IBM (Tanzania) kupunguza msongamano wa magari katika Barabara za DSM!

Baba_Enock

JF-Expert Member
Aug 21, 2008
7,076
2,443
Well: Well: Well:

Leo alfajiri (saa 11 CAT) nikiwa nasikiliza BBC (Swahili Service), nimemsikia afisa wa IBM (T) - David Sawe - akisema kuwa wapo kwenye mkakati wa kujadiliana/kuishauri serikali jinsi gani kampuni hiyo inavyoweza kuisadia serikali katika kupunguza "foleni" ndani ya JIJI la DSM...

Alisema mojawapo ya njia wanazoweza kutumia ni kwa njia ya CCTV (data collection) na kwa kutumia data hizo inawezekana kufanya maamuzi ya barabara ipi itumike vipi, e.t.c

Inawezekana wazo ni zuri, lakini kwa maoni yangu hii haiwezi kuwa "sure way" ya kutatua tatizo la "foleni" kwa kuwa DSM "hamna barabara" na nadhani hilo ndilo tatizo la msingi!

Sawe - I hope hii isije kuwa "nitoke vipi ya IBM(T)"!
 
Well: Well: Well:

Leo alfajiri (saa 11 CAT) nikiwa nasikiliza BBC (Swahili Service), nimemsikia afisa wa IBM (T) - David Sawe - akisema kuwa wapo kwenye mkakati wa kujadiliana/kuishauri serikali jinsi gani kampuni hiyo inavyoweza kuisadia serikali katika kupunguza "foleni" ndani ya JIJI la DSM...

Alisema mojawapo ya njia wanazoweza kutumia ni kwa njia ya CCTV (data collection) na kwa kutumia data hizo inawezekana kufanya maamuzi ya barabara ipi itumike vipi, e.t.c

Inawezekana wazo ni zuri, lakini kwa maoni yangu hii haiwezi kuwa "sure way" ya kutatua tatizo la "foleni" kwa kuwa DSM "hamna barabara" na nadhani hilo ndilo tatizo la msingi!

Sawe - I hope hii isije kuwa "nitoke vipi ya IBM(T)"!


David Sawe David sawe David sawe. mhhhhh

Kumbe alishatoka utumishi. Au ni sawe mwingine?
 
folleni za dar chanzo ni barabara mbovu,poor driving skills,madala dala kusimama hovyo ,hapo ibm haina mchango kabisa
 
tunatapeliwa, hebu tuuchunguze vizuri mkataba wa IBM na tuuhoji uwezo wao na mbinu zao za kuondoa foleni.
Bila kujengwa kwa barabara za kutosha foleni haiwezi kwisha
 
Sioni uhusiano wa IBM

  • na kupunguza foleni
  • sioni uhusiano wa CCTV na kupunguza foleni?
  • Je IBM wamafanya kazi hii wapi au Tanzania ndio Pilot site yao ya solution zao na congestation ???
But kwa serikali yetu ya Tazania ukmjumulisha na huyo jamaa mhhh any project is possible
 
Sioni uhusiano wa IBM

  • na kupunguza foleni
  • sioni uhusiano wa CCTV na kupunguza foleni?
  • Je IBM wamafanya kazi hii wapi au Tanzania ndio Pilot site yao ya solution zao na congestation ???
But kwa serikali yetu ya Tazania ukmjumulisha na huyo jamaa mhhh any project is possible

Mkuu usisahau bongo ni kichwa cha mwenda wazimu!

Suala la msongamano Dar linahitaji maamuzi magumu kweli,

Ninashaka na utashi wa wasimamia mambo, hiyo dili ya IBM (T)

Nahisi itapita kama kama wameandaa mgawo wa kutosha wala sio kwa effeciency ya proposal yao.

Kuna njia za ku-utilize miundombinu mbadala hapa mjini kama anga, maji na reli (yote haya ni maamuzi magumu) mbele ya walaji.
 
kila nchi kuna poor driving. Sio Dar tu.
japo watu wengi bado wanaamini kuwa magari yameongezeka Dar lakini itakuwa ni ujinga kuamini kuwa kuna ufumbuzi mwingine nje ya improvement ya barabara zetu hapa jijini!
Angalia wenzetu (sio US, UK, EU au Japan) Nairobi na Kampala: Kampala wamejenga Northern bypass na japo foleni zipo lakini imabadilisha kwa kiasi kikubwa foleni za awali, angalia kinachoendelea Nairobi wakati Dar bado ina Barabara zilizile za Mzee Kitwana Kondo ambapo Tabata, Mbezi, Rangi tatu, Kitunda n.k yalikuwa mapoli.
Nimesikia pia hiyo habari BBC lakini IBM watafanya simulations za kawaida tu na watapendekeza improvement za miundombinu tatizo tunalolijua wote.
Lakini utawala wetu huu tunaoujua si ajabu wakatoa some $ mm kwa ajili ya "IBM Feasibility Study on eradicating congestion in Dar"!!!
 
Mimi nilivyosikia asubuhi kidogo nizime radio, nikadhan hii radio siku hizi imeanza kusema uongo, IBM na foleni kweli inawezekana.

Unatuletea teknolojia ya kompyuta kwenye issue inahitaji barabara, kuna siku watasema tuwaachie tataizo la ujenzi holela walitatue wao kwa kompyuta.
 
Nafikiri cctv itasaidia kukontroo poor driving, hivyo kusaidia kupunguza msongamano!

... inawezekana wazo lako ni relevant. Hata Dar ikipewa zawadi ya bure ya traffic management system bado tatizo la msingi linabaki pale pale. Miaka 50 baadae miundombinu imebaki pale pale na imeharibika zaidi. Nani hakumbuki lami iliyokuwepo hata mitaa ya ndani ya Mwenge ukiacha maeneo mengine? Natamani kwamba Dar ya kileo yenye wakazi millioni tano na ushee ingekuwa tofauti na siyo SLUM (aftermath of ISLUMIZATION) na kwa hiyo hata kwa kuiga mijiji ya kikweli infrastructure ya ki-jiji ingekuwepo. Hii ni pamoja na mifumo ya ki-leo ya barabara na mipango endelevu inayokabiliana na ukuaji wa jiji. Wapo jamaa kibao walio na Ph D za urban planning tofauti na miaka ile ya mwanzo wa Jamhuri yetu.
Whats good fo the goose?
 
Hii ni "NITOKE VIPI!!!" hakuna lolote... Kama walivyotangulia Wadau Kupunguza Foleni Dar kunahitaji MAAMUZI MAGUMU!!!
1.Bandari kavu maeneo ya Ruvu Station... Malori ya Mizigo yachukue Mizigo,Mafuta na Ma-container hapo.
2.Ghorofa la Police Salender,na yale mawili ya kwenye makutano ya Ocean na A.H.Mwinyi Road.ilikufanya Ocean Road kuwa Dual carriage.
3.Shule za msingi za Bunge,Jamhuri,Kisutu zihamishwe badala yake pajengwe Parking za ghorofa...
4.Masoko ya Samaki la Msasani,Kunduchi,Ununio na Kawe yaboreshwe kupunguza Msongamano wa kwenda soko la Ferry.
5.Barabara ya Toure itokayo Maeneo ya Seacliff baadaye inakuwa Kenyata Road ambayo inakutana A.H.Mwinyi Road pale Salender iwe Dual carriage na ijengewe daraja lake pembeni ya Salender na ipite pale litakapobomolewa la Ghorofa la Police Salender,na yale mawili ya kwenye makutano ya Ocean na A.H.Mwinyi Road.
Hayo ni baadhi tu yapo mengi sana...
 
Kinachozungumzwa hapa tayari kilishafanyiwa utafiti na JICA kwenye ule mradi uliojulikana "The Study on Dar es Salaam Transport Policy and System Development Master Plan". Na kimsingi DART ni sehemu ya utekelezaji wa mapendekezo ya hiyo master plan, pamoja na ujenzi wa "fly-overs/under-pass" kwenye jiji la DSM. Bahati mbaya report kama hizi haziwekwi hadharani, utadhani ni siri wakati siyo siri. Wanachopendekeza IBM tayari kilishafanyiwa utafiti na hao JICA, na naamini traffic count ni shehemu ya takwimu zilizo kusanywa. Kwa hiyo siyo kitu kipya.
 
Kinachozungumzwa hapa tayari kilishafanyiwa utafiti na JICA kwenye ule mradi uliojulikana "The Study on Dar es Salaam Transport Policy and System Development Master Plan". Na kimsingi DART ni sehemu ya utekelezaji wa mapendekezo ya hiyo master plan, pamoja na ujenzi wa "fly-overs/under-pass" kwenye jiji la DSM. Bahati mbaya report kama hizi haziwekwi hadharani, utadhani ni siri wakati siyo siri. Wanachopendekeza IBM tayari kilishafanyiwa utafiti na hao JICA, na naamini traffic count ni shehemu ya takwimu zilizo kusanywa. Kwa hiyo siyo kitu kipya.


Sasa traffic count itapunguzaje congestation . kama JAICA wanazo takwimu za road usage ya barabara za dar hii solution ya IBM ni duplicate ya kazi waliyofanya JICA ?

Au ni solition ya ku
monitor tu. Monitoring Road usage hitasaidi tunataka solution ya management . Ni sawa sawa na kumpima mgonjwa wa ukiwmi useme umetatua tatizo kwakugundua tu ana CD4 ngapi, Bila kumpatia dawa haisaidiii.

Nchi isiyokuwa na pesa inahitaji kufanya priority makini kwenye miradi yake. Kama JICA walifanya monitoring na kutoa takwimu kinachtakiwa na kinachofuata ni suluisho nini kifanyike kupungza congestion sio duplication ya ya kurecod tena msongamano wa magari . kazi ambayo JICA wameshafanya. Au mimi sijaelewa.

Kuna tofauti ya Solution finding a problem to solve and a problem finding a solution . Hii ya IBM ni Solution finding a problem to solve.
 
The conceipt is good. Tatizo ni miundombinu. Barabara zenyewe hazitoshi.
Ujenzi wa FLYING OVER umeishia wapi? Au ilikuwa danganya toto tu mradi kura zitoshe?
 
Mimi nilivyosikia asubuhi kidogo nizime radio, nikadhan hii radio siku hizi imeanza kusema uongo, IBM na foleni kweli inawezekana.

Unatuletea teknolojia ya kompyuta kwenye issue inahitaji barabara, kuna siku watasema tuwaachie tataizo la ujenzi holela walitatue wao kwa kompyuta.

Jamani solution ya foleni Dar sio kujenga barabara tu kama wengi tunavyofikiria. Kuna mambo mengi yanayopashwa kuendana na ujenzi huo wa barabara na hapa najua wengi wanazungumzia fylovers. Mojawapo ya suluhisho lingine la foleni ni kupanua mji na kuzitoa baadhi ya ofisi muhimu katikati ya mji ili watu badala ya wote kuamka asubuhi tukielekea Samora Avenue, tuwe tunaelekea mbagala, Tegeta au Mbezi!!!!

Tiba
 
Back
Top Bottom