IGP Ernest Mangu Hebu Muulize IGP Said Mwema maswali haya ili upate pa kuanzia!

iPad ya Apple

JF-Expert Member
Jul 21, 2013
322
126
1. Je, Makao Makuu ya police ni nyumbani kwa police wanaoharibu? Kuna mifano mingi ya police mikoani wanaoharibu hupandishwa cheo na kuhamishiwa makao Makuu ya jeshi la police Michael Kamuhanda is a case study.

2. Kwanini Jeshi la police limekuwa likituhumiwa kukandamiza Upinzani hasa Chadema bila kukanusha na katika vifo vyote vilivyotokea ktk mikutano ya CDM kuna mkono wa jeshi la police, mfano Arusha, morogoro , Iringa na Igunga?

3. Ilikuwaje walio wauua kamanda Barlow na Dr. Mvungi wakakamatwa mapema kuliko walio walio wateka, kutesa na kuwang'oa baadhi ya viungo Dr. Ulimmboka na Absolom Kibanda?

4. Wako wapi police walio Kuwa wanatembea na kichwa cha binadamu na kubambikia kesi watu huko morogoro?

5. Wako wapi police waliojimilikisha mamilioni ya liyokuwa yameporwa kariakoo?

6. Je, ni kweli kuna kikundi cha uharifu kilicho wahi kumpelekea gari Said Mwema linalodaiwa Kuwa ni la milioni Karibu 400. Ambalo
liliingia Tanzania na KM 0?

7. Je ni kwanini jeshi la police linapokuwa linatuhumiwa hukimbilia kuunda tume za kujichunguza lenyewe?

8. Je wako wapi wale maofisa wa jeshi la police walio watapeli vijana kule CCP Moshi kwa kuwachangisha laki moja hadi laki mbili kila mmoja na kisha kuwanyooa vipara na baadaye kuwaambia Hakuna nafasi za kujiunga na jeshi la police?


9. Wako wapi Askari walio badilisha heroine na Kuwa sukari kule mbeya na Kagera?

10. Pia muulize na wewe kama uendelee kufanya kazi kwa maelekezo ya CCM badala ya kwa mujibu wa sheria.


NB: Akikujibu kwa ufasaha hayo maswali utapata pa kuanzia vinginevyo utavurunda ukiingia kichwa kichwa tu.
 
Hoja zako zimekaa kichama zaidi!!! Utaifa kwanza vyama baadae.
 
nimekubali wewe ni miongoni mwa watu ambao ni wasikilizaji wazuri lakini yawezekana kabisa umepungukiwa suala la ufuatiliaji, mimi niliwahi kusikia juu ya hatua zilizowahi kuchukuliwa dhidi ya hao uliowataja. Hata hao ambao mapolisi waliorudishwa makao makuu ya Upolisi mimi si dhani hiyo makao makuu eti ni sehemu ya watu walioharibu la asha! ni nacho amini makao makuu ndiyo kitovu cha uboreshaji na jeshi alifuati sera za chama jeshi linafuata sheria na ikiwa kazi kubwa waliyonayo ni kulinda raia na mali zao. Kingine IGP Mangu, hakutoka kwenye Asasi ama Taasisi za Kiraia ziwe za hapa ndani ya nchi ama nje huyu yumo ndani ya Idara ya Polisi na kwa kumbukumbu zangu ameshakuwa RPC katika mikoa miwili Pwani na Mwanza, hivyo anafahamu vyema.
 
1. Je, Makao Makuu ya police ni nyumbani kwa police wanaoharibu? Kuna mifano mingi ya police mikoani wanaoharibu hupandishwa cheo na kuhamishiwa makao Makuu ya jeshi la police Michael Kamuhanda is a case study.

2. Kwanini Jeshi la police limekuwa likituhumiwa kukandamiza Upinzani hasa Chadema bila kukanusha na katika vifo vyote vilivyotokea ktk mikutano ya CDM kuna mkono wa jeshi la police, mfano Arusha, morogoro , Iringa na Igunga?

3. Ilikuwaje walio wauua kamanda Barlow na Dr. Mvungi wakakamatwa mapema kuliko walio walio wateka, kutesa na kuwang'oa baadhi ya viungo Dr. Ulimmboka na Absolom Kibanda?

4. Wako wapi police walio Kuwa wanatembea na kichwa cha binadamu na kubambikia kesi watu huko morogoro?

5. Wako wapi police waliojimilikisha mamilioni ya liyokuwa yameporwa kariakoo?

6. Je, ni kweli kuna kikundi cha uharifu kilicho wahi kumpelekea gari Said Mwema linalodaiwa Kuwa ni la milioni Karibu 400. Ambalo
liliingia Tanzania na KM 0?

7. Je ni kwanini jeshi la police linapokuwa linatuhumiwa hukimbilia kuunda tume za kujichunguza lenyewe?

8. Je wako wapi wale maofisa wa jeshi la police walio watapeli vijana kule CCP Moshi kwa kuwachangisha laki moja hadi laki mbili kila mmoja na kisha kuwanyooa vipara na baadaye kuwaambia Hakuna nafasi za kujiunga na jeshi la police?


9. Wako wapi Askari walio badilisha heroine na Kuwa sukari kule mbeya na Kagera?

10. Pia muulize na wewe kama uendelee kufanya kazi kwa maelekezo ya CCM badala ya kwa mujibu wa sheria.


NB: Akikujibu kwa ufasaha hayo maswali utapata pa kuanzia vinginevyo utavurunda ukiingia kichwa kichwa tu.

Swali La Nyongeza;
Ni lini wezi wa vifaa vya kwenye magari "Wazee wa Power Window" watakamatwa na kuacha kutamba mitaani kila kukicha??
 
Umemuuliza mangu maswali ya msingi sana,ila kwa jinsi navyoifahamu inji hii,hakuna lolote litakalobadilika,ndo maana vijana wengi hawana uzalendo na inji yao,I mean nchi yao!
 
wewe siyo Advera Senzo

utambulisho wangu si upo hapo? au unadhani nimeficha kama wa kwako.tena umetukuza uzungu wakati ss waafrika tunayo majina meengi mazuri. lkn isiwe taabu mm siyo senzo ila changamoto za jeshi la polisi ni kubwa mno. kuanzia askari,maslahi,vitendea kazi mahusiano na raia.makazi yao.uchache wa vituo bora vya polisi.mafuta ya magari ,nyaraka za kazi nk.kingine askari au ofisa wa polisi kuamishiwa makao makuu yao kule alikotoka hakubaki wazi anapelekwa mwingine hivyo ni njia mojawapo ya kuboresha utendaji kazi. mh kamuhanda alipandishwa cheo hivyo alistahili kuhamishwa kwenda makao makuu.mafuvu walifukuzwa kazi na kufikishwa mahakamani.kariakoo walifukuzwa kazi na kufikishwa mahakamani. CDM wao wenyewe sio wasikivu,wanadharau kwa vyombo vya dola kwa kuwa ndo stahili yao ya kujitangaza kwa umma.CCM iko wazi ni lazima sera zake zisimamiwe na serikali polisi ni moja ya vyombo vya usimamizi wa sheria..ukamatwaji wa wahalifu ili mhalifu akamatwe kunatakiwa kuwe na chanzo kilichoachwa na mhalifu.lkn kama mhalifu amefanya kazi yake kwa umakini ni vigumu mno kubainika hapa jamii nzima inahusika si polisi peke yao.mwisho mavazi ya askari yako hovyo.mbwa wa polisi hovyo.farasi hovyo.magari hovyoo.makazi yao hovyo. vituo vya polisi vichache na hovyo.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom