IGP ateua makamanda wapya wa mikoa, AHMED MSANGI AULA

Una rekodi za utendaji wao mkuu ili kukazia msimamo wako??!!!!

mkuu nia yangu ni kuchokoza mada ili tufike mahali tuache propaganda zisizo na maana tuache mambo ya udini ukabila na haya mambo ya rika yanayochipukia kwa kasi
 
mkuu nia yangu ni kuchokoza mada ili tufike mahali tuache propaganda zisizo na maana tuache mambo ya udini ukabila na haya mambo ya rika yanayochipukia kwa kasi

Tupo pamoja mkuu I wish mtu alete hiyo rekodi maana.si umesoma inasemekana tangu mzee wao alikuwa RPC, brothers wawili RPCs sasa hapo huwezi kusimama passive without even thinking on this leave alone to say or write on the same!!!!
 
Taarifa ya IGP ya uteuzi wa Makamanda wa Polisi wa Mwanza, Mbeya na Simiyu
08/12/20130 Comments

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Said Mwema, amefanya uteuzi wa Makamanda wa Polisi kwa Mikoa mitatu Mwanza, Mbeya na Simiyu, ambapo amemteua Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Valentino Mlowola kuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza, Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ahmed Msangi kuwa Kamanda wa Polisi mkoa
wa Mbeya na Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Charles Mkumbo kuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Simiyu na aliyekuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Simiyu, SACP Salum Msangi amehamishiwa Makao Makuu ya Polisi Dar es Salaam.


Aidha, Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Mara Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP) Jafary Ibrahim amehamishiwa Kanda Maalum ya Dar es Salaam kuwa Mkuu wa Upelelezi na nafasi yake inachukuliwa na Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP) Rogathe Mlasani kutoka Makao Makuu ya Upelelezi Dar es Salaam.


Wengine ni Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP) David Mnyambuga kutoka Makao Makuu ya Upelelezi Dar es Salaam anaenda kuwa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Tabora, Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP) Martin Otieno kutoka Kanda Maalum ya Dar es salaam amehamishiwa Makao Makuu ya Polisi kuwa Mkuu wa kitengo cha Teknohama na Mrakibu wa Polisi (SP) Gidion Msuya ambaye alikuwa Kaimu Mkuu wa Upelelezi wa mkoa wa Tarime Rorya amehamishiwa Tunduru kuwa Mkuu wa Polisi wa Wilaya (OCD).


Imetolewa na:
Advera Senso-SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.









Source: Taarifa ya IGP ya uteuzi wa Makamanda wa Polisi wa Mwanza, Mbeya na Simiyu - wavuti.com

Kwani 20130 imeshafika kamanda, au duuuuu!!
 
Ernest Mangu aliyekuwa rpc wa mwanza mara baada ya kumuua yule mwenzao naye kapelekwa wapi?
 
Huyo msangi mng'a meno na kucha huko mbeya tayari muandike maumivu na muwe mnatembea na ganzi.
Viva home boy mkumbo.

Mapuma Miyoga! Acha ukabila kaka wewe ni wa Kinampanda na Mimi wa Kisiriri na Mkubo wa Tutu!

Songela sana Mkumbo! Ukiwa chadema unaathirika na dhana ya ukabila!
 
Jamani wana jamvi ninachukua furusa hii kumpongeza kijana mchapa kazi yule aliyekuwa RCO Central Ahmed Msangi, ameteuliwa kuwa RPC Mbeya baadaya kuonyesha ufanisi katika utendaji wake. Kweli mungu akutie nguvu kwenye nafasi uliyopewa hasa kutokana kwamba, unakwenda kufanya kazi na vichwa vya mapolisi wenye elimu kukuzidi wewe. Hongera.
 
Jamani wana jamvi ninachukua furusa hii kumpongeza kijana mchapa kazi yule aliyekuwa RCO Central Ahmed Msangi, ameteuliwa kuwa RPC Mbeya baadaya kuonyesha ufanisi katika utendaji wake. Kweli mungu akutie nguvu kwenye nafasi uliyopewa hasa kutokana kwamba, unakwenda kufanya kazi na vichwa vya mapolisi wenye elimu kukuzidi wewe. Hongera.
 
Loooh. Si huyu yule mng'oa kucha ? Haya Mbeya anzeni kujihami maana kucha zeenu na pumb ndio zake. Mwamkumbuka Ulimboka? Huyu jamaa ni noma .
 
Back
Top Bottom