolewa hukumu hadi leo

3.Ni kesi ngapi ambazo jeshi la polisi linalowakilisha jamuhuri limeshinda.

4. Kama kama hakuna kilichofanyika kwa nini muendelee kuwafikisha mahakamani wakati mkijua wanaachiwa?

5.Kwa nini ustumie busara zako kuwashauri hao wanaokutuma njia bora ya kufanya ili kuzima nguvu ya umma kuliko
kuendelea kutumika kuua raia wasio na hatia?
 
Kufuatia matumizi ya nguvu unayowaamrisha polisi wako na baadaye kukamata viongozi wa chama cha Demokrasia na maendeleo na kuwafikisha mbele ya mahakama, nina maswali matano ya kukuuliza ndugu IGP Mwema.

1. Ni kesi ngapi walizofunguliwa viongozi wa Chadema wakiwa kwenye mikutano munayoiita haina kibali? naomba
ufafanue vizuri, mfano, Mbowe ana kesi ngapi, Slaa,Zitto, Lema, Lissu, na wengine

2.Ni kesi ngapi zilizotolewa hukumu hadi leo

3.Ni kesi ngapi ambazo jeshi la polisi linalowakilisha jamuhuri limeshinda.

4. Kama kama hakuna kilichofanyika kwa nini muendelee kuwafikisha mahakamani wakati mkijua wanaachiwa?

5.Kwa nini ustumie busara zako kuwashauri hao wanaokutuma njia bora ya kufanya ili kuzima nguvu ya umma kuliko
kuendelea kutumika kuua raia wasio na hatia?
Ushauri huo ataupata pale atakapo ona mauaji kwa viongozi wa Serikali yamekuwa hayazuiliki,mauaji kwa polisi kila siku,uchomaji wa vituo vya polisi na si mda mrefu silaha zitakapo sambaa mikononi mwa raia au Bomu litakapomlipua bosi wake atapata akili kwamba leo ndio makosa yalipotokea siku hizo leo itakuwa inaitwa mwaka juzi au miaka kadhaa iliyopita,maana Polisi na Ccm wanaleta ugomvi wa mawe wakati wananyumba za vioo....Na uvumilivu sasa basi kilichobaki wasubiri majibu yao maana sasa inabidi polisi ajue kazi hiyo ikikosewa husababisha mauaji ya Kimbari
 
Usidhani hawafahamu kwamba wamechemsha, sasa hivi kwenye vikao vyao wamechanganyikiwa waseme nini. Wanaoneana aibu kwani wakati wanapanga hawakujua kama matokeo yake yatakuwa haya. Wabunge wa chadema wakimaliza hapo wawaite wananchi watupe mrejesho na hatua stahiki za kuchukua kwani sheria zinavunjwa dhahiri na tuliowapa dhamana ya kuzisimamia. Kuna wakati nikiona wazungu wanatudharau nachukia sana, lakini kama mambo yetu ndo hivi unategemea nini. Hakuna kesi yoyote iliyoko the Hague kurudishwa afrika maana viongozi wetu hawafuati sheria full stop.
 
Back
Top Bottom