popbwinyo
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 4,986
- 3,608
Mkuu watoto ni faraja aisee,ukimudu kuwatunza,Kweli kuzaa ni kama kupanda mbegu,hutakiwi kupanda mbegu moja panda nyingi maana hujui IPI itakufaa....
Mkuu watoto ni faraja aisee,ukimudu kuwatunza,Kweli kuzaa ni kama kupanda mbegu,hutakiwi kupanda mbegu moja panda nyingi maana hujui IPI itakufaa....
Mkuu,usisahau huyo unaemjibu ni mvaa mlege anaewazia maisha km anayoyaona ktk tamthilia za ulaya,hayajui maishakiuhalisia ila anajua matamanio na hisia,Nakaribia kuwa mhenga ila ki ukweli familia ya watoto kuanzia nne kuendelea ina raha sana hata kwa watoto wenyewe.
Kikubwa uwamudu maana usipo wamudu napo dhambiHata 10 sawa bora tu unaweza kuamudu wote
Mkuu uko sahihi kabisa watu wanaiga tu.Mkuu,usisahau huyo unaemjibu ni mvaa mlege anaewazia maisha km anayoyaona ktk tamthilia za ulaya,hayajui maishakiuhalisia ila anajua matamanio na hisia,
Kuna muda mkuu,
Ndugu waliniacha,wanawake waliniacha lkn wanangu hawajaniacha,japo bado wadogo kiasi lkn wamekuwa baraka na furaha maisha yangu yote,aisee bila faraja ya watoto nadhani ningesha haribika sana,maisha siyo makuuubwa lkn tunasukumana hvo hvo na tunaishi kwa furaha zaidi hata ya wenye mtoto mmoja ama wasio na mtoto kabisa,kuna watu wanabeza humu wakisema kuhusu maisha,lkn huku kitaa kuna watu wanashida sana kimaisha na hawana mtoto hata mmoja,lkn wapi watu wanawatoto kibao na bado wanawazidi ubora wa maisha,
Kifupi ni vile unavyofaendesha wewe,
Maisha magumu nitashindwa kuwapa matumizi sahihi na stahikiNaongeza wawili hapo
Hahahaaaa. Duuh!
Wewe uliefyatua wawili unataka kutuambia unamzidi ubora wa maisha na matunzo kila aliyezaa watoto saba?Watoto wawili maximum watatu sasa wewe ukifyatuana utaisoma namba
Mkuu ndio umeamua kuniandikia risala duuh!Wewe uliefyatua wawili unataka kutuambia unamzidi ubora wa maisha na matunzo kila aliyezaa watoto saba?
Wapo watu wana watoto kumi na wanakuzidi kiwango cha ubora wa malezi wewe mwenye mtoto mmoja,
Usihamishie ubavu wako mdogo kwa kila mtu,unadhani wazungu kuzaa mmoja wanapenda?
Life style na mazingira kwao vinawabana,kuna watu Leo hii wanaogopa kuoa na kuzaa eti hawana uwezo,sasa umri unaenda uwezo hauji na wanaishia kuishi km wanyama,
Mara ingine tujifunze kuyakabiri matatizo na changamoto ndo kukua kwa akili na uwezo,
Nikushirikishe jambo,
Wakati sina watoto,nilikuwa na godoro na nguo Kali,raba Kali,
niliogopa kuoa na kuzaa sababu nilidhani sina uwezo,kumbe uwezo nilikuwa nao na sikuutumia kwa ukubwa Mungu alouweka ndani yangu,
Nilikuwa najifikilia mm tu,
Nilipo oa tena kwa nguvu,nilihisi mzigo na nikajua ntaibika,hii ilifanya niamue kujituma sababu kila siku mke anataka kula na kuvaa na aonekane mrembo,nikaongeza nguvu ya kufanya kazi,nikaacha kuchagua kazi,nikawa na bidii Mara mbili ya awali,kilichotokea japo mwanzo nilitaabika sana lkn nikaanza kujijenga,nikanunua vistuli,nikaanza kuwaza kodi,nikanunua vyombo na kidogo kidogo nikaanza kuwa na vitu,
Nikapata shamba,
Nilipopata watoto mapacha,nilihisi mzigo mzito Mungu kanipa,trust me,ile hofu iliniongezea nguvu Mara mbili zaidi ya nilivyokuwa na mke tu,nikajikuta nafanya kazi km mbwa,napata pesa hadi ya kuweka akiba kwa tahadhari,nikajifunza kuweka akiba maana sijui kesho ya wanangu,
Nikapata balaa la kukimbiwa na mke maana alikuwa na ndoto zake kubwa zaidi ya nilivyokuwa,
Hili nalo likanipa hasira ya kutafutamaana niliamini pesa imefanya nikimbiwe,ndugu pia walinichukulia poa,nilifanya kazi kazi mnyama,nikalea wanangu,na nnavyoongea wapo form five,maisha yangu si mabaya,nnaishi vizuri sana na nnawapenda wanangu,na kwa ajili yao nna nyumba nimeoangisha na nnakiwanja,
We ar doing best,
Lkn yote hii ni sababu ya kutolikimbia jukumu,nililivaa likanipa msukumo,
Saa hizi aaaaaaah kaheshima kapo,nipo sawasawa,
NB tusikimbie majukumu
Majukumu huzaa msukumo,
Msukumo huzaa ari ya kupigana,
Ari ya kupambana huzaa kipato na ziada,
hahahaEti mkuu wawili ni ukiwa, raha wagombanie maanadazi yaishe si kulaza viporo kila siku