Idrisa abadili mawazo. Hatojiuzulu tena

M

MegaPyne

Guest
Kwa habari nilizozipata sasa hivyi zinasema Meneja mkuu wa Tanesco Dr. Rashid Idrisa kabadili msimamo wake na kwamba hata jiuzulu tena.

Habari zaidi zitawajia baadaye

Stay tuned!
 
Kwa habari nilizozipata sasa hivyi zinasema Meneja mkuu wa Tanesco Dr. Rashid Idrisa kabadili msimamo wake na kwamba hata jiuzulu tena.

Habari zaidi zitawajia baadaye

Stay tuned!

..indeed, we'll stay tuned! Thanks for being prompt, simply GREAT WORK!

SteveD.
 
Confirmed, TvT wametangaza dakika 10 zilizopita, huyu bwana ame-withrdraw resignation yake.

Inaelekea alikuwa anatikisa kiberiti akakuta kimejaa!
 
Confirmed, TvT wametangaza dakika 10 zilizopita, huyu bwana ame-withrdraw resignation yake.

Inaelekea alikuwa anatikisa kiberiti akakuta kimejaa!

Duuh, hii misemo mingine inaniacha hoi ndugu zangu, Kakalende wako hapo juu ni mtamu haswaaa....nimeupenda, naomba ruhusa kuutumia tu pahala pengine. :)

You better love it more. This ain't a Joke. its True!

CMB, I do and I do!!

SteveD.
 
Hii habari ilijulikana tangu jana, na kama nilivyosema kwenye ile post ya kujiuzulu, kati ya vitu ambavyo CCM haihitaji sasa hivi ni kujiuzulu kwa senior official hasa baada ya kupata ujiko wa Kamati na wimbi limegeuka na sasa pressure ilikuwa iwe kwa wapinzani; sasa kujiuzulu kwa Idris kungekuwa ni distraction ambayo CCM haiwezi kuimudu wakati huu kwani mambo yanawaendea vizuri..
 
Inaonekana Muungwana hakukubaliana na Habari Nzima ya Kujiuzulu kwa Dr.Rashid.Kuna ukweli na Ushahidi wa Barua ya Kuomba Kujiuzulu kwa Dr.Rashid(Baadhi ya vyombo vya habari vina nakala).Kitendo cha kutengua Maamuzi yake hayo bila shaka ni Ushauri kutoka kwa Mkuu wa Nchi,na wala Sio Waziri Karamagi ambaye pia anatofautiana sana kimsimamo na Dr.Rashid.

Bodi ya Wakurugenzi wa Tanesco inakutana tena kujadili suala zima la Dr.Rashid na wadeni sugu wa Tanesco (Ikiwamo Serikali ya Mapinduzi).Kuna kila Dalili kuwa Balozi Fulgence Kazaura atakuwa ktk wakati Mgumu,na pengine ndio itakuwa mwisho wake ktk Utumishi wa Bodi hiyo.Kuna makundi makubwa ndani ya Tanesco ambayo nayo yamekuwa kikwazo katika kuikwamua Tanesco ktk Ukwasi Mkubwa!!!Drama hii ndio kwanza imeanza kuna mengi yatafurumuka hapo,na Ikizingatiwa kuwa Tume ya Bunge ipo Tanesco kufuatilia mambo ya Richmond.
 
Bongo bwana....mambo kama haya wala raisi hakutakiwa kuhusika nayo kabisa unless ni dharura ya kitaifa..
 
Hii habari ilijulikana tangu jana, na kama nilivyosema kwenye ile post ya kujiuzulu, kati ya vitu ambavyo CCM haihitaji sasa hivi ni kujiuzulu kwa senior official hasa baada ya kupata ujiko wa Kamati na wimbi limegeuka na sasa pressure ilikuwa iwe kwa wapinzani; sasa kujiuzulu kwa Idris kungekuwa ni distraction ambayo CCM haiwezi kuimudu wakati huu kwani mambo yanawaendea vizuri..

kama ulijua kwa nini usingesema ! halafu mbona unaweka siasa katika kila kitu wewe ! its boring meeeeeeeen !
 
Mzee Mwenzangu Nyani.. kinachotokea ni political angle yake; Ingekuwa nchi nyingine wataalam washughulikie matatizo bila kuweka siasa zitaathirika vipi. Nyumbani bado somo hilo halijaiva; hata hivyo siwezi kushangaa kuwa barua ya kujiuzulu iwe imeandikwa na mtu mwingine baada ya Dr. Idris kutishia kujiuzulu.. Lengo likiwa ni kumpiku
 
hivi wapi inaonyesha rais amemshauri jamaa asijiuzulu wazee au wapi kunaonyesha rais ameweka mkono wake ? and plzzzzzzzzzz dont talk about speculations maana najua mnazo nyingi tena sana !
 
Bongo bwana....mambo kama haya wala raisi hakutakiwa kuhusika nayo kabisa unless ni dharura ya kitaifa..

Ngabu, kwa mazingira ya nchi yetu na historia yake hii ni dharura bwana. Ulishawahi kusikia kiongozi gani katika kipindi cha miaka mitano iliyopita amejiuzulu Tanzania?... lakini angalia habari kutoka huko nchi za Ulaya magharibi na Amerika, kila leo hii unasikia waziri fulani amejiuzulu, meneja ameachia ngazi, huyu au yule kastaafishwa kabla ya muda wake... n.k.

Basi kwa tukio kama hili la mara moja katika kizazi, wala sitashangaa kuona Rais amejitumbukiza kwenye issue jumla jumla, maanake hata yeye mwenyewe anashangaa.. kumbe nchi hii siyo kila mtu mfuata mkumbo.. unless, kama Kakalende alivyosema hapo awali kuwa, Mkurugenzi 'katikisa box la kiberiti na kukuta limejaa'...yetu macho na masikio kwa sasa, but as always the truth prevail.

SteveD.
 
kama ulijua kwa nini usingesema ! halafu mbona unaweka siasa katika kila kitu wewe ! its boring meeeeeeeen !

sikujua kama ataghairi, sasa wakati mwingine uwe unasoma basi; halafu siasa bahati mbaya huwezi kuiondoa hasa kama unakumbuka maana ya "siasa" ni nini.? Bahati mbaya siasa ipo katika kila kitu kinachomzunguka mwananchi.. sasa kama hukuchukua somo la siasa au ndio masomo yaliyokushinda sidhani kama naweza kukusaidia ndugu yangu. Siasa iko katika kila kitu...
 
hivi wapi inaonyesha rais amemshauri jamaa asijiuzulu wazee au wapi kunaonyesha rais ameweka mkono wake ? and plzzzzzzzzzz dont talk about speculations maana najua mnazo nyingi tena sana !

wapi panaposema Rais hajafanya hivyo na sisi speculation hatuhitaji kwani unazo nyingi...
 
wakuu..jamaa aliandika barua ya kusudio la kujiuzulu..ila hali ilivyo ni kuwa serikali kwa sasa inakabiliana na hali ya kuchafuka kwa siasa..kutokana na masuala ya madini,perfomance ndogo ya serikali ya jk,tume ya richmond ..ets
kwa kifupi ingekuwa pigo sana na imebidi serikali ifanye juhudi zote jamaa abakie..[labda wanangojea right time kwa yeye ku exit] au watamuandalia ajali ya kikazi aondoke kwa kashfa..
jambo lingine ni kuwa TANESCO ni chaka la ufujaji la vigogo...kuanzia richmond hadi IPTL....ukipata wasaa wa kuongea na mtu wa ndani pale namna watu wakubwa wanavyofuja pesa za TANESCO Na kuongeza bei kwenye mikataba ..unaweza ukalia UTALIONA SAKATA LA BOT NI CHAMTOTO....INASIKITISHA SANA...
 
Mie kwa mtazamo wangu...kaambiwa hali Hairuhusu..kwani mtu anapojiuzulu huwa anaomba ajiuzulu kwa mtu aliempa madaraka, obvious aliempa madaraka ni RAIS..so Rais bado ana mamlaka ya kukubali ua kukataa au kukaa nae mezan kujadili zaid...
 
kwa Tanzania yetu yote yanawezekana! 'no coordination at all'!! Waziri husika anakuja na hili, mkuu wa Kaya anawaza yale alimradi kunakucha twende tu!

Wasi wasi wangu sijui tutafika salama?
 
wapi panaposema Rais hajafanya hivyo na sisi speculation hatuhitaji kwani unazo nyingi...

wanaposhindwa huleta vioja ! nimekuuliza na ww unauliza wapi na wapi kunguru kunyea manati mzee ? jibu kwanza. kama huwezi lets keep it moving lakini sio kusema kila kitu rais hivi rais vile hadi saa nyingine inakuwa tooo much yaani ni sawa na kusema huyo rais anafanya toooo much skendos zaidi ya kazi iliyomuweka pale KITU AMBACHO SI KWELI !!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom