Idara ya elimu wilaya ya Kwimba imewataka walimu kutoa mitihani kila wiki kwa Darasa la iv na vii kipindi hiki cha COVID-19

ndiga

JF-Expert Member
Jan 28, 2014
582
592
WanaJF salaam,

Binafsi ninashukuru jitihada zilizochukuliwa na serikali katika suala zima la kudhibiti kuenea kwa ugonjwa huu wa corona ikiwa ni pamoja na kufunga shule zote za msingi sekondari na vyuo.

Ni kweli kuwa hawa wanafunzi wanatakiwa waendelee kujifunza wakiwa majumbani kwao lakini siyo kwa njia ambayo imependekezwa na idara ya elimu wilaya ya Kwimba.

Idara ya elimu Kwimba imezitaka shule zote za msingi kutunga mitihani kwa drs la nne na drs la saba kila wiki na kisha kuwapa wanafunzi wa madarasa hayo kupitia kwa w/viti wa vitongoji/ serikali za mitaa .

Baada ya kufanya mitihani hiyo wairudishe kwa walimu kwa ajili ya kusahihisha na kupanga matokeo yatakayokuwa yanatumwa wilayani kila wiki .

Je, hawa watu wamejipanga kupambana na corona au wanampango wa kuwatoa kafara hawa walimu watakaokuwa wanasahihisha hizi karatasi za mitihani na masikini hawa wenyeviti wa vitongoji wa serikali za mitaa wasio na posho za kusambazia mitihani hiyo kwa kila mwanafunzi wa drs iv na vii huku wakijiweka katika mazingira ya kupata corona.

Nawasilisha.
 
Huo ndio mfumo wanaotumia shule binafsi nyingj kwasasa ni hatari sana wanaisambaza corona bila kujua
 
Kwa hiyo Hilo tu ndio mmeliona linasambaza corona
Je, kuhusu kuruhusu ibada kuendelea
Je, kuhusu Shughuli na mikusanyiko masokini kuendelea
Je, kuhusu movement kuruhusiwa kuendelea
Kwa hyo muangalie na hizo sehemu maana corona haichagui wanafunzi tu
 
WanaJF salaam,

Binafsi ninashukuru jitihada zilizochukuliwa na serikali katika suala zima la kudhibiti kuenea kwa ugonjwa huu wa corona ikiwa ni pamoja na kufunga shule zote za msingi sekondari na vyuo.

Ni kweli kuwa hawa wanafunzi wanatakiwa waendelee kujifunza wakiwa majumbani kwao lakini siyo kwa njia ambayo imependekezwa na idara ya elimu wilaya ya Kwimba.

Idara ya elimu Kwimba imezitaka shule zote za msingi kutunga mitihani kwa drs la nne na drs la saba kila wiki na kisha kuwapa wanafunzi wa madarasa hayo kupitia kwa w/viti wa vitongoji/ serikali za mitaa .

Baada ya kufanya mitihani hiyo wairudishe kwa walimu kwa ajili ya kusahihisha na kupanga matokeo yatakayokuwa yanatumwa wilayani kila wiki .

Je, hawa watu wamejipanga kupambana na corona au wanampango wa kuwatoa kafara hawa walimu watakaokuwa wanasahihisha hizi karatasi za mitihani na masikini hawa wenyeviti wa vitongoji wa serikali za mitaa wasio na posho za kusambazia mitihani hiyo kwa kila mwanafunzi wa drs iv na vii huku wakijiweka katika mazingira ya kupata corona.

Nawasilisha.
Binafsi nasikitika sana shule zimefungwa na hakuna maelekezo yoyote kutoka juu yanayo agiza kufanya hivyo angalia kilichofanyika walitangaziwa wazazi wakachukue mitihani badala yake watoto wakaenda shuleni na wakakusanyika na walikaa mpaka saa 6 mchana toka saa 2 asubuhi wakisubili mitihani bila kuwa na tahadhari yoyote juu ya kujikinga na covid -19
20200506_121910_1.gif


Sent using Jamii Forums mobile app
 
elimu yetu yenyewe ni kukariri, bora wangewaacha watoto wapumzike hadi pale hali itakapotengemaa kidogo. Waache mbwembwe na elimu za kukalili
 
Kwa hiyo Hilo tu ndio mmeliona linasambaza corona
Je, kuhusu kuruhusu ibada kuendelea
Je, kuhusu Shughuli na mikusanyiko masokini kuendelea
Je, kuhusu movement kuruhusiwa kuendelea
Kwa hyo muangalie na hizo sehemu maana corona haichagui wanafunzi tu
Lakini shule tayari zilikuwa zimefungwa hayo masoko na makanisa hayakufungwa toka mwanzo.

Ni hatua ambayo angalau ilichukuliwa na serikali sasa na yenyewe ndo kama hivyo inaelekea kubaya.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
spoon feeding zinaleta shida mkuu, inamaana hujanielewa kweli?
Kwa hiyo unafikiri mimi nataka uni spoon feed?

Nimekuuliza umesoma nje ya nchi?

Umejibu hujasoma msimu wa ugonjwa.

Hilo jibu ni ambiguous kwa sababu huo ugonjwa uko karibu dunia nzima iwe ndani au nje ya nchi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ili kuondoa mikanganyiko yote ni bora shule zifunguliwe ili wanafunzi wote waendelee na masomo katika mfumo rasmi. Zaidi nisome hapa chini nilichoshauri

shule zifunguliwe mwezi wa sita wanafunzi waendelee na masomo

Serikali imeanzisha program maalum ya ufundishaji wa umahiri wa marejeo ya masomo kwa njia ya TV, redio na online TV's. Ofcourse, it is a good idea lakini kuna hali ya ubaguzi fulani kwenye hii program kwa sababu siyo wanafunzi wote wananufaika nayo.

Kwanza, siyo wanafunzi wote, wazazi wao wana uwezo wa kumiliki TV au simu janja. Pili, umeme bado ni changamoto hasa maeneo ya vijijini. Tatu, masomo yanayohusisha calculations kama vile hesabu, fizikia na kemia ni ngumu kuyafundisha kwa njia ya redio wanafunzi wakaelewa. Nne, uwezo wa kununua vifurushi vya data(mb) ili kuaccess masomo hayo kwenye mtandao wa YouTube pia ni tatizo.

Kutokana na changamoto hizo ni bora shule zifunguliwe ili wanafunzi wote waendelee na masomo katika mfumo rasmi. Ukizingatia hali ya maambukizi ya ugonjwa wa corona siyo ya kutisha sana kwani tangu gonjwa hili limeingia nchini mpaka sasa ni vifo 16 tu vimeripotiwa.

Binafsi napendekeza shule zifunguliwe mwezi wa sita wanafunzi waendelee na masomo pale walipoishia. Hii itasaidia kuepusha mkanganyiko wa ratiba ya masomo siku za mbeleni endapo shule zitachelewa kufunguliwa. Kwakuwa ni miezi 3 itakuwa imepotea basi likizo ya mwezi wa 6 baada ya shule kufunguliwa isiwepo, likizo ya mwezi wa tisa pia na likizo ya mwezi wa 12 ili kufidishia miezi iliyopotea.

Pamoja na serikali kuzuia mikusanyiko bado watu wakiwemo wanafunzi wameendelea kukusanyika makanisani, misikitini, minadani, masokoni na baadhi ya wanafunzi wanaonekana magengeni na mitaani wakifanya biashara ya kuuza maandazi,mayai, karanga, ubuyu n.k. Kwahiyo ni bora shule zikafunguliwa waendelee na masomo kuliko kuwaacha wakizagaa mitaani kwa sababu huko ni hatari zaidi kuliko wakiwa shuleni.
 
Hizo karatasi zinasambaza corona na ni hatari sana kwa mstakabal wa maabukizi kuenea kwa kasi.
Waache maramoja.Mamlaka zinazohusika zichukue hatua mara moja kuwakinga watoto dhidi ya corona
 
Binafsi nasikitika sana shule zimefungwa na hakuna maelekezo yoyote kutoka juu yanayo agiza kufanya hivyo angalia kilichofanyika walitangaziwa wazazi wakachukue mitihani badala yake watoto wakaenda shuleni na wakakusanyika na walikaa mpaka saa 6 mchana toka saa 2 asubuhi wakisubili mitihani bila kuwa na tahadhari yoyote juu ya kujikinga na covid -19View attachment 1442569

Sent using Jamii Forums mobile app
Hatua kali za kinidhamu zinawastahili Afisa Elimu na Mkurugenzi kwa kuhujumu jitihada za serikali kupambana na corona
 
Mie naona ni wazo zuri tu, ili angalau kuwakeep busy wanafunzi na mambo ya kusoma. Maana huku mitaani wanazurura tuuu
 
Back
Top Bottom