sir.JAPHET
JF-Expert Member
- May 18, 2012
- 699
- 133
[h=2][/h] Jumanne, Novemba 20, 2012 06:59 Na Oliver Oswald, Dar es Salaam
CHUO cha Usimamizi wa Fedha (IFM), kinatarajia kufanya mdahalo mkubwa Desemba 7, mwaka huu, kuhusu Fao la Kujitoa kwa wafanyakazi nchini. Hatu hiyo ni moja ya kutambua changamoto mbalimbali zinazolikabili Taifa kwa kuchambua mada mbalimbali zinazohusu jamii.
Akizungumza na MTANZANIA, Dar es Salaam jana, Mhadhiri Msaidizi wa Sheria za Biashara chuoni hapo, Agustus Fungo, alisema mdahalo huo utajikita kujadili masuala mbalimbali.
Fungo alisema mdahalo huo utaangazia Sera ya Hifadhi ya Jamii, sheria za mfuko, nadharia ya hifadhi ya jamii na hali halisi ya maisha ya Watanzania kwa sasa.
Fungo alisema mdahalo huo unatarajiwa kuongozwa na Mkufunzi Mkuu wa Chuo cha Takwimu cha Afrika Mashariki (EASTC,) Camillus Kassala.
Alisema mada nyingine zitakazojadiliwa ni pamoja na ulipaji wa kodi katika sekta ya madini, iwapo Serikali inanufaika.
Mdahalo huu ni mwendelezo wa maadhimisho ya miaka 40 ya chuo hiki na pia utahusisha shule mbalimbali za sekondari zilizopo hapa jijini.
Lakini pia tunataka kujua ukweli kuhusu Fao la Kujitoa iwapo linakubalika duniani na taratibu zake zipo vipi, hivyo tunaamini kupitia mdahalo huu tunaweza kupata majibu, alisema.
Fungo alisema kwamba pamoja na hayo, lakini pia mdahalo huo ni moja ya njia ya kuujulisha umma kupitia wanafunzi kuhusu msingi wa jambo hilo.
IFM ikiwa kama moja ya taasisi za elimu hapa nchini, imeona ni vema kutumia fursa hii kufikisha ujumbe kwa jamii kupitia midahalo tunayoiandaa kwa kuwashirikisha wanafunzi, alisema.
[h=4]Toa Maoni yako kwa habari hii[/h]
CHUO cha Usimamizi wa Fedha (IFM), kinatarajia kufanya mdahalo mkubwa Desemba 7, mwaka huu, kuhusu Fao la Kujitoa kwa wafanyakazi nchini. Hatu hiyo ni moja ya kutambua changamoto mbalimbali zinazolikabili Taifa kwa kuchambua mada mbalimbali zinazohusu jamii.
Akizungumza na MTANZANIA, Dar es Salaam jana, Mhadhiri Msaidizi wa Sheria za Biashara chuoni hapo, Agustus Fungo, alisema mdahalo huo utajikita kujadili masuala mbalimbali.
Fungo alisema mdahalo huo utaangazia Sera ya Hifadhi ya Jamii, sheria za mfuko, nadharia ya hifadhi ya jamii na hali halisi ya maisha ya Watanzania kwa sasa.
Fungo alisema mdahalo huo unatarajiwa kuongozwa na Mkufunzi Mkuu wa Chuo cha Takwimu cha Afrika Mashariki (EASTC,) Camillus Kassala.
Alisema mada nyingine zitakazojadiliwa ni pamoja na ulipaji wa kodi katika sekta ya madini, iwapo Serikali inanufaika.
Mdahalo huu ni mwendelezo wa maadhimisho ya miaka 40 ya chuo hiki na pia utahusisha shule mbalimbali za sekondari zilizopo hapa jijini.
Lakini pia tunataka kujua ukweli kuhusu Fao la Kujitoa iwapo linakubalika duniani na taratibu zake zipo vipi, hivyo tunaamini kupitia mdahalo huu tunaweza kupata majibu, alisema.
Fungo alisema kwamba pamoja na hayo, lakini pia mdahalo huo ni moja ya njia ya kuujulisha umma kupitia wanafunzi kuhusu msingi wa jambo hilo.
IFM ikiwa kama moja ya taasisi za elimu hapa nchini, imeona ni vema kutumia fursa hii kufikisha ujumbe kwa jamii kupitia midahalo tunayoiandaa kwa kuwashirikisha wanafunzi, alisema.
[h=4]Toa Maoni yako kwa habari hii[/h]