PakaJimmy
JF-Expert Member
- Apr 29, 2009
- 16,203
- 8,720
Mr. Amin is carried by four British businessmen during a party for diplomats in 1975. A Swedish businessman holds an umbrella in the manner of servants who once shielded tribal rulers from the sun.
Charles Arube:
Huyu alikuwa mmoja kati ya Makamanda wa ngazi za juu kabisa wa jeshi la Idd Amin Dadda, mtu wa kabila lake Amin liitwalo Kakwa, akitumikia nafasi ya Mkuu wa Majeshi, huku akiwa na cheo cha Ubrigadia Jenerali.
Arube,akiwa mkristo, alichukizwa sana na kasi ya uondolewaji wa wanajeshi wa jamii na kabila za Waacholi, Langi na wengineo wa dini ya Kikiristo jeshini, na nafasi zao kuchukuliwa na watu wa makabila mengine, mpango ambao ulikuwa ukibuniwa na mtukufu rais, Amin, aliyejiita Big Daddy.
Inasemekana huyu jamaa kwa kutumia nafasi yake hiyo alipanga mapinduzi kumng'oa Amin, lakini baada ya intelijenisia ya Amin kuhisi jambo hilo, huyu jamaa alipelekwa kwenye mafunzo huko Jamhuri ya Soviet,na aliporudi alikuta Askari wa kukodiwa(mercenary) wa Kisudani aliyekuwa rafiki yake Amin ameshapewa nafasi yake ya Ukuu wa Majeshi, jambo ambalo lilimzidishia hasira.
Arube aliunda kwa siri kikosi cha mauajia ambacho kilikuwa kimvamie Amin nyumbani kwake, Kokolo Hill huko Kampala.
Usiku wa manane, kikosi hiki kiliwasili nyumbani kwa Amin na kwa mshangao walimkosa, hakuwepo!
Matokeo yake, Arube alizingirwa na askari wa Amin na kupigwa risasi, akafa.
Amin alipoambiwa jambo hilo alienda moja kwa moja mochwari kutazama na kuhakikisha kama kweli huyu mtu alikuwa maiti, na alipofika kwenye chumba hicho aliwafukuza nje waganga wote na wahudumu wa mochwari, akabaki na maiti hiyo peke yake kwa zaidi ya dakika ishirini, akiwa amejifungia makomeo, na hadi leo haijajulikana alikuwa anafanya nini huko chumbani na maiti ile!..Alipotoka aliingia kwenye gari na kuondoka!