swan
Senior Member
- Oct 11, 2012
- 132
- 356
Hivi kuicheka picha ya rais ni kitu kimoja na kumcheka rais??
rejea kisa cha Abunuwas na mlio wa punda
SIKU moja abunuwas alipata dinari zake mia. Akaenda sokoni akanunua punda mzuri, akampanda. Akaenda naye mpaka nyumbani kwake. Hata siku moja akaja mtu kuazima punda wake Abunuwas. Abunuwas akanena, Punda hayuko. Mara Yule punda akalia. Yule mtu akanena, punda si huyo analia, na wewe wasema hayuko? Abunuwas akajibu, sasa wewe umekuja kuazima punda ama umekuja kuazima mlio? Kama umekuja kuazima mlio na mimi nitalia. Abunuwas akalia, Ho! Ho! Ho! Akamwambia, haya panda uende zako.
rejea kisa cha Abunuwas na mlio wa punda
SIKU moja abunuwas alipata dinari zake mia. Akaenda sokoni akanunua punda mzuri, akampanda. Akaenda naye mpaka nyumbani kwake. Hata siku moja akaja mtu kuazima punda wake Abunuwas. Abunuwas akanena, Punda hayuko. Mara Yule punda akalia. Yule mtu akanena, punda si huyo analia, na wewe wasema hayuko? Abunuwas akajibu, sasa wewe umekuja kuazima punda ama umekuja kuazima mlio? Kama umekuja kuazima mlio na mimi nitalia. Abunuwas akalia, Ho! Ho! Ho! Akamwambia, haya panda uende zako.