GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,546
- 108,876
Hapana hata kidogo Mimi ni mwana CCM na wala sioni Aibu kujiweka hivi wazi ila nimevumilia huu Upuuzi na sasa nasema wazi kabisa sipendezwi na hii tabia ya kila mara Wapinzani wakitaka kufanya Mikutano yao Polisi wanawazuia kwa Kigezo cha Usalama.
Hii hali haina Afya kwa CCM na kama kweli CCM inataka Kuwa Imara basi ikubali Changamoto. Inaboa na inakera kama si kuudhi pia. Hivi ni Mikutano tu ya Wapinzani nchini ndiyo huwa ina Visharia vibaya vya Usalama ila yetu Sisi wana CCM ndiyo huwa iko Shwari?
Hebu na Sisi wana CCM ifike muda basi tuone Aibu na tumuogope Mwenyezi Mungu kwani hiki kinachofanywa na Polisi ambacho nashawishika kusema kuwa kina baraka kutoka CCM Kwetu si kitendo cha Hekima na Busara na sidhani kama hata Chama chetu Kitabarikiwa kwa Upuuzi huu wa Kiuonevu dhdi ya Wapinzani nchini.
Kwani kama Sisi CCM tunajiamini kuwa tupo vyema katika Kuwaletea Maendeleo Watanzania hivi Wapinzani wakipita Kutusema vibaya huku na kule Sisi tutaathirika na nini hadi tuanze Kuwazuia na Kuwasumbua kila Uchao kana kwamba Wao siyo Watanzania na hawana Haki ya Kufanya Siasa zao hapa nchini?
Na hakuna Jambo lililonikera kama kusikia kuwa kuna Chama Kimoja ( nadhani ni CHADEMA ) walikuwa wamepanga Kufanya Dua / Maombi huko Mkoani Morogoro hasa ya Kuwaombea Marehemu wa ile Ajali mbaya ya Moto wa Petroli na cha Kushangaza Polisi wamewazuia kwa sababu ambazo hazina Miguu wala Kichwa na siogopi Kusema wazi hapa kuwa ni sababu za Kipumbavu na narudia tena kusema kuwa ni sababu za Kipumbavu ( mkinuna nuneni tu hadi mpasuke )
Kinachoniuma zaidi ni kuona wana CCM wengi wakinyamaza katika hili na kuona kuwa ni Jambo jema kabisa wakati katika Medani za Siasa na Demokrasia wala halina Afya na Ustawi mwema kwa nchi yetu kwa Siku za baadae kwani linazidi Kuzalisha Uadui na Chuki Kubwa baina ya Watanzania ambayo inaweza hata Kuathiri Usalama wetu kwa Siku zijazo.
Namalizia kwa Kusema Polisi Tanzania na Mamlaka za Kiuongozi acheni kuwaonea, kuwasumbua na kuwanyanyasa mno Wapinzania na waacheni tu wafanye Siasa zao ila nyie wapeni tu Ulinzi kama Jukumu lenu Mama na Kazi ya kujua kuwa Wao ni Waongo au Wafitini au Wachochezi mtuachie Sisi Wananchi.
Tunaposema kuwa tunamuenzi Hayati Baba wa Taifa Nyerere basi tuhakikishe tunamuenzi Kiukweli na Kuyaiga yale mema aliyokuwa akipenda Kuyafanya. Nyerere hakupenda Visasi, Nyerere hakupenda Kutengeneza Maadui, Nyerere hakupenda Kusifiwa, Nyerere hakupenda Unafiki, Nyerere hakupenda Uwongo, Nyerere hakupenda Dharau bali alipenda mno Kusikilizana na Kuheshimiana. Mambo yenu mengine mnayoyafanya sasa mnatufanya kila mara tuwe tunamkumbuka huyu Mzee na kuanza Kumlilia kwani huenda angekuwepo hai angewakemeeni na mngemuelewa.
Kuna vitu hata kama Wewe ni mwana CCM ila vinaudhi, vinakera na havivumiliki. Nipo tayari Kuchukiwa kwa huu Uzi ila najua mbele ya Mwenyezi Mungu nimesema ukweli wangu Kwenu na huenda wakati nyie mtanichukia Mimi An Eagle kwa haya niliyoyasema hapa ila kwa Mungu ataniongezea Baraka kadhaa kwakuwa Yeye hutupenda mno Watu wawazi na wakweli kama Mimi na Wana CCM wenzangu baadhi tunaojitambua.
Hii hali haina Afya kwa CCM na kama kweli CCM inataka Kuwa Imara basi ikubali Changamoto. Inaboa na inakera kama si kuudhi pia. Hivi ni Mikutano tu ya Wapinzani nchini ndiyo huwa ina Visharia vibaya vya Usalama ila yetu Sisi wana CCM ndiyo huwa iko Shwari?
Hebu na Sisi wana CCM ifike muda basi tuone Aibu na tumuogope Mwenyezi Mungu kwani hiki kinachofanywa na Polisi ambacho nashawishika kusema kuwa kina baraka kutoka CCM Kwetu si kitendo cha Hekima na Busara na sidhani kama hata Chama chetu Kitabarikiwa kwa Upuuzi huu wa Kiuonevu dhdi ya Wapinzani nchini.
Kwani kama Sisi CCM tunajiamini kuwa tupo vyema katika Kuwaletea Maendeleo Watanzania hivi Wapinzani wakipita Kutusema vibaya huku na kule Sisi tutaathirika na nini hadi tuanze Kuwazuia na Kuwasumbua kila Uchao kana kwamba Wao siyo Watanzania na hawana Haki ya Kufanya Siasa zao hapa nchini?
Na hakuna Jambo lililonikera kama kusikia kuwa kuna Chama Kimoja ( nadhani ni CHADEMA ) walikuwa wamepanga Kufanya Dua / Maombi huko Mkoani Morogoro hasa ya Kuwaombea Marehemu wa ile Ajali mbaya ya Moto wa Petroli na cha Kushangaza Polisi wamewazuia kwa sababu ambazo hazina Miguu wala Kichwa na siogopi Kusema wazi hapa kuwa ni sababu za Kipumbavu na narudia tena kusema kuwa ni sababu za Kipumbavu ( mkinuna nuneni tu hadi mpasuke )
Kinachoniuma zaidi ni kuona wana CCM wengi wakinyamaza katika hili na kuona kuwa ni Jambo jema kabisa wakati katika Medani za Siasa na Demokrasia wala halina Afya na Ustawi mwema kwa nchi yetu kwa Siku za baadae kwani linazidi Kuzalisha Uadui na Chuki Kubwa baina ya Watanzania ambayo inaweza hata Kuathiri Usalama wetu kwa Siku zijazo.
Namalizia kwa Kusema Polisi Tanzania na Mamlaka za Kiuongozi acheni kuwaonea, kuwasumbua na kuwanyanyasa mno Wapinzania na waacheni tu wafanye Siasa zao ila nyie wapeni tu Ulinzi kama Jukumu lenu Mama na Kazi ya kujua kuwa Wao ni Waongo au Wafitini au Wachochezi mtuachie Sisi Wananchi.
Tunaposema kuwa tunamuenzi Hayati Baba wa Taifa Nyerere basi tuhakikishe tunamuenzi Kiukweli na Kuyaiga yale mema aliyokuwa akipenda Kuyafanya. Nyerere hakupenda Visasi, Nyerere hakupenda Kutengeneza Maadui, Nyerere hakupenda Kusifiwa, Nyerere hakupenda Unafiki, Nyerere hakupenda Uwongo, Nyerere hakupenda Dharau bali alipenda mno Kusikilizana na Kuheshimiana. Mambo yenu mengine mnayoyafanya sasa mnatufanya kila mara tuwe tunamkumbuka huyu Mzee na kuanza Kumlilia kwani huenda angekuwepo hai angewakemeeni na mngemuelewa.
Kuna vitu hata kama Wewe ni mwana CCM ila vinaudhi, vinakera na havivumiliki. Nipo tayari Kuchukiwa kwa huu Uzi ila najua mbele ya Mwenyezi Mungu nimesema ukweli wangu Kwenu na huenda wakati nyie mtanichukia Mimi An Eagle kwa haya niliyoyasema hapa ila kwa Mungu ataniongezea Baraka kadhaa kwakuwa Yeye hutupenda mno Watu wawazi na wakweli kama Mimi na Wana CCM wenzangu baadhi tunaojitambua.