Idadi ya watoto uliozaa

God'sBeliever

JF-Expert Member
Sep 1, 2015
5,790
3,019
Habari za jumapili wana MMU, natumai wazima, ambao hamko sawa jaribuni kujiweka karibu zaidi na Mungu na kutafutta suluhisho la matatizo yenu

Leo nimeona nije kivingine sio kila siku watu wanaleta mada za kuumizwa tuu hapa, kuambikizwa UKIMWI na kupigwa mizinga. Tuambie una watoto wangapi umezaa, changamoto gani umekumbana nazo kuwalea.

Ambao bado hawajazaa wanategemea kuwa na watoto wangapi? Mimi binafsi sijazaa naomba Mungu anijalie watatu, wote wa kiume, mimi sio mbaguzi ila kulea mtoto wa kike akue kwenye maadili mema asiharibiwe huko shuleni n.k ni ushujaa uliotukuka wenye uwezo naomba msini jadili vibaya ni hisia zangu.

Najiandaa katika mazingira ya kuwa baba, najifunza zaidi zaidi ili niweze kutengeneza stable family changamoto yangu kubwa kwa sasa ni mke bomba wa kuoa, kwa kweli naona chenga tuu ila namtegemea Mungu anipe kifaa cha maana.
 
Changamoto zipo kwa watoto wa jinsia zote katika malezi yao.Chamsingi mzazi kuwa imara katika kuwalea kumuomba Mungu pia atusaidie kuwalea manake dunia hii ya utandawazi kuna mambo mengi sana.
 
Zamani ilikuwa ukizaa mtoto wa kike unapata na mawazo, ila tulipo sasa hivi na tunapoelekea, kulea mtoto wa kiume ni presha zaidi

Wewe mshukuru Mungu Kwa mtoto yoyote utakayejaliwa, mlee kwenye maadili na muombee Kwa Mungu. Mengine ni majaaliwa ya Mungu tu
 
Zamani ilikuwa ukizaa mtoto wa kike unapata na mawazo, ila tulipo sasa hivi na tunapoelekea, kulea mtoto wa kiume ni presha zaidi

Wewe mshukuru Mungu Kwa mtoto yoyote utakayejaliwa, mlee kwenye maadili na muombee Kwa Mungu. Mengine ni majaaliwa ya Mungu tu


Mwenyezi Mungu aepushilie mbali
 
Kwa maisha yetu haya ya mwendokimbiza, baba busy na mama busy, mtoto utakaeweza kupanga ni wa kwanza tu..!!
Baada ya hapo hamna atakaeweza kukumbuka kalenda tena, utashtukia mkeo ana mimba ya miezi mitano..!!

Ni wachache sana tuliofanikiwa kupanga na kuchagua jinsia.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom