Ibara ya 30 (d): MwanaHalisi kufungiwa kwa kuvunja katiba ya Tanzania?

Walifungie waone. Ndipo watadhihirisha umafia wao. Tulisha jua uozo wote wa nch hii, hakuna jipya. Labda Wanataka furugu, He!!
 
Hamna kitu nisee tu story na kichea tofauti; kiapo cha Ben tayari na kinamlinda mshtakiwa Mahalu; swali je kesi itaendelea? sidhani kama kuna chochote naona wametoa habari iliyofichea kumbe hata Ben huwa anaapa kama raia kuthibitisha madai yake; halafu JK alishitaki vipi wakati wote walikuwa mambo ya nje na habari hiyo alishawahi kuithibitisha bungeni?

Mkuu hiyo ndio lugha ya wapi? Ni kitanzania hikihiki au ni kile kilichochanganywa na Kiswahili au ndio hicho kigagagigikoko??? Maana nimeshindwa kuelewa mchango wako, punguza haraka tulia uandike vizuri ili tupate ujumbe wako.
 
Wameweka ushahidi so wakiona hawajaridhika akina JK na mkapa waende mahakamani waache kumwagia watu kwa tindikali; limeenda chimbo kweli kweli leo si mchezo ila kulifungia ni kuonea maana lina uahsahidi kama vipi wakane ushahidi huo

ivi kaka ukiibiwa dola zako na mara ukagundua aliyekuibia ni Mr.Mwanza je kati ya Mr.Mwanza na wewe uliyeibiwa nani anawajibika kwenda kumshitaki mwenzake?
Tafakari kabla ya kuandika
 
Magazeti mengi tu yanakiuka misingi ya uandishi kwa kuzingatia kuuza bila kuona kama jamii itakachokisoma itaathirika nacho.
 
...jee kama inawezekana ulitaka kuziiba mwenyewe, Mr Mwanza akaweka kauzibe jiulize hivi, inawezekana kumshitaki Mr Mwanza? (Na hapo wewe mwenyewe ukiwa na miguvu kibao hata ya kusaini miswada kuwa sheria kamili)

Reading between the lines waweza kubaini pia kwamba ni nani amesafishwa na article yenyewe. Huyo huyo mwenye miguvu.
 
Mh selina Kombani atafanya kazi yake

Watu wameshaandika nani mhusika lakini bado naona hamuelewi, tafadhali soma comment za watu kabla ya kuandika na muache kupotosha wengine waziri wa Katiba na mabo ya habari wapi na wapi
 
Gazeti hili litafungiwa kweli

kwa hii habari duuh

Aisee yaani wewe unachekesha kweli, thread hii umeanzisha wewe mwenyewe kwa ID yako ya jeykey, halafu unakuja kwa ID ya kupeng'e unajifanya eti ni mtu mwingine ndio unasupport yaani unaniacha hoi. ila waombe Mods wakurudishie ile ID yako ya marelia sugu, watu wameimis sana.
 
Huyu jeykey
katoroka mirembe
polis wako wapi wamtie pingu wamrudishe
gazeti kufungiwa kwann kwa vile limeandika ukweli?
Au anataka liandike kusifia maovu
afu sheria haijui bora akae kimya
 
binafsi sijasoma sheria wala taaluma ya habari. Je hizo habari zilizoandikwa ni za kweli au zimetungwa ? kama ni za kweli kwa nini hatustahili kuzipata et ni siri! Kama ni hivyo maana yake habari zote hatutaruhusiwa kuzipata kwa sababu waandishi watakuwa wamevunja uhuru wa mtu?
 
Msilizingatie gazeti hilo kwani linaongoza kwa kukiuka misingi ya uandishi wa habari. Mkitaka kuniamini someni cv ya mhariri wake. Pia, ili habari iwe habari kuna mambo ya msingi matatu ambayo yote mwanahalisi huwa linakiuka.

1. Ni lazima kuwe na 5 Ws + H.

2. Ni lazima maadili yote ya Newsworthiness yazingatiwe.

3. Ni lazima news elements zizingatiwe.

Hayo yote kwa mwanahalisi hayazingatiwi kabisa. Zamani uandishi wa aina hiyo ulikuwa unaitwa yellow Journalism na umewahi kusababisha vita ya nchi kwa nchi.

INASHANGAZA SANA KUONA GAZETI HILI BADO LINACHAPISHWA. NADHANI KUKIUKWA KWA MAADILI YA UONGOZI KATIKA NCHI KUNASABABISHA MAGAZETI KAMA HAYA KUDUMU.
Nitaweza fafanua kama sijaeleweka.

This is more academical !!!
 
Binafsi napenda kumpongeza Said Kubenea kwa kazi nzuri aliyo kwisha kuifanya mpaka dakika hii. Huu uhandishi wa kufwata vigezo hautusaidii na hauna tija. Sina tahaluma ya habari na sitaki kujua kama amevunja au hajavunja kanununi au ameisigina katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania. Ukweli utabaki kuwa ukweli. Je wewe unaridhika na mwenendo wa hali ya watanzania kwa hivi sasa ukilinganisha na watawala wao?
Hii ina nikumbusha mtawala maharufu wa Haiti (Aristide???). Kipindi hicho ilikuwa raisi unatakiwa uwe na nyumba. Jamaa hakuwa na nyumba na ilibidi wapiga kura wake wampatie ili aweze kukidhi vigezo. Hatimaye aliukwaa uraisi na baada ya miezi kadhaa alikuwa ni bilionea wa kutupwa na kusahau aliko toka. Jamani kama ni kweli kwa nini wakuu hawa wasifikishwe mahakamani. Kwani na wao pia si walisigina katiba.
Achaneni na vigezo na taaluma ya Said Kubenea. Hivo ni vigezo vilivyo wekwa na watufulani ili iwe vigumu kuhalalisha hiyo habari. Walio weka hizo W5+H nawashangaa sana. Kwa nini mimi pia nisitunikiwe shahada ya uzambivu (PHD) kwa kuchunga mbuzi kwa miaka saba kabla sijaanza masomo? au ndo tusubiri vigezo vya wazungu.....
Said Kubenea kaza buti, kazi yako tunaiheshimu na tutazidi kukumbuka wakifungia Mwanahalisi tutaanzisha jingine la MWANAUWAZI
.
 
1. Mathias Byabato umefanya vema kuwafafanulia kuhusu 5W + H. Lakini umesahao W moja ni WHY. Pia uandishi huo wa kufuata formula hiyo ni uandishi tunaouita TRADITION na uandishi wa sasa haulazimishi sana kufuata 5W + H badala yake unaweza ukachukua W + H na habari yako ikawa na impact kubwa zaidi kuliko 5W. W ninayoizungumzia hapa no WHY na H ni HOW. Hizi zinatosha sana kuchimba issue na kuiweka kwenye jamii kwamba kwanini iko hivyo na kwa namna gani iko hivyo na impact yako ipo kwa namna gani.

2. Swala la waziri kufungia gazeti hili hata kama limeingilia uhuru wa mahakama halipo. Isipokuwa ni swala la mahakama yenyewe kueleza kuwa Mwanahalisi limeingilia uhuru wa mahakama na kisha mahakama husika ichukue hatua dhidi ya Gazeti Mwanahalisi na wala sio jukumu la Waziri wa sheria ama waziri wa Habari. Wakichukua hatua mawaziri hao nao watakuwa wamekiuka katiba ibara ya 18 inayohusu Freedom of expression.

3. Asanteni na naomba kutoa hoja!!
 
Aliyeandika hakukurupuka,we usiye na taaluma ya habari unakurupuka na kuchonga,ulitaka afiche ukweli?bug up sana mwanahalisi.
 
Kwa umafia wa nchi hii, sitashangaa hili gazeti likufungiwa kwa sababu ya kuweka ukweli hadharani....
 
Nkurukumbi, nkurukumbi, niyo yazaile mayenjeeeeeeeeeeeeeeeee, otalitela, otalijumaaaaaaaa, niyo yazaaile mayenjeeeeeeeeeeee......... aghhhhhhhh....... inabidi tuimbe kilugha. We Jeykey utakuwa kama Kombani na Werema. Walisema katiba ibaki kama ilivyo, president au boss wao akasema ifanyiwe mabadiriko sasa na wewe utachongaaaaaaaa alafu gazeti liaendelea kupeta.

Umenikumbusha mbali sana maana nilienda kumtembelea rafiki yangu alikuwa anasoma Ihungo nikakutana na watoto wanaimba huo wimbo.
 
kwani kuna ushahidi uliotolewa?

Mhe kombani atafanya kazi yake kwa gazeti hili , hii itakuwa FUNDISHO KWA MAGAZETI MENGINE

ina maana jeykey unafurahi na kuomba mwanahalisi lifungiwe???sijakusikia ukikashifu al-nuur kwa kutoa mafuvu ya kichwa front page eti chadema italeta haya...we umeguswa tu na mwahahalisi kumgusa mkapa....viva forever
 
Gazeti la mwanahalisi linastahili tuzo jamani,lipo huru kutupa ukweli muda wote. Mafisadi naona hawalali ikifikaga jumanne
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom