Idhini ya Rais peke yake haitoshi kupata Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi

DaudiAiko

JF-Expert Member
Dec 2, 2012
302
274
Wanabodi,

Kabla ya yote, tukubaliane kwamba wana CHADEMA ndio wanaojitoa muwanga katika sakata hili la kudai katiba mpya na tume huru ya uchaguzi

Nina amini kwamba kila tatizo lina umuhimu wa kutafutiwa suluhisho. Vile vile katika kukosoa, kuna umuhimu sana wa kuwa na ukosoaji unaojenga na sio ukosoaji unaodhalilisha bila kuleta manufaa yoyote. Ukosoaji huu unahitaji sana kitu kinachoitwa "Open-mindedness" ili kuruhusu majadiliano yenye tija na yenye kuwezesha upatikanaji wa suluhisho mbali mbali. Mengi yanaendelea katika sakata hili la kudai tume huru na katiba mpya lakini swali la kujiuliza ni kama juhudi za wana CHADEMA kufanya mikutano ya hadhara na makongamano yana nguvu za kutosha kuwafikia walengwa. Kitu ninachokiona kwa wana CHADEMA ni kwamba wana amini kabisa kwamba mabadiliko ya katiba na tume ya uchaguzi yanahitaji maamuzi ya mtu mmoja tu iliku idhinisha. Wana kubali kabisa kwamba Rais Samia peke yake, anatosha kubadilisha hali ya siasa nchini kwa kutia saini makubaliano ya kubadilisha katiba na tume ya uchaguzi.

Kama miradi ya kimakakati ya serikali ilivyo, lazima kuwe na sababu iliyofanyiwa tafiti kwa muda mrefu mpaka kufikia hatua ya kuwa na uhakika na kutekeleza miradi hiyo. Wana CHADEMA wanaweza wakawa wana fahamu hilo lakini wana amini kabisa kwamba hawawezi kupata madai yao kwa amani na kwasababu hiyo kutafuta haki barabarani. Sio sahihi kumlaumu Rais kwa kila kitu kisichokuwa sawa kwenye siasa zetu vile vile ni vyema kwa wana CHADEMA kupeleka mfano wa katiba wanayo pendekeza pamoja na mapendekezo yao ya tume huru kwa wahusika kwanza. Ni muhimu kuwa na viongozi ambao wako tayari kusikiliza maoni ya wengine kuhusu kitu chochote hata kama hawakubaliani nao...

Mungu ni mwema, wakati wote
 
Mkuu mada yako imekuwa na ukakasi kwa sababu hizi:

1. Suala la katiba mpya si geni.
2. Mchakato wa katiba mpya ulianza kwenye awamu ya nne.
3. Maoni ya watu yalikwisha kusanywa nchi nzima, ikatengenezwa katiba ya Warioba.
4. Bunge la katiba likaundwa ikazaliwa katiba pendekezwa.
5. Hatua zote nne hizi zilikwisha wagharimu watanzania mabilioni ya pesa.
6. Wananchi wanastahili kupata katiba yao ikizingatiwa mapungufu mengi yaliyomo kwenye iliyopo.
7. Chadema kama sehemu ya wananchi wanahitaji katiba mpya iliyo bora zaidi.
8. Kiungwana kwa niaba ya wananchi Chadema wamekuwa wakiomba kujua ratiba ya kuanzishwa kwa mchakato wa katiba mpya uliokuwa umekwama.
9. Katika kujua ratiba ya kurejelewa kwa mchakato huo wamependekeza uchaguzi ujao kufanyika, kama si ndani ya katiba mpya uwe ndani ya tume huru ya uchaguzi kama ilivyo katika katiba mpya.
10. Ni nia ya CCM na hasa Samia na washirika zake kuendelea kutokuwa na tume huru ya uchaguzi kwa angalau hadi 2030 kwa maslahi yao binafsi.

Kuna mtu wa kulaumiwa kwenye kadhia hii.

Kwanini Samia anakomalia katiba yenye tume ya uchaguzi, mahakama na bunge vinavyoegemea kwake kuendelea bila ukomo?

Majibu yako wazi:

Katiba Mpya: Kwanini CCM hawataridhia kirahisi

Labda hapa cha kuangalia ilikuwa kumbaini mwenye kumfunga paka kengele.
 
Usizunguke sana, tatizo ni CCM ndio maana katiba mpya hatuna mpaka leo, wanajisumbua tuu maana INAKUJA na ndio utakuwa mwisho wao wa kutawala kwa wizi wa kura na kukandamiza wapinzani
 
Mkuu mada yako imekuwa na ukakasi kwa sababu hizi:

1. Suala la katiba mpya si geni.
2. Mchakato wa katiba mpya ulianza kwenye awamu ya nne.
3. Maoni ya watu yalikwisha kusanywa nchi nzima, ikatengenezwa katiba ya Warioba.
4. Bunge la katiba likaundwa ikazaliwa katiba pendekezwa.
5. Hatua zote nne hizi zilikwisha wagharimu watanzania mabilioni ya pesa.
6. Wananchi wanastahili kupata katiba yao ikizingatiwa mapungufu mengi yaliyomo kwenye iliyopo.
7. Chadema kama sehemu ya wananchi wanahitaji katiba mpya iliyo bora zaidi.
8. Kiungwana kwa niaba ya wananchi Chadema wamekuwa wakiomba kujua ratiba ya kuanzishwa kwa mchakato wa katiba mpya uliokuwa umekwama.
9. Katika kujua ratiba ya kurejelewa kwa mchakato huo wamependekeza uchaguzi ujao kufanyika, kama si ndani ya katiba mpya uwe ndani ya tume huru ya uchaguzi kama ilivyo katika katiba mpya.
10. Ni nia ya CCM na hasa Samia na washirika zake kuendelea kutokuwa na tume huru ya uchaguzi kwa angalau hadi 2030 kwa maslahi yao binafsi.

Kuna mtu wa kulaumiwa kwenye kadhia hii.

Kwanini Samia anakomalia katiba yenye tume ya uchaguzi, mahakama na bunge vinavyoegemea kwake kuendelea bila ukomo?

Majibu yako wazi:

Katiba Mpya: Kwanini CCM hawataridhia kirahisi

Labda hapa cha kuangalia ilikuwa kumbaini mwenye kumfunga paka kengele.
Yote uliyo eleza ni muonekano mzuri wa yale yanayo endelea ila wana CHADEMA wanahisi kwamba kupaza sauti pamoja maandamano ya hapa na pale yanatosha kuwafanya viongozi serikalini kupitisha mchakato wa katiba mpya. Huu ndio wakati kwa wana CHADEMA kueleza kwa undani kuhusu katiba wanayo pendekeza pamoja na tume huru inayo pendekezwa
 
Yote uliyo eleza ni muonekano mzuri wa yale yanayo endelea ila wana CHADEMA wanahisi kwamba kupaza sauti pamoja maandamano ya hapa na pale yanatosha kuwafanya viongozi serikalini kupitisha mchakato wa katiba mpya. Huu ndio wakati kwa wana CHADEMA kueleza kwa undani kuhusu katiba wanayo pendekeza pamoja na tume huru inayo pendekezwa

Kama nilivyo eleza yote yamo kwenye rejea:

1. Katiba ya Warioba
2. Katiba pendekezwa

Kinachotakiwa ni tarehe ya kuurejelea sehemu ya mchakato uliobakia ili katiba pendekezwa iuzwe kwa wananchi, ipitishwe au la.

Mengine hapo kati kati ya tume itakayo simamia hiyo yameelezwa mno.
 
Mkuu mada yako imekuwa na ukakasi kwa sababu hizi:

1. Suala la katiba mpya si geni.
2. Mchakato wa katiba mpya ulianza kwenye awamu ya nne.
3. Maoni ya watu yalikwisha kusanywa nchi nzima, ikatengenezwa katiba ya Warioba.
4. Bunge la katiba likaundwa ikazaliwa katiba pendekezwa.
5. Hatua zote nne hizi zilikwisha wagharimu watanzania mabilioni ya pesa.
6. Wananchi wanastahili kupata katiba yao ikizingatiwa mapungufu mengi yaliyomo kwenye iliyopo.
7. Chadema kama sehemu ya wananchi wanahitaji katiba mpya iliyo bora zaidi.
8. Kiungwana kwa niaba ya wananchi Chadema wamekuwa wakiomba kujua ratiba ya kuanzishwa kwa mchakato wa katiba mpya uliokuwa umekwama.
9. Katika kujua ratiba ya kurejelewa kwa mchakato huo wamependekeza uchaguzi ujao kufanyika, kama si ndani ya katiba mpya uwe ndani ya tume huru ya uchaguzi kama ilivyo katika katiba mpya.
10. Ni nia ya CCM na hasa Samia na washirika zake kuendelea kutokuwa na tume huru ya uchaguzi kwa angalau hadi 2030 kwa maslahi yao binafsi.

Kuna mtu wa kulaumiwa kwenye kadhia hii.

Kwanini Samia anakomalia katiba yenye tume ya uchaguzi, mahakama na bunge vinavyoegemea kwake kuendelea bila ukomo?

Majibu yako wazi:

Katiba Mpya: Kwanini CCM hawataridhia kirahisi

Labda hapa cha kuangalia ilikuwa kumbaini mwenye kumfunga paka kengele.
Mbona umeruka, liliitishwa bunge la katiba, rasimu wa warioba ijapigiwa kura kifungu kwa kifungu, hatimae tukapata katiba pendekezwa ambayo inasubiri KURA YA MAONI
 
Yote uliyo eleza ni muonekano mzuri wa yale yanayo endelea ila wana CHADEMA wanahisi kwamba kupaza sauti pamoja maandamano ya hapa na pale yanatosha kuwafanya viongozi serikalini kupitisha mchakato wa katiba mpya. Huu ndio wakati kwa wana CHADEMA kueleza kwa undani kuhusu katiba wanayo pendekeza pamoja na tume huru inayo pendekezwa
Sisi wanachadema, tunaamini wazee wa chama cha chadema wakuongozwa na mwenyekiti wa chama, mr mbowe, watatupatia tume huru ya uchaguzi na pia katiba mpya,
Hivyo kazi hiyo serikali ituachie sisichadema tuifanye kwa uadilifu na umakini mkubwa kwa faida ya vizazi vyetu
 
Mbona umeruka, liliitishwa bunge la katiba, rasimu wa warioba ijapigiwa kura kifungu kwa kifungu, hatimae tukapata katiba pendekezwa ambayo inasubiri KURA YA MAONI

Tuna mengi mkuu na kufuatilia pia mahakamani. Ukizingatia hapa wala siyo UE na achilia mbali utopolo m wingi wenye kukera.

Au nasema uongo ndugu yangu?
 
Back
Top Bottom