Ibara ya 30 (d): MwanaHalisi kufungiwa kwa kuvunja katiba ya Tanzania?

kwanza lifungiwe daily news ambalo salva alipost ule upupu wake eti slaa hatokuwa rais kwa sababu ule ni ukiukaji wa uandishi first degree,..jk anamuogopa kubenea kuliko anavyomuogopa slaa,..siku likifungiwa zitto atafurahi au atachukia?otea..
 
gazeti limevunja taratibu za mahakama na katiba ya JMT
Yawezekana na Mkapa kama Alishiriki Kuliibia Taifa kwa Kugushi Nae Pia atakuwa kavunja Sheria za Nchi na Kavunja Katiba ya Nchi ... Huyo hafai ni waa kuogopwa kama Ukoma China hunyongwa tu arabuni anakatwa Mikono..

Mvua na Jua Bora Nini!!
 
Mimi hapa nini hardcopy(nakala ngumu):eyeroll1: najaribu kuitype nitaiweka soon

ama kweli kwa habari hii GAZETI lazima lifungiwe

Ukimaliza Kutype na wewe hutokuwa unaingilia uhuru wa Mahakama na kuvunja Katiba? si ungeiscan na kuipaste tu.
kumbuka Hatutaki vichapizi
 
Yafungie uone utakavyoshushwa Mshipa! Unafanya mchezo na mali za SHEIKH TWANI ??

Yes! Kwa wao watashushwa, lakini kwa watu wa ukweli kama mimi na wengine baadhi hakuna cha shipa wala nini. Shipa anashushwa mfuasi wa Sheikh Twain tu. Wengine Mungu wa ukweli tunaye.
 
Habari nilizozipata ni kwamba waziri anajiandaa kuitisha press conference kulifungia gazeti hili kwa kukiuka taratibu za nchi
 
Habari nilizozipata ni kwamba waziri anajiandaa kuitisha press conference kulifungia gazeti hili kwa kukiuka taratibu za nchi

Hahaha lol
we jamaa ni una kazi sana,
Haya tunasubiri mwisho wa huyo "waziri" wako, akishalifungia!
 
... umetumia neno UMAFIA ipasavyo. Sasa ndani ya srtucture ya UMAFIA yupo pia Mafioso kiboko yao wote. Si unaona jamaa kakaa kimya miaka yote licha ya midongo kibao. Ukiacha ya hii mada, kanifurahisha sana na harakati za uhamasishaji wa maendeleo ya kwetu Ntwala. Niwaambieni kitu, yuko tayari kwenda KISUTU kutoa ushahidi wake. Siku hiyo ikiwadia, wapo watakaotamani ardhi ipasuke. Ubishi hakuna hapo. Siku hiyo atatema cheche, kibarua na fundi wake atajulikana.
 
Leo gazeti la mwanahalisi limechapisha makala yenye kichwa cha " mkapa kutinga kortini"

Makala hii ya kubenea imeeleza jinsi mkapa na jakaya walivyoshiliki katika ununuzi wa nyumba ya ubarozi ROMa kwa kesi inayomkabili Pro Mahalu


Je Mwanahalisi haijaingilia uhuru wa mahakama


30.-(1) Haki na uhuru wa binadamu ambavyo misingi yake imeorodheshwa katika Katiba hii havitatumiwa na mtu mmoja kwa maana ambayo itasababisha kuingiliwa kati au kukatizwa kwa haki na uhuru wa watu wengine au maslahi ya umma

(d)kulinda sifa, haki na uhuru wa watu wengine aumaisha binafsi ya watu wanaohusika katika mashauri mahakamani, kuzuia kutoa habari za siri; kutunza heshima, mamlaka na uhuru wa mahakama;

Toa pombe zako hapa, unapenda ufisadi au ni fisadi?
 
Leo gazeti la mwanahalisi limechapisha makala yenye kichwa cha " mkapa kutinga kortini"

Makala hii ya kubenea imeeleza jinsi mkapa na jakaya walivyoshiliki katika ununuzi wa nyumba ya ubarozi ROMa kwa kesi inayomkabili Pro Mahalu


Je Mwanahalisi haijaingilia uhuru wa mahakama


30.-(1) Haki na uhuru wa binadamu ambavyo misingi yake imeorodheshwa katika Katiba hii havitatumiwa na mtu mmoja kwa maana ambayo itasababisha kuingiliwa kati au kukatizwa kwa haki na uhuru wa watu wengine au maslahi ya umma

(d)kulinda sifa, haki na uhuru wa watu wengine aumaisha binafsi ya watu wanaohusika katika mashauri mahakamani, kuzuia kutoa habari za siri; kutunza heshima, mamlaka na uhuru wa mahakama;


Watu kama nyie mnatia shaka. Pengine mmezeeka sana, mnaumwa, mmefugwa na mafisadi au ni mafisadi wenyewe. La msingi ni lazima kujua, mnaweza kufungia gazeti hili ila mawazo ya kimapinduzi hamuwezi kuyafungia moyoni mwa watu wengi. Ni vyema mjue kuwa si rahisi kuendelea kutengeneza MISUKULE kama ilivyokuwa zamani.
 
Wakuu naona jeykey bado anatype hii habari.

Jisevieni wenyewe hii kitu ya Mwanahalisi

Mkuu ahsante sana kwa kazi ya kuweka hili bandiko hapa! Nimesoma na kuelewa nini MWANAHALISI alikusudia kuieleza jamii. Hapa sioni kama Waziri Kombani anaweza lifungia hili gazeti. Maana sioni kama limeingilia uhuru wa mahakama kwa namna yeyote ile. Kilichofanyika ni kuieleza jamii ukweli tena wa vitu ambavyo haiyumkini sio vigeni na nina uhakika vilikuwa vinafahamika kwa baadhi ya watu ila kukosekana kwa ujasiri tu wa nani awe wa panya wa kwanza kumfunga paka kengere. Maana yote hayo ni kama report tu hakuna jipya na wala jamaa hawajaamuru wala kuishurutisha mahakama iamue kutokana na vielelezo ambavyo MWANAHALISI imevitoa. Kazi kwao maana sasa kuna watu nina uhakika wameshikwa pabaya kwa maamuzi yao ya kukurupuka na kuzushiana!
 
Nkurukumbi, nkurukumbi, niyo yazaile mayenjeeeeeeeeeeeeeeeee, otalitela, otalijumaaaaaaaa, niyo yazaaile mayenjeeeeeeeeeeee......... aghhhhhhhh....... inabidi tuimbe kilugha. We Jeykey utakuwa kama Kombani na Werema. Walisema katiba ibaki kama ilivyo, president au boss wao akasema ifanyiwe mabadiriko sasa na wewe utachongaaaaaaaa alafu gazeti liaendelea kupeta.

Umenikumbusha mbali sana kwa ka huo wimbo!!!
 
Msilizingatie gazeti hilo kwani linaongoza kwa kukiuka misingi ya uandishi wa habari. Mkitaka kuniamini someni cv ya mhariri wake. Pia, ili habari iwe habari kuna mambo ya msingi matatu ambayo yote mwanahalisi huwa linakiuka.

1. Ni lazima kuwe na 5 Ws + H.

2. Ni lazima maadili yote ya Newsworthiness yazingatiwe.

3. Ni lazima news elements zizingatiwe.

Hayo yote kwa mwanahalisi hayazingatiwi kabisa. Zamani uandishi wa aina hiyo ulikuwa unaitwa yellow Journalism na umewahi kusababisha vita ya nchi kwa nchi.

INASHANGAZA SANA KUONA GAZETI HILI BADO LINACHAPISHWA. NADHANI KUKIUKWA KWA MAADILI YA UONGOZI KATIKA NCHI KUNASABABISHA MAGAZETI KAMA HAYA KUDUMU.
Nitaweza fafanua kama sijaeleweka.

Unaudhi kweli, lakini basi tuzuie hasira ili tukuelimishe. Haya mambo 3 uliyooredhasha yana mantiki kweli? Nyerere alikuwa akitumia msemo, ''Mambo ya kijinga sana haya''. Kwa nini usieleze Gazeti limekosea nini hasa? Kuripoti kwamba Mkapa atasimama kizimbani ni makosa? Kueleza kuhusika kwake kwenye manunuzi ya ofisi za ubalozi ni makosa? Unataka magazeti yote yaipambe tu serikali, kama kuna tatizo lisitajwe kwa kujificha kwenye ''Maadili ya news worthness'' Kwanza ni kitu gani hiki?

Nadhani kushangaa ni kuona baadhi ya mawazo kama ya kwako, kutaka kuminya uhuru wa habari. Hampendi kupata changamoto. Jibuni hoja kwa hoja ni siyo vitisho. Ni lazima watu wapatiwe mbadala wa kila kitu ili wao wachague hasa pumba na ngano halisi ni ipi. Mnaogopa watu kupata options kwa sababu mwajua watakachokichagua. Kama hamuwezi basi mrudi kwenye mfumo mbinyo tujue tu moja, ka Libya.
 
ivi kaka ukiibiwa dola zako na mara ukagundua aliyekuibia ni Mr.Mwanza je kati ya Mr.Mwanza na wewe uliyeibiwa nani anawajibika kwenda kumshitaki mwenzake?
Tafakari kabla ya kuandika

Mr Mwanza aligawana na Mr Tabora afu unatakiwa ukashtaki kwa Mr Tabora

Tafakari..
 
Guys,
Huyu Jeykey amekurupuka sana na haya ndiyo matatizo ya Watanzania wengi. Mimi nimeisoma hiyo habari jana na nakala ninayo home !
Mkapa atakwenda kutoa tu ushahidi yeye kama alivyokuwa Mtendaji Mkuu wa JMT na jinsi alivyofanya kazi na Prof Mahalu na jinsi yeye kama Mkapa alivyoruhusu ununuzi wa nyumba ile ya Ubalozi kule Rome. Alafu kuna kitu ambacho huyu Jeykey anatakiwa kujifunza ni kwamba hata kama Mwanahalisi litafungiwa yeye kama yeye na jamaa zake watafaidika ama watapata hasara kwa kufungiwa Mwanahalisi ? Mwanahalisi limefichua uozo mwingi sana wa Serikali na kusaidia watendaji kujipanga vizuri ! Sasa kama Jeykey yeye anafurahia uozo na ufisadi kutoanikwa hadharani basi ajue yeye ndio looser kwani wenzake wanatibiwa nje ya nchi na familia zao, Yeye tutapishana kwenye vikorido vya Zahanati za Kata tu ! Kufungiwa kwa Mwanahalisi inatakiwa kuwa ni msiba kwetu na sio furaha ! Ufisadi ukitokomezwa huduma zitaboreshwaaaa.............!!! Jeykey are you thinking positive....????
 
Msilizingatie gazeti hilo kwani linaongoza kwa kukiuka misingi ya uandishi wa habari. Mkitaka kuniamini someni cv ya mhariri wake. Pia, ili habari iwe habari kuna mambo ya msingi matatu ambayo yote mwanahalisi huwa linakiuka.

1. Ni lazima kuwe na 5 Ws + H.

2. Ni lazima maadili yote ya Newsworthiness yazingatiwe.

3. Ni lazima news elements zizingatiwe.

Hayo yote kwa mwanahalisi hayazingatiwi kabisa. Zamani uandishi wa aina hiyo ulikuwa unaitwa yellow Journalism na umewahi kusababisha vita ya nchi kwa nchi.

INASHANGAZA SANA KUONA GAZETI HILI BADO LINACHAPISHWA. NADHANI KUKIUKWA KWA MAADILI YA UONGOZI KATIKA NCHI KUNASABABISHA MAGAZETI KAMA HAYA KUDUMU.
Nitaweza fafanua kama sijaeleweka.

Ndugu Kibana, Ufahamu wako ni mdogo sana ktk taaluma ya Habari. Huenda umebahatika kusoma certificate ukajua a,b,c za uandishi ndo unasumbua nazo.

Hizo 5w's+H unazozingumzia huenda hata huzifahamu vizuri.

Taaluma ya uandishi (writing for print media) inagawanya habari kwa namna mbili. Kwanza ni habari za kuripoti matukio (news reporting), pili ni habari za uchambuzi (news analysis ambazo pia hujulikana kama feature writting).

Mwandishi anayeandika kwa kuripoti matukio, kwa mfano Kikwete kasafiri nje ya nchi, Gari la abiria lapata ajali etc, ni lazima aoneshe hizo 5w's+H. Yaani What,Who,Where,Why,When and How. Na zinakuwa kwenye aya ya kwanza ya habari (Lead of the story).

Lakini kwa mwandishi anachambua habari (news analysis) ambazo mara nyingi ni feature articles si lazima azingatie hiyo kanuni.

Ndio maana mwandishi wa makala (feature) ukisoma aya ya kwanza ya habari yake mara nyingi haifanani na kicha cha habari yenyewe.

Sasa kabla hatujahukumu kama MwanaHalisi wamefanya kosa au lah, tujiulize kwanza uandishi wa MwanaHalisi ni wa Kuripoti matukio (news reporting) au ni wa uchambuzi (news analysis).

Bila shaka MwanaHalisi ni wachambuzi. Na kama ndivyo dhana ya kutafuta 5w's+H imetoka wapi?? Kwenye feature writting hizo 5w's+H zinaweza zikawepo lakini si lazima ziwe zote, kwa sababu habari nyingi huwa ni za uchunguzi hivyo baadhi ya taarifa huweza kuzuiwa kwa sababu za kiusalama au kitaaluma.

Pia si lazima ziwe kwny aya ya kwanza ya habari kama ilivyo kwny habari za kuripoti. Labda ndugu Kibana umetafuta hizo elements kwenye aya ya kwanza ukazikosa ukakimbilia kusema hazipo.

Kama unabisha leta habari yoyote iliyoandikwa na MwanaHalisi ambayo haina What kwa maana ya tukio,Who kwa maana ya anayehusika na hilo tukio, When kwa maana ya muda wa tukio, Where kwa maana ya mahali etc.

Kwa mfano katika hiyo makala inayokalamikiwa elements zote zinaonekana kama ifuatavyo:

WHAT-Kigogo kutinga kortini.

WHO-rais Mkapa,

WHY-tuhuma za ufisadi,

WHEN-23/02/2003 wakati Mkapa alipozindua jengo hilo la ubalozi.

WHERE-Rome, Italy

HOW-Kutajwa katika hati ya ushahidi ya Prof.Mahalu.

Sasa wewe Kibana ulitaka 5w's+H zipi tena zaidi ya hizo??

Kibana unachekesha sana kwa kujifanya unajua taaluma ya habari kumbe mbumbumbu.

Kama kweli taaluma yako ni habari, ukiangalia House Style ya MwanaHalisi utagundua wanafanya Investigative Journalism. Na hawawezi kushtakiwa popote kwa kuandika kama walivyoandika.

Kasome Media Law utaelewa kitu kinachoitwa Journalism of Outrage. Na ndicho wanachofanya MwanaHalisi. It means the watchdog role of the media. It is driven by outrage agaist people entrusted with power and responsibility abusing their positions of trust.

Rudi darasani kijana, ama sivyo usijaribu kujiita mwanahabari maana unadhalilisha taaluma. Kasome Authoritative statements on Media Protection utaelewa nachosema.
 
Back
Top Bottom