James7
Senior Member
- Nov 2, 2010
- 120
- 80
Wanabodi,
John Pombe Magufuli ndiye Mahundi wa urais Tanzania kwa mwaka huu wa 2015-2025!, Kuna walioshindana naye, waliopingana nae, na waliopingana nae!. Kuna msemo usemao, "if you can't beat them, join them!".
Maria wito kwa wote walioshindana nae, kwanza kukubali matokeo, Pili kumpatia ushirikiano kwa ku join him.
Wakati wa mchaka to wa kumpata mgombea wa CCM nilipandisha uzi huu, kuhusu baadhi ya wagombea wa CCM wakipita wana hatari ya ku make the worst Dictators, John Pombe Magufuli was number 2 ya Rais who can make the worst dictator this country has ever had!.
Hoja kuwa Magufuli ni dictator haina mjadala, kitu cha muhimu ni kumuombea tuu kwa Mungu, angalau amfanye ni a benevolent one, vinginevyo tutajuta!.
Jakaya Kikwete ukiondoa mambo yake ya Kikwete ya uswahili Swahili, alikuja ni mtu mwenye huruma iliyooitiliza kiasi cha kutafsiriwa ni Rais dhaifu, hivyo CCM ya Kikwete ilikuwa ni CCM dhaifu!, CCM ya Magufuli itakuwa ni CCM sasa kazi tuu, ambayo ni hatari kwa waliozoea CCM lege lege, hivyo akijenga CCM imara sana, huu upinzani mwisho ni 2020!.
JK tumemchekea, tumemdhihaki, tumembeza, tumemkejeli, hadi kumchezea, yeye akicheka tuu na kuwaacha yapite. Kwa Magufuli, hakuna kucheka, wala hakuna mchezo, ni kazi tuu, hivyo hili ni angalizo muhimu sana na hata majaaliwa ya huu Uhuru tulionao humu jf mbele ya unpredictable dictator, ni mashaka matupu unless we join them!.
Thanks God, mimi ni mmoja wa wachache, wanaojua huyu Magufuli aliibukia wapi hadi yeye kuwa ndie mgombea wa CCM na sababu ni zipi!. Hivyo let's hope, only zile sababu, zilizopelekea kwa nini ni Magufuli, ndio the only ones zitakazo mcheck and balance him in between being a real dictator and a benevolent dictator, so to be on a safe side, if you can't beat them, just join them!.
Wana Chadema, Wana UKAWA na Watanzania wenzangu, najua wengi wetu tulimtaka Lowassa, tumemkosa!, tukapewa Magufuli, let's just take him!. If you can't get what you want, just take what you get!.
Sio tumjoin kwa sababu ndio tumemkubali, au kwa sababu ndio sasa tunampenda, no way, we have to join them because we have to!.
Pasco!.
Andika vizuri.