Zanzibar ninavyo ifahamu ina ukubwa wa kilomita za mraba 2643 sawa na ukubwa wa kama jimbo moja au mawili ya huku bara na kwa sensa ya 2002 ilikuwa na idadi ya watu 1070000 sawa na idadi ya wilaya kama mbili au tatu za huku bara. Kinacho nishangaza ni idadi ya wabunge ambao ni 50 wa kuteuliwa na 20 viti maalumu, sijuwi madiwani na wenyeviti wa mitaa watakuwa wangapi ama huko kwa kata ndiyo jimbo na kijiji ndiyo kata na kaya ndiyo kijiji nashindwa kuelewa na je gharama za kuiendesha hiyo serekali inapatikana vipi