SNAP J
JF-Expert Member
- Dec 26, 2013
- 7,079
- 7,976
Kampuni moja ya ndege nchini Austria imezindua ruti mpya ya ndege inayofanya safari zake kati ya Uswisi na Ujerumani inayokatiza juu ya Ziwa Constance linalounganisha nchi hizo zinazopakana zilizopo barani Ulaya.
Ruti hiyo mpya inasemekana ndio ruti fupi kabisa ya kimataifa (international flight) duniani kwani muda ambao ndege kutoka St. Gallen-Altenrhen Airport nchini Uswisi hutumia hadi Friedrichshafen Airport Ujerumani ni dakika nane tu.
Safari hiyo ya ndege inayoenda na kugeuza kwa siku (twice-daily service) yenye kutumia dakika nane ni ya umbali wa kilomita 20 ambapo kama usafiri wa gari utatumika, basi dakika si nchini ya sitini zitatumika kulizunguka Ziwa Constance na hivyo kuonekana kuwa mkombozi kwa wasafiri wa nchini hizo jirani, na hasa wafanyabishara kwani gharama zake pia ni nafuu, yapata Uro 40 , sawasawa na dola 44 za Kimarekani.