mpayukaji
JF-Expert Member
- Oct 31, 2010
- 940
- 349
Ingawa majonzi bado yapo kutokana na msiba wa Steven Kanumba, kuna haja ya kuwakumbusha CCM kuwa ahueni waliyoipata hasa Livingstone Lusinde aka Domo Chafu aka Kichaa imetoweka. Lazima tuwarejee ili Lusinde ashughulikiwe. Ingawa CCM waliutumia msiba kuficha aibu yao, bado tatizo liko mlangoni likiwangoja. Sasa igizo la CCM la kumtumia Kanumba limekwisha turejee kwenye kashfa za Lusinde na kipigo cha CCM. Hata hili la Lema kuvuliwa ubunge bila mkashifiwa kukanyaga mahakamani laweza kuishia kuwa aibu ya mahakama hata CCM. Je wadau mna mawazo gani?