Idd Azan, mwanamume hasusi! Usiliachie jimbo la Kinondoni kwa sababu ya fitina za CCM

mbeyaman

Member
Sep 28, 2013
97
28
Utakuwa huwatendei haki wananchi wa jimbo la Kinondoni kutokana na uamuzi wako wa kutogombea tena ubunge jimbo la Kinondoni. Hao akina Tarimba, Madabida wanaoliwania jimbo la Kinondoni wasikunyime raha. Kuna msemo unasema ukisusa sisi twala.

Una kila sababu ya kugombea tena ubunge wa jimbo la Kinondoni katika uchaguzi mkuu wa 2015. Unatarajiwa kuwepo katika baraza la mawaziri la serikali itakayoundwa. Usiwe na jazba, umefanya maendeleo makubwa katika jimbo la Kinondoni.

Nimesikitika kusikia kwamba wana CCM hawa wenzako wakishirikiana na kijana wa usalama wa Taifa wakitumia vyombo vya habari kukuchafua ati unafanya biashara ya madawa ya kulevya. Walidiriki hata kutaka kukubambikia madawa nyumbani kwako, hii yote ni harakati za kukumaliza kisiasa. Lakini pamoja na hayo unatakiwa ujikaze kiume, usiyumbe.

Wanakuchafua ati pesa zako zinatokana na madawa ya kulevya. Sisi tuliokaribu na wewe tunajua jinsi ulivyohangaika kutafuta pesa kihalali kuanzia udereva wa taxi, mkopo wa kigari cha mizigo mpaka sasa unamiliki kampuni kubwa ya malori. Tunajua jinsi unavyofanya biashara ya kupeleka simenti Congo, Rwanda, Burundi, Uganda na nchi nyingine za Afrika. Hii hoja ya wewe kujihusisha na madawa inatokea wapi ?

Mchango wako kwa ajili ya maendeleo ya wana Kinondoni unahitajika. USIWATELEKEZE WANANCHI WA JIMBO LAKO KWA KUTOGOMBEA TENA UBUNGE. BADILI MSIMAMO WAKO.
 
Bila shaka. Masuala ya kihuni-huni yasikukatishe tamaa. Wengi wa hao wanaokutungia kashfa wana lao jambo. Hasidi mara zote sababu hana. Jitihada zako kwa maendeleo ya Jimbo la Kinondoni bado zinahitajika. Tafadhali durusi msimamo wako kuhusu kutogombea 2015.
 
Wewe ni mchepuko wake?maana Idd Azzan hata form 4 alifeli awe waziri
 
Usimjaze ujinga hana mchango wowote ama bungeni au jimboni,Tandale hawajawahi kumuona.Jimbo la CUF mwaka huu.
 
....duh,kweli tutasikia na kuona mengi kabla ya uchaguzi wa mwaka 2015,hasa kutoka kwa wazee wa Magamba,maana kila mtu anajiona yeye ndiye zaidi,mjanja,tajiri,maarufu,mtoto wa mjini kuliko mwingine kumbe ni uroho tu wa mali..yetu macho na masikio!
 
Utakuwa huwatendei haki wananchi wa jimbo la Kinondoni kutokana na uamuzi wako wa kutogombea tena ubunge jimbo la Kinondoni. Hao akina Tarimba, Madabida wanaoliwania jimbo la Kinondoni wasikunyime raha. Kuna msemo unasema ukisusa sisi twala.

Una kila sababu ya kugombea tena ubunge wa jimbo la Kinondoni katika uchaguzi mkuu wa 2015. Unatarajiwa kuwepo katika baraza la mawaziri la serikali itakayoundwa. Usiwe na jazba, umefanya maendeleo makubwa katika jimbo la Kinondoni.

Nimesikitika kusikia kwamba wana CCM hawa wenzako wakishirikiana na kijana wa usalama wa Taifa wakitumia vyombo vya habari kukuchafua ati unafanya biashara ya madawa ya kulevya. Walidiriki hata kutaka kukubambikia madawa nyumbani kwako, hii yote ni harakati za kukumaliza kisiasa. Lakini pamoja na hayo unatakiwa ujikaze kiume, usiyumbe.

Wanakuchafua ati pesa zako zinatokana na madawa ya kulevya. Sisi tuliokaribu na wewe tunajua jinsi ulivyohangaika kutafuta pesa kihalali kuanzia udereva wa taxi, mkopo wa kigari cha mizigo mpaka sasa unamiliki kampuni kubwa ya malori. Tunajua jinsi unavyofanya biashara ya kupeleka simenti Congo, Rwanda, Burundi, Uganda na nchi nyingine za Afrika. Hii hoja ya wewe kujihusisha na madawa inatokea wapi ?

Mchango wako kwa ajili ya maendeleo ya wana Kinondoni unahitajika. USIWATELEKEZE WANANCHI WA JIMBO LAKO KWA KUTOGOMBEA TENA UBUNGE. BADILI MSIMAMO WAKO.


Mbona maelezo haya ni kama vile ya mkewe? mfano "sisi tuliokaribu na wewe tunajua jinsi........." duhh!! kweli kuna mijitu mingine inapenda sana kugongwa.
 
Utakuwa huwatendei haki wananchi wa jimbo la Kinondoni kutokana na uamuzi wako wa kutogombea tena ubunge jimbo la Kinondoni. Hao akina Tarimba, Madabida wanaoliwania jimbo la Kinondoni wasikunyime raha. Kuna msemo unasema ukisusa sisi twala.

Una kila sababu ya kugombea tena ubunge wa jimbo la Kinondoni katika uchaguzi mkuu wa 2015. Unatarajiwa kuwepo katika baraza la mawaziri la serikali itakayoundwa. Usiwe na jazba, umefanya maendeleo makubwa katika jimbo la Kinondoni.

Nimesikitika kusikia kwamba wana CCM hawa wenzako wakishirikiana na kijana wa usalama wa Taifa wakitumia vyombo vya habari kukuchafua ati unafanya biashara ya madawa ya kulevya. Walidiriki hata kutaka kukubambikia madawa nyumbani kwako, hii yote ni harakati za kukumaliza kisiasa. Lakini pamoja na hayo unatakiwa ujikaze kiume, usiyumbe.

Wanakuchafua ati pesa zako zinatokana na madawa ya kulevya. Sisi tuliokaribu na wewe tunajua jinsi ulivyohangaika kutafuta pesa kihalali kuanzia udereva wa taxi, mkopo wa kigari cha mizigo mpaka sasa unamiliki kampuni kubwa ya malori. Tunajua jinsi unavyofanya biashara ya kupeleka simenti Congo, Rwanda, Burundi, Uganda na nchi nyingine za Afrika. Hii hoja ya wewe kujihusisha na madawa inatokea wapi ?

Mchango wako kwa ajili ya maendeleo ya wana Kinondoni unahitajika. USIWATELEKEZE WANANCHI WA JIMBO LAKO KWA KUTOGOMBEA TENA UBUNGE. BADILI MSIMAMO WAKO.

Wewe utakuwa ni Idd Azan mwenyewe unajipigia chapuo watoto wa mjini wanasrma.kama unamjua vizuri toka anaendesha tax mfuate kwake kamueleze sio unatuletea matangazo humu Jukwaani sisi watu wa Kinondoni hatujamtuma mtu.huo ugomvi wao hautuhusu Mkuu hili ni jukwaa la ma GT hizo habari za umbeya mpelekee kwake hazituhusu Mkuu
 
Punda waliofungwa china ndio waliomtaja IDD AZAN kwamba ni zungu la unga, sasa kama wafungwa hao wanaweza kumsingizia mtu hiyo ni shauri ingine, Ila huyo Tarimba Abbas hana mvuto wa kisiasa ni mnafiki,kwenye uchaguzi wa NEC uliopita kabla ya huu uliopo alikuwa wa mwisho,hana lolote chotara huyu
 
Atakuwa amepima upepo na kuona moto wa Ukawa utambabua hasa baada yakuona mwenzake alivyojisalimisha chini ya daraja jana!
 
Nyambafu kabisa huyu si ndiye lile 'zungu la unga' aka poda aliye taja na wafungwa (mapunda) wa Ki-TZ waliopo kwenye magereza ya china/hong kong ambaye kila kikicha anaongeza idadi ya matejaa hapa bongo,

Tena akafie mbele ya mbele ya safari kabla ya 'uprising' haijachukua mkondo wake
 
Hivi jamaa alishindwa timu ya mpira ataweza Ubunge ? Kino harudi tena yule muda ndio utakaosema.
 
Hivi Kinondoni kumbe ina mbunge? Ndio nimejuwa leo.

Huwa anashriki bunge hili hili au haruhusiwi kuongea bungeni?
 
Back
Top Bottom