Ignore list on JamiiForums: Maboresho ya mwaka 2020

Melo to me this is not crucial

Kila mara humu tunalalamika viongozi wetu katika mambo mbalimbali na hata kudai watusikilize na wasipotusikiliza tunandelea kulalama je kumbe wanavyotuignore ni sawa? Pía wakiignore maendeleo kwa umma ni sawa kwani nasi kama binadamu tunapenda kusikia na kuona yanayotupendeza! Basi tusiwakwaze na viongozi wetu ili wasituignore bali watupende kwa kusifia
Binadamu si option kupatwa, kusikia au kuona mabaya au mazuri tu kwani sarafu ya maisha ni pande mbili( uzuri/ubaya)

Kuna watu wanaweza kutumia fursa hii kuniignore pale juu, ni sawa kwa kuwa majumbani mwao watakutana na haya wanayoyakimbia, huwezi kuwa bora bila kupingwa hadharani na sirini( tuko na vivuli lkn bado tunaignore vipi tungekuwa og)
Kama unajitoa ufahamu muda wote
Kuwa ignored hakuepukiki
 
Daah sijui kwanini huwa sipendi kublock wala kuignore mtu yeyote kwenye mtandao wowote wa kijamii. Wanaonikwaza huwa naamua kuishi nao hivyo hivyo tu kibishibishi.
 
Akina kivuruge hawana Raha. Nimechagua kutomuignore mtu Kwani unaweza kufanya hivyo kumbe kiumbe huyo ana kasoro. Mfano mdogo ni ushabiki dhidi ya Corona, ukipewa taarifa kila siku maabara ya Taifa zinaingia sample ngapi utashangaa , ngoja tunyamaze majuha waendee kushabikia uongo.
 
Mkuu Maxence Melo , this improvement is good. Lakini pia hii yaweza kupunguza chachu ya mijadala humu jf.

Mfano jukwaa la Siasa ndiyo jukwaa ambalo nadhani linaongoza kuwa viewed na mijadala mingi. Kupamba moto kwa jukwaa hili ni kutokana na migongano ya hoja za wachangiaji. Migongano ya hoja ni based on political affiliation/belief ya mtu husika.

Na nionavyo mimi binafsi, members wanaonekana 'kuchukiwa' humu ni wale wanaotoa maoni yao kusupport or kufavor utawala huu wa awamu ya tano wa ccm, mfano members kama Bia yetu , USSR , Magonjwa Mtambuka , jingalao , n.k

Hao ni baadhi ya members ambao wao wameamua kuweka wazi political affiliations zao na wanaandika mawazo yao kwa mlengo huo.

Nikiangalia trend kufuatia maboresho haya ya 'ignore' button, member BIA YETU ndiye ataongoza kuwa ignored sana humu jf, sio kwa sababu anatukana sana watu, bali ni kwa sababu tu maoni yake ya kisiasa hayapendwi na mtu wa upande mwingine kisiasa!

Tukianza kutandikana 'ignore' button kwa sababu ya political affiliations/oppion, then tunaelekea pia kutandikana 'ignore' button kwa sababu ya religious affiliations/opinion zetu.

Jf portrays itself as the place "Where We Dare To Talk Openly". Kwa kuzingatia na kuitekeleza kauli mbiu hii, jf is adhering to one of the principles of natural justice ambayo ni Haki ya Kusikilizwa. Yes, mtu unapompa platform ya yeye azungumze openly, impliedly unakuwa umempatia haki ya kusikilizwa (right to be heard).

'Ignore' button ni systematic switch ya kuziba masikio. Right to be heard is meaningless endapo wasikilizaji/wasomaji wameziba masikio na kuvaa miwani ya mbao (ignore button)!

Mtu akiwa ignored sana, itaathiri contribution flow yake ya threads or posts. Ikifanyika kwa yule na yule na yule, in the long run itaathiri chachu ya mijadala hapa Jf. Jukwaa litakosa hoja ama mawazo kinzani, eventually jf will be full of threads za maoni ya mlengo mmoja.

Uwepo wa migongano ya hoja na mijadala kinzani, ni chachu kubwa na pia inaisaidia sana jf kutoonekana ni politically based upande mmoja.

Mimi nashauri 'Ignore Button' iwekwe kwenye Threads tu, not at individual level.

Mfano tu: mkuu Mshana Jr naweza bonyeza Ignore Button kwenye thread yake ya kisiasa, ila nikafaidika maarifa kwenye thread yake nyingine ya mambo ya ulozi.

Au naweza block/ignore Thread ya kisiasa ya mkuu Hornet , ila Thread yake nyingine ya mambo ya biashara ikanipa maarifa.

-Kaveli-
Huu ujumbe murua wahuni wa upinzani wanaupita kama hawauoni

Ni ajabu wanashangilia kuwablock watu, uoga tu

Basi bakini peke yenu tuone mtafika wapi
 
Ni ubunifu mzuri lakini kwa upande wa siasa si mzuri. Hii maana yake wale wasiotaka hoja za upande mwingine watakuwa wanapigana makufuli na mwisho itaua msisimko wa mijadala. Raha ya mjadala wowote ni uhakika wa kupata hoja kinzani au mawazo tofauti hata kama huyapendi.
 
Back
Top Bottom