Idadi kubwa ya wahamiaji wakamatwa katika mji wa Mississippi Marekani

FRANC THE GREAT

JF-Expert Member
May 27, 2016
5,416
7,828
Idadi kubwa ya wahamiaji wakamatwa katika mji wa Mississippi Marekani

1565290977353.png


Katika harakati za kupambana na uhamiaji haramu maafisa wa uhamiaji wa Marekani wamewakamata karibu wahamiaji 700 wasiokuwa na vibali halali katika mji wa kusini wa nchi hiyo wa Mississippi.

Mwendesha mashtaka wa umma amesema watu hao 680 wamekamatwa baada ya uvamizi uliofanywa katika viwanda vinavyotengeza chakula.

1565291038328.png

1565291158359.png


Kiasi kikubwa cha waliokamatwa ni raia wa Amerika ya Kusini. Maafisa wa uhamiaji nchini humo wanasema huenda ikawa hiyo ndiyo idadi kubwa zaidi ya wahamiaji kukamatwa katika jimbo moja la Marekani.

Mapambano dhidi ya wahamiaji haramu ni mojawapo ya ahadi kuu alizotoa Rais Donald Trump wakati alipokuwa anachukua mamlaka.


DW | CNN | Los Angeles Times
 
... Trump anapiga kazi ya maana sana! Jamaa anatekeleza ahadi zake kwa wamarekani hana longolongo.
 
Wahamiaji wengi sana hao,inakuaje wanaingia hawajulikani kirahisi
 
Dah! Trump anachuki kubwa kwa wabeba boksi anaona wanaiharibu Marekani. ila taifa lake kuvamia na kupora rasilimali kwenye mataifa mengine anaona haki yake.
 
... Trump anapiga kazi ya maana sana! Jamaa anatekeleza ahadi zake kwa wamarekani hana longolongo.
Mbona ukuta wa Mexico hajaujenga bado wakati alisema ndani ya siku 100 ataukamilisha kukamatwa kwa wahamiaji haramu Marikani ni zoezi endelevi la kila jimbo la Malikani hiyo hikua ahadi yake kila Raisi walilifanya, anaogopa sasa uchaguzi umekaribia ndomaana propaganda zimeanza
 
Dah! Trump anachuki kubwa kwa wabeba boksi anaona wanaiharibu Marekani. ila taifa lake kuvamia na kupora rasilimali kwenye mataifa mengine anaona haki yake.

wanasahau kuwa chanzo cha hao wahamiaji ni wao kuharibu huko walikotoka, mimi naombea warudi nyumbani wkajipange na kujiuliza wamefikaje hapo, ndipo watakapogunduan serekali zao vibaraka wa marekani na hakika kitanuka.
 
... Trump anapiga kazi ya maana sana! Jamaa anatekeleza ahadi zake kwa wamarekani hana longolongo.
Hapa wamarekani hawawezi kumsifu because watakosa manpower ya black collar jobs
 
Back
Top Bottom